< Yeremia 17 >

1 “Dhambi ya Yuda imechorwa kwa kalamu ya chuma, imeandikwa kwa ncha ya almasi, kwenye vibao vya mioyo yao na kwenye pembe za madhabahu zao.
The sin of Judah is inscribed with an iron stylus, engraved with an adamant point, on their minds and on corners of their altars where they worship.
2 Hata watoto wao wanakumbuka madhabahu zao na nguzo za Ashera, kandokando ya miti iliyotanda na juu ya vilima virefu.
Even their children remember to worship at their pagan altars and Asherah poles, set up by the green trees and on the high hills,
3 Mlima wangu katika nchi pamoja na utajiri na hazina zako zote nitazitoa ziwe nyara, pamoja na mahali pako pa juu pa kuabudia miungu kwa sababu ya dhambi katika nchi yako yote.
on my mountain in the fields. I will hand over your wealth and all your valuable possessions as plunder, because of the sin committed on your pagan high places inside your country.
4 Kwa kosa lako mwenyewe utaupoteza urithi niliokupa. Nitakufanya mtumwa wa adui zako katika nchi usiyoijua, kwa kuwa umeiwasha hasira yangu, nayo itawaka milele.”
You will have to give up the land I gave you. I will have your enemies make you their slaves in an unfamiliar country for you made my anger blaze, and it will burn forever.
5 Hili ndilo asemalo Bwana: “Amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu, ategemeaye mwenye mwili kwa ajili ya nguvu zake, ambaye moyo wake umemwacha Bwana.
This is what the Lord says: Cursed are those who put their confidence in human beings, who trust in human strength and give up relying on the Lord.
6 Atakuwa kama kichaka cha jangwani; hataona mafanikio yatakapokuja. Ataishi katika sehemu zisizo na maji, katika nchi ya chumvi ambapo hakuna yeyote aishiye humo.
They will be like a shrub alone in the desert that isn't even aware when good things happen. It just goes on living in the dry desert, in a salt flat that's uninhabited.
7 “Lakini amebarikiwa mtu ambaye tumaini lake ni katika Bwana, ambaye matumaini yake ni katika Bwana.
Blessed are those who trust in the Lord, who put their confidence in him.
8 Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji. Hauogopi wakati wa joto ujapo; majani yake ni mabichi daima. Hauna hofu katika mwaka wa ukame na hautaacha kuzaa matunda.”
They are like trees planted by water, sending out roots toward the stream. They don't panic when it gets hot; their leaves are always green. They don't worry during a time of drought—they go on producing fruit.
9 Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote, ni mwovu kupita kiasi. Ni nani awezaye kuujua?
The mind is more deceptive than anything else—it's incurably sick! Who can possibly understand it?
10 “Mimi Bwana huchunguza moyo na kuzijaribu nia, ili kumlipa mtu kwa kadiri ya mwenendo wake, kwa kadiri ya matendo yake yanavyostahili.”
But I, the Lord, see what people are thinking. I examine their minds, so I can reward them depending on their attitudes and the way they behave.
11 Kama kware aanguaye mayai asiyoyataga, ndivyo alivyo mtu apataye mali kwa njia zisizo za haki. Maisha yake yafikapo katikati, siku zitamwacha, na mwishoni atabainika kuwa mpumbavu.
Like a partridge hatching eggs it didn't lay is someone who makes a fortune by cheating others. Their riches will fly away at midday, and in the end they'll look like a fool.
12 Kiti cha enzi kilichotukuzwa, kilichoinuliwa tangu mwanzo, ndiyo sehemu yetu ya mahali patakatifu.
Our Temple is a throne of glory, raised up high from the beginning.
13 Ee Bwana, uliye tumaini la Israeli, wote wakuachao wataaibika. Wale wanaogeukia mbali nawe wataandikwa mavumbini kwa sababu wamemwacha Bwana, chemchemi ya maji yaliyo hai.
Lord, you are Israel's hope, anyone who deserts you will be disgraced. Anyone who turns their back on you will vanish like names written in the dust, for they have abandoned the Lord, the source of living water.
14 Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe nami nitaokoka, kwa maana wewe ndiwe ninayekusifu.
Please heal me, Lord, and I'll be healed; save me, and I'll be saved, for you are the one I praise.
15 Wao huendelea kuniambia, “Liko wapi neno la Bwana? Sasa na litimie!”
See how they keep on saying to me, “Where is the disaster that the Lord's predicted? Is it ever going to happen?”
