< Yeremia 23 >

1 “Ole wao wachungaji wanaoharibu na kutawanya kondoo wa malisho yangu!” asema Bwana.
"Woe to the shepherds who destroy and scatter the sheep of my pasture." says Jehovah.
2 Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, analowaambia wachungaji wanaowachunga watu wangu: “Kwa sababu mmelitawanya kundi langu na kuwafukuzia mbali, wala hamkuwatunza, basi mimi nitawaadhibu kwa ajili ya uovu mliofanya,” asema Bwana.
Therefore thus says Jehovah, the God of Israel, against the shepherds who feed my people: "You have scattered my flock, and driven them away, and have not visited them; look, I will visit on you the evil of your doings," says Jehovah.
3 “Mimi mwenyewe nitayakusanya mabaki ya kundi langu kutoka nchi zote ambazo nimewafukuzia, nami nitawarudisha katika malisho yao, mahali ambapo watazaa na kuongezeka idadi yao.
"I will gather the remnant of my flock out of all the countries where I have driven them, and will bring them again to their folds; and they shall be fruitful and multiply.
4 Nitaweka wachungaji juu yao ambao watawachunga, nao hawataogopa tena au kutishwa, wala hatapotea hata mmoja,” asema Bwana.
I will set up shepherds over them, who shall feed them; and they shall fear no more, nor be dismayed, neither shall any be lacking," says Jehovah.
5 Bwana asema, “Siku zinakuja, nitakapomwinulia Daudi Tawi lenye haki, Mfalme atakayetawala kwa hekima, na kutenda lililo haki na sawa katika nchi.
"Look, the days come," says Jehovah, "that I will raise to David a righteous Branch, and he shall reign as king and deal wisely, and shall execute justice and righteousness in the land.
6 Katika siku zake, Yuda ataokolewa na Israeli ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.
In his days Judah shall be saved, and Israel shall dwell safely; and this is his name by which he shall be called: 'Jehovah our righteousness.'
7 “Hivyo basi, siku zinakuja, wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
Therefore look, the days come," says Jehovah, "that they shall no more say, 'As Jehovah lives, who brought up the children of Israel out of the land of Egypt';
8 bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wazao wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia,’ asema Bwana. Ndipo wataishi katika nchi yao wenyewe.”
but, 'As Jehovah lives, who brought up and who led the descendants of the house of Israel out of the north country, and from all the countries where he had driven them.' They shall dwell in their own land."'
9 Kuhusu manabii: Moyo wangu umevunjika ndani yangu; mifupa yangu yote inatetemeka. Nimekuwa kama mtu aliyelewa, kama mtu aliyelemewa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
Concerning the prophets: My heart within me is broken, all my bones shake; I am like a drunken man, and like a man whom wine has overcome, because of Jehovah, and because of his holy words.
10 Nchi imejaa wazinzi; kwa sababu ya laana, nchi imekauka na malisho yaliyoko nyikani yamekauka. Mwenendo wa manabii ni mbaya na mamlaka yao si ya haki.
For the land is full of adulterers; for because of swearing the land mourns; the pastures of the wilderness are dried up. "Their course is evil, and their might is not right;
11 “Nabii na kuhani wote si wacha Mungu; hata hekaluni mwangu ninaona uovu wao,” asema Bwana.
for both prophet and priest are profane; yes, in my house have I found their wickedness," says Jehovah.
12 “Kwa hiyo mapito yao yatakuwa utelezi, watafukuziwa mbali gizani na huko wataanguka. Nitaleta maafa juu yao katika mwaka wa kuadhibiwa kwao,” asema Bwana.
"Therefore their way shall be to them as slippery places in the darkness: they shall be driven on, and fall in it; for I will bring evil on them, even the year of their visitation," says Jehovah.
13 “Miongoni mwa manabii wa Samaria nililiona jambo la kuchukiza: Walitabiri kwa Baali na kuwapotosha Israeli watu wangu.
"I have seen folly in the prophets of Samaria; they prophesied by Baal, and caused my people Israel to err.
14 Nako miongoni mwa manabii wa Yerusalemu nimeona jambo baya sana: Wanafanya uzinzi na kuenenda katika uongo. Wanatia nguvu mikono ya watenda mabaya, kwa ajili hiyo hakuna yeyote anayeachana na uovu wake. Wote wako kama Sodoma kwangu; watu na Yerusalemu wako kama Gomora.”
