< Yeremia 13 >

1 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ununue mkanda wa kitani, ujivike kiunoni mwako, lakini usiuache uguse maji.”
Ainsi m'a dit l'Éternel: Va, achète-toi une ceinture de lin, et mets-la sur tes reins; mais ne la trempe pas dans l'eau.
2 Kwa hiyo nikanunua mkanda, kama Bwana alivyoniagiza, nikajivika kiunoni.
J'achetai donc la ceinture, suivant la parole de l'Éternel, et je la mis sur mes reins.
3 Ndipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili:
Et la parole de l'Éternel me fut adressée une seconde fois, en disant:
4 “Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.”
Prends la ceinture que tu as achetée, et qui est sur tes reins; lève-toi, va-t'en vers l'Euphrate, et là, cache-la dans la fente d'un rocher.
5 Ndipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.
J'allai donc et je la cachai près de l'Euphrate, comme l'Éternel me l'avait commandé.
6 Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”
Et il arriva, plusieurs jours après, que l'Éternel me dit: Lève-toi, va vers l'Euphrate, et reprends la ceinture que je t'avais commandé d'y cacher.
7 Hivyo nikaenda Frati na kuuchimbua ule mkanda kutoka pale nilipokuwa nimeuficha, lakini sasa ulikuwa umeharibika na haufai tena kabisa.
Et j'allai vers l'Euphrate, et je creusai, et je pris la ceinture du lieu où je l'avais cachée, mais voici, la ceinture était gâtée; elle n'était plus bonne à rien.
8 Ndipo neno la Bwana likanijia:
Et la parole de l'Éternel me fut adressée, en disant:
9 “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Vivyo hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikuu cha Yerusalemu.
Ainsi a dit l'Éternel: C'est ainsi que je gâterai l'orgueil de Juda, le grand orgueil de Jérusalem.
10 Watu hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wafuatao ukaidi wa mioyo yao na kufuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu, watakuwa kama mkanda huu ambao haufai kabisa!
Ce peuple de méchants, qui refusent d'écouter mes paroles, et qui marchent suivant la dureté de leur cœur, et qui vont après d'autres dieux pour les servir et pour se prosterner devant eux, il sera comme cette ceinture qui n'est plus bonne à rien.
11 Kwa maana kama vile mkanda ufungwavyo kiunoni mwa mtu, ndivyo nilivyojifunga nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda,’ asema Bwana, ‘ili wawe watu wangu kwa ajili ya utukufu wangu, sifa na heshima yangu. Lakini hawajasikiliza.’
Car, comme on attache la ceinture aux reins d'un homme, ainsi je m'étais attaché toute la maison d'Israël et toute la maison de Juda, dit l'Éternel, afin qu'elles fussent mon peuple, mon renom, ma louange et ma gloire; mais ils ne m'ont point écouté.
12 “Waambie: ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo.’ Kama wao wakikuambia, ‘Kwani hatujui kwamba kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo?’
Tu leur diras donc cette parole: Ainsi a dit l'Éternel, le Dieu d'Israël: Tout vase à vin se remplit de vin. Et ils te diront: Ne savons-nous pas bien que tout vase à vin se remplit de vin?
13 Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: nitawajaza ulevi wote waishio katika nchi hii, pamoja na wafalme waketio juu ya kiti cha enzi cha Daudi, makuhani, manabii na wale wote waishio Yerusalemu.
Mais tu leur diras: Ainsi a dit l'Éternel: Voici, je vais remplir d'ivresse tous les habitants de ce pays, les rois qui sont assis sur le trône de David, les sacrificateurs, les prophètes et tous les habitants de Jérusalem.
14 Nitawagonganisha kila mmoja na mwenzake, baba na wana wao, asema Bwana. Sitawarehemu wala kuwahurumia ili niache kuwaangamiza.’”
Et je les briserai les uns contre les autres, les pères et les fils ensemble, dit l'Éternel; je n'épargnerai pas; je n'aurai ni pitié, ni miséricorde; rien ne m'empêchera de les détruire.
15 Sikieni na mzingatie, msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amenena.
Écoutez et prêtez l'oreille; ne vous élevez point, car l'Éternel a parlé.
16 Mpeni utukufu Bwana Mungu wenu, kabla hajaleta giza, kabla miguu yenu haijajikwaa juu ya vilima vitakavyotiwa giza. Mlitarajia nuru, lakini ataifanya kuwa giza nene na kuibadili kuwa huzuni kubwa.
Donnez gloire à l'Éternel, votre Dieu, avant qu'il fasse venir les ténèbres, avant que vos pieds heurtent contre les montagnes obscures; vous attendrez la lumière, et il la changera en ombre de la mort, il la réduira en obscurité profonde.
17 Lakini kama hamtasikiliza, nitalia sirini kwa ajili ya kiburi chenu; macho yangu yatalia kwa uchungu, yakitiririka machozi, kwa sababu kundi la kondoo la Bwana litachukuliwa mateka.
Si vous n'écoutez point ceci, mon âme pleurera en secret à cause de votre orgueil; mon œil pleurera, il se fondra en larmes, parce que le troupeau de l'Éternel sera emmené captif.
18 Mwambie mfalme na mamaye, “Shukeni kutoka kwenye viti vyenu vya enzi, kwa kuwa taji zenu za utukufu zitaanguka kutoka vichwani mwenu.”
Dis au roi et à la reine: Asseyez-vous bien bas! Car elle est tombée de vos têtes, la couronne de votre gloire!
19 Miji iliyoko Negebu itafungwa, wala hapatakuwa na mtu wa kuifungua. Watu wa Yuda wote watapelekwa uhamishoni, wakichukuliwa kabisa waende mbali.
Les villes du Midi sont fermées, il n'y a personne qui les ouvre; tout Juda est transporté, transporté entièrement.
20 Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini. Liko wapi lile kundi ulilokabidhiwa, kondoo wale uliojivunia?
Lève tes yeux! Vois ceux qui viennent du Nord. Où est le troupeau qui t'a été donné, où sont les brebis qui faisaient ta gloire?
21 Utasema nini Bwana atakapowaweka juu yako wale ulioungana nao kama marafiki wako maalum? Je, hutapatwa na utungu kama mwanamke aliye katika utungu wa kuzaa?
Que diras-tu de ce qu'il te châtie? C'est toi-même qui leur as appris à dominer en maîtres sur toi. Les douleurs ne te saisiront-elles pas, comme