< Yeremia 18 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
Cette parole fut [adressée] de par l'Eternel à Jérémie, disant:
2 “Shuka uende mpaka nyumba ya mfinyanzi, nami huko nitakupa ujumbe wangu.”
Lève-toi, et descends dans la maison d'un potier, et là je te ferai entendre mes paroles.
3 Kwa hiyo nikashuka mpaka kwenye nyumba ya mfinyanzi, nikamkuta akifinyanga kwa gurudumu lake.
Je descendis donc dans la maison d'un potier, et voici, il faisait son ouvrage, assis sur sa selle.
4 Lakini chombo alichokuwa akikifinyanga kutokana na udongo kilivunjika mikononi mwake, hivyo mfinyanzi akakifanya kuwa chombo kingine, umbo jingine kama vile ilivyoonekana vyema kwake yeye.
Et le vase qu'il faisait de l'argile qui [était] en sa main, fut gâté, et il en fit encore un autre vase, comme il lui sembla bon de [le] faire.
5 Kisha neno la Bwana likanijia kusema:
Alors la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
6 “Ee nyumba ya Israeli, je, siwezi kuwafanyia kama huyu mfinyanzi afanyavyo?” asema Bwana. “Kama vile udongo ulivyo katika mikono ya mfinyanzi, ndivyo mlivyo katika mkono wangu, ee nyumba ya Israeli.
Maison d'Israël, ne vous pourrai-je pas faire comme a fait ce potier; dit l'Eternel? voici, comme l'argile est dans la main d'un potier, ainsi êtes-vous dans ma main, maison d'Israël.
7 Ikiwa wakati wowote nikitangaza kuwa taifa au ufalme utangʼolewa, utaangushwa na kuangamizwa,
En un instant je parlerai contre une nation, et contre un Royaume, pour arracher, pour démolir, et pour détruire;
8 ikiwa lile taifa nililolionya litatubia uovu wake, ndipo nitakapokuwa na huruma, wala sitawapiga kwa maafa niliyokuwa nimewakusudia.
Mais si cette nation contre laquelle j'aurai parlé se détourne du mal qu'elle aura fait, je me repentirai aussi du mal que j'avais pensé de lui faire.
9 Ikiwa wakati mwingine nitatangaza kuwa taifa ama utawala ujengwe na kuwekwa wakfu,
Et si en un instant je parle d'une nation et d'un Royaume, pour l'édifier et pour le planter;
10 ikiwa utafanya maovu mbele zangu na hukunitii, ndipo nitakapoghairi makusudio yangu mema niliyokuwa nimeyakusudia.
Et que cette nation fasse ce qui me déplaît, en sorte qu'elle n'écoute point ma voix, je me repentirai aussi du bien que j'avais dit que je lui ferais.
11 “Basi kwa hiyo waambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Tazama! Ninaandaa maafa kwa ajili yenu, nami ninabuni mabaya dhidi yenu. Kwa hiyo geukeni kutoka njia zenu mbaya, kila mmoja wenu, tengenezeni njia zenu na matendo yenu.’
Or donc parle maintenant aux hommes de Juda, et aux habitants de Jérusalem, en disant: ainsi a dit l'Eternel: voici, je projette du mal contre vous, et je forme un dessein contre vous; abandonnez donc maintenant chacun sa mauvaise voie, et changez votre voie, et vos actions.
12 Lakini wao watajibu, ‘Hakuna faida. Tutaendelea na mipango yetu wenyewe, kila mmoja wetu atafuata ukaidi wa moyo wake mbaya.’”
Et ils répondirent: il n'y a plus d'espérance; c'est pourquoi nous suivrons nos pensées, et chacun de nous fera selon la dureté de son cœur mauvais.
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “Ulizia miongoni mwa mataifa: Ni nani alishasikia jambo kama hili? Jambo la kutisha sana limefanywa na Bikira Israeli.
C'est pourquoi ainsi a dit l'Eternel: Demandez maintenant aux nations qui a entendu de telles choses? la vierge d'Israël a fait une chose très-énorme.
14 Je, barafu ya Lebanoni iliwahi kutoweka kwenye miteremko yake ya mawe wakati wowote? Je, maji yake baridi yatokayo katika vyanzo vilivyo mbali yaliwahi kukoma kutiririka wakati wowote?