In the prophets of Jerusalem also I have seen a horrible thing: they commit adultery, and walk in lies; and they strengthen the hands of evildoers, so that none does return from his wickedness: they are all of them become to me as Sodom, and its inhabitants as Gomorrah.
15 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo kuhusu manabii: “Nitawafanya wale chakula kichungu na kunywa maji yaliyotiwa sumu, kwa sababu kutokana na manabii wa Yerusalemu kutokumcha Mungu kumeenea katika nchi yote.”
Therefore thus says Jehovah of hosts concerning the prophets: 'Look, I will feed them with wormwood, and make them drink the water of gall; for from the prophets of Jerusalem is ungodliness gone forth into all the land.'
16 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Msisikilize wanachowatabiria manabii, wanawajaza matumaini ya uongo. Wanasema maono kutoka akili zao wenyewe, hayatoki katika kinywa cha Bwana.
Thus says Jehovah of hosts, 'Do not listen to the words of the prophets who prophesy to you: they teach you vanity; they speak a vision of their own heart, and not out of the mouth of Jehovah.
17 Huendelea kuwaambia wale wanaonidharau mimi, ‘Bwana asema: Mtakuwa na amani.’ Kwa wale wote wafuatao ugumu wa mioyo yao, wao husema, ‘Hakuna dhara litakalowapata.’
They say continually to those who despise me, "Jehovah has said, 'You shall have peace'"; and to everyone who walks in the stubbornness of his own heart they say, "No evil shall come on you."
18 Lakini ni yupi miongoni mwao aliyesimama katika baraza la Bwana ili kuona au kusikia neno lake? Ni nani aliyesikiliza na kusikia neno lake?
For who has stood in the council of Jehovah, that he should perceive and hear his word? Who has marked my word, and heard it?
19 Tazama, dhoruba ya Bwana itapasuka kwa ghadhabu, kisulisuli kitazunguka na kuanguka vichwani vya waovu.
Look, the storm of Jehovah, his wrath, has gone forth. Yes, a whirling storm. It shall burst on the head of the wicked.
20 Hasira ya Bwana haitageuka mpaka amelitimiza kusudi la moyo wake. Siku zijazo mtalifahamu kwa wazi.
The anger of Jehovah shall not return, until he has executed, and until he have performed the intents of his heart: in the latter days you shall understand it perfectly.
21 Mimi sikuwatuma manabii hawa, lakini bado wamekimbia wakitangaza ujumbe wao. Mimi sikusema nao, lakini wametabiri.
I sent not these prophets, yet they ran: I did not speak to them, yet they prophesied.
22 Lakini kama wangesimama barazani mwangu, wangetangaza maneno yangu kwa watu wangu, nao wangewageuza kutoka njia zao mbaya na kutoka matendo yao maovu.”
But if they had stood in my council, then had they caused my people to hear my words, and had turned them from their evil way, and from the evil of their doings.
23 “Je, mimi ni Mungu aliyeko hapa karibu tu,” Bwana asema, “wala si Mungu aliyeko pia mbali?
Am I a God at hand,' says Jehovah, 'and not a God afar off?
24 Je, mtu yeyote aweza kujificha mahali pa siri ili nisiweze kumwona?” Bwana asema. “Je, mimi sikuijaza mbingu na nchi?” Bwana asema.
Can any hide himself in secret places so that I shall not see him?' says Jehovah. 'Do I not fill heaven and earth?' says Jehovah.
25 “Nimesikia wanayoyasema manabii, hao wanaotabiri uongo kwa jina langu. Wanasema, ‘Nimeota ndoto! Nimeota ndoto!’
'I have heard what the prophets have said, who prophesy lies in my name, saying, "I have dreamed, I have dreamed."
26 Mambo haya yataendelea mpaka lini ndani ya mioyo ya hawa manabii wa uongo, ambao hutabiri maono ya uongo ya akili zao wenyewe?
How long shall this be in the heart of the prophets who prophesy lies, even the prophets of the deceit of their own heart,
27 Wanadhani ndoto wanazoambiana wao kwa wao zitawafanya watu wangu walisahau jina langu, kama baba zao walivyolisahau jina langu kwa kumwabudu Baali.
who think to cause my people to forget my name by their dreams which they tell every man to his neighbor, as their fathers forgot my name for Baal.
28 Mwache nabii aliye na ndoto aseme ndoto yake, lakini yule aliye na neno langu na aliseme kwa uaminifu. Kwa maana jani kavu lina uhusiano gani na ngano?” asema Bwana.
The prophet who has a dream, let him tell a dream; and he who has my word, let him speak my word faithfully. What is the straw to the wheat?' says Jehovah.
29 “Je, neno langu si kama moto,” asema Bwana, “na kama nyundo ivunjayo mwamba vipande vipande?
'Isn't my word like fire?' says Jehovah; 'and like a hammer that breaks the rock in pieces?
30 “Kwa hiyo, niko kinyume na manabii wanaoibiana maneno kana kwamba ni yangu,” asema Bwana.
Therefore look, I am against the prophets,' says Jehovah, 'who steal my words everyone from his neighbor.
31 “Naam, mimi niko kinyume na manabii wanaotikisa ndimi zao wenyewe na kusema, ‘Bwana asema.’
Look, I am against the prophets,' says Jehovah, 'who use their tongues, and say, "He says."
32 Kweli, niko kinyume na hao wanaotabiri ndoto za uongo,” asema Bwana. “Wanazisimulia na kuwapotosha watu wangu kwa uongo wao bila kujali, lakini sikuwatuma wala sikuwaamuru. Hawawafaidi watu hawa hata kidogo,” asema Bwana.
Look, I am against the prophets who prophesy lying dreams,' says Jehovah, 'and do tell them, and cause my people to err by their lies, and by their vain boasting: yet I did not send them, nor commanded them; neither do they profit this people at all,' says Jehovah.
33 “Wakati watu hawa, au nabii, au kuhani watakapokuuliza, ‘Mzigo wa Bwana ni nini?’ wewe utawaambia, ‘Ninyi ndio mzigo. Nami nitawavua kama vazi, asema Bwana.’
'When this people, or the prophet, or a priest, shall ask you, saying, "What is the burden of Jehovah?" Then you shall tell them, "You are the burden, and I will cast you off," says Jehovah.
34 Nabii, kuhani, au mtu yeyote akisema, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ nitamwadhibu huyo na nyumba yake.
As for the prophet, and the priest, and the people, who shall say, "The burden of Jehovah," I will even punish that man and his house.
35 Hivyo mnaambiana kila mmoja na mwenzake, au kwa mtu wa nyumba yao: ‘Bwana amejibu nini?’ au ‘Bwana amesema nini?’
You shall say everyone to his neighbor, and everyone to his brother, "What has Jehovah answered?" and, "What has Jehovah spoken?"
36 Lakini kamwe msiseme tena, ‘Nina mzigo wa Bwana,’ kwa sababu kila neno la mtu binafsi linakuwa mzigo wake mwenyewe, na hivyo kupotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wetu.
You shall mention the burden of Jehovah no more: for every man's own word shall be his burden; for you have perverted the words of the living God, of Jehovah of hosts our God.
37 Hivi ndivyo utakavyoendelea kumuuliza nabii: ‘Bwana amekujibu nini?’ au ‘Je, Bwana amesema nini?’
You shall say to the prophet, "What has Jehovah answered you?" and, "What has Jehovah spoken?"
38 Ingawa unadai, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hili ndilo Bwana asemalo: Ulitumia maneno, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hata ingawa nilikuambia kuwa kamwe usiseme, ‘Huu ni mzigo wa Bwana.’
But if you say, "The burden of Jehovah"; therefore thus says Jehovah: Because you say this word, "The burden of Jehovah," and I have sent to you, saying, "You shall not say, 'The burden of Jehovah'";
39 Kwa hiyo, hakika nitakusahau na kukutupa mbali na uso wangu pamoja na mji niliowapa ninyi na baba zenu.
therefore, look, I will surely lift you up and I will cast you off, and the city that I gave to you and to your fathers, away from my presence:
40 Nitaleta juu yako fedheha ya kudumu: yaani aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”
and I will bring an everlasting reproach on you, and a perpetual shame, which shall not be forgotten.'"

< Yeremia 23 >