16 Sijakukimbia na kuacha kuwa mchungaji wako; unajua sijaitamani siku ya kukata tamaa. Kile kipitacho midomoni mwangu ki wazi mbele yako.
But I haven't been in a hurry to give up being your shepherd. I haven't wanted the time of trouble to come. You know that whatever I said was said in front of you.
17 Usiwe kwangu kitu cha kunitia hofu kuu; wewe ndiwe kimbilio langu katika siku ya maafa.
Please don't be the one who terrifies me! You are my protection in the time of trouble.
18 Watesi wangu na waaibishwe, lakini nilinde mimi nisiaibike; wao na watiwe hofu kuu, lakini unilinde mimi na hofu kuu. Waletee siku ya maafa; waangamize kwa maangamizi maradufu.
Bring shame on my persecutors, but not on me. Terrify them, but not me, Let them experience the time of trouble, and smash them to pieces.
19 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ukasimame kwenye lango la watu, mahali ambako wafalme wa Yuda huingilia na kutokea, simama pia kwenye malango mengine yote ya Yerusalemu.
This is what the Lord told me: Go and stand at the main gate of the city, the one used by kings of Judah, and do the same at all the other gates of Jerusalem.
20 Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda, nanyi watu wote wa Yuda, na kila mmoja aishiye Yerusalemu apitaye katika malango haya.
Tell them, Listen to the Lord's message, kings of Judah, and all you people of Judah and Jerusalem who come in through these gates.
21 Hili ndilo asemalo Bwana: Jihadharini msije mkabeba mzigo siku ya Sabato, wala kuingiza mzigo kupitia malango ya Yerusalemu.
This is what the Lord says: Pay attention, if you value your lives! Don't carry a load on the Sabbath day, and don't bring it through the gates of Jerusalem.
22 Msitoe mizigo nje ya nyumba zenu wala kufanya kazi yoyote wakati wa Sabato, lakini itakaseni siku ya Sabato, kama nilivyowaamuru baba zenu.
Don't carry a load out of your houses, and don't do any work on the Sabbath day. Keep the Sabbath day holy, just as I ordered your forefathers.
23 Hata hivyo hawakusikiliza wala kujali, walishupaza shingo zao, na hawakutaka kusikia wala kukubali adhabu.
However, they refused to listen or pay attention. Instead they were stubborn and refused to obey or accept instruction.
24 Lakini mkiwa waangalifu kunitii, asema Bwana, nanyi msipoleta mzigo wowote kupitia malango ya mji huu wakati wa Sabato, lakini mkaitakasa siku ya Sabato kwa kutofanya kazi siku hiyo,
Listen carefully to me, says the Lord, and don't bring any load through the gates of this city on the Sabbath day, and keep the Sabbath day holy, and don't do any work on it.
25 ndipo wafalme wakaao juu ya kiti cha enzi cha Daudi wataingia kupitia malango ya mji huu, pamoja na maafisa wao. Wao na maafisa wao watakuja wakiwa wamepanda magari na farasi, wakiandamana na watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, nao mji huu utakaliwa na watu daima.
Then kings and princes will enter through the gates of this city. They will sit on the throne of David. They will ride in chariots and on horses with their officials, accompanied by the people of Judah and those living in Jerusalem, and this city will be inhabited forever.
26 Watu watakuja kutoka miji ya Yuda na vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, kutoka nchi ya Benyamini na chini ya vilima vya magharibi, kutoka nchi ya vilima na Negebu, wakileta sadaka za kuteketezwa na dhabihu, sadaka za nafaka, uvumba na sadaka za shukrani kwenye nyumba ya Bwana.
People will come from the towns of Judah and everywhere around Jerusalem, from the land of Benjamin, and from the lowlands the hill country, and the Negev. They will bring burnt offerings and sacrifices, grain offerings and frankincense, and thank offerings to the Lord's Temple.
27 Lakini ikiwa hamtanitii mimi kwa kuitakasa Sabato na kwa kutochukua mzigo wowote mnapoingia katika malango ya Yerusalemu wakati wa Sabato, basi nitawasha moto usiozimika katika malango ya Yerusalemu utakaoteketeza ngome zake.’”
But if you refuse to listen to me and keep the Sabbath day holy by not carrying a load while entering the gates of Jerusalem on the Sabbath day, then I will set its gates alight with a fire that can't be put out, and it will burn down Jerusalem's fortresses.

< Yeremia 17 >