N'abandonnera-t-on pas la neige du Liban pour la roche du champ? et ne laissera-t-on pas les eaux qui ne sont point naturelles, et qui sont froides, [encore] qu'elles coulent?
15 Lakini watu wangu wamenisahau mimi, wanafukizia uvumba sanamu zisizofaa kitu, zilizowafanya wajikwae katika njia zao na katika mapito ya zamani. Zimewafanya wapite kwenye vichochoro na kwenye barabara ambazo hazikujengwa.
Mais mon peuple m'a oublié, et il a fait des parfums à ce qui n'est que vanité, et qui les a fait broncher dans leurs voies, pour [les faire retirer] des sentiers anciens, afin de marcher dans les sentiers d'un chemin qui n'est point battu;
16 Nchi yao itaharibiwa, itakuwa kitu cha kudharauliwa daima; wote wapitao karibu nayo watashangaa na kutikisa vichwa vyao.
Pour faire venir sur leur pays une désolation et un opprobre perpétuel; [tellement que] quiconque passera par là en sera étonné, et branlera la tête.
17 Kama upepo utokao mashariki, nitawatawanya mbele ya adui zao; nitawapa kisogo wala sio uso, katika siku ya maafa yao.”
Je les disperserai devant l'ennemi, comme par le vent d'Orient; je leur tournerai le dos, au jour de leur calamité.
18 Wakasema, “Njooni, tutunge hila dhidi ya Yeremia; kwa kuwa kufundisha sheria kwa kuhani hakutapotea, wala shauri litokalo kwa mwenye hekima, wala neno la manabii. Hivyo njooni, tumshambulie kwa ndimi zetu na tusijali chochote asemacho.”
Et ils ont dit: venez, et faisons quelques machinations contre Jérémie; car la Loi ne se perdra pas chez le Sacrificateur, ni le conseil chez le Sage, ni la parole chez le Prophète; venez, et frappons-le de la langue, et ne soyons point attentifs à aucun de ses discours.
19 Nisikilize, Ee Bwana, sikia wanayosema washtaki wangu!
Eternel, entends-moi, et écoute la voix de ceux qui plaident contre moi.
20 Je, mema yalipwe kwa mabaya? Lakini wao wamenichimbia shimo. Kumbuka kwamba nilisimama mbele yako na kunena mema kwa ajili yao, ili wewe ugeuze hasira yako kali mbali nao.
Le mal sera-t-il rendu pour le bien? car ils ont creusé une fosse pour mon âme. Souviens-toi que je me suis présenté devant toi afin de parler pour leur bien, [et] afin de détourner d'eux ta grande colère.
21 Kwa hiyo uwaache watoto wao waone njaa; uwaache wauawe kwa makali ya upanga. Wake zao wasiwe na watoto, na wawe wajane; waume wao wauawe, nao vijana wao waume wachinjwe kwa upanga vitani.
C'est pourquoi livre leurs enfants à la famine, et fais couler leur sang à coups d'épée; que leurs femmes soient privées d'enfants, et veuves, et que leurs maris soient mis à mort; et leurs jeunes gens tués avec l'épée dans la bataille.
22 Kilio na kisikike kutoka kwenye nyumba zao ghafula uwaletapo adui dhidi yao, kwa kuwa wamechimba shimo ili kunikamata na wameitegea miguu yangu mitego.
Que le cri soit ouï de leurs maisons, quand tu auras fait venir subitement des troupes contre eux; parce qu'ils ont creusé une fosse pour me prendre, et qu'ils ont tendu des filets à mes pieds.
23 Lakini unajua, Ee Bwana, hila zao zote za kuniua. Usiyasamehe makosa yao wala usifute dhambi zao mbele za macho yako. Wao na waangamizwe mbele zako; uwashughulikie wakati wa hasira yako.
Or tu sais, ô Eternel! que tout leur conseil est contre moi pour me mettre à mort; ne sois point apaisé à l'égard de leur iniquité, et n'efface point leur péché de devant ta face, mais qu'on les fasse tomber en ta présence; agis contre eux au temps de ta colère.

< Yeremia 18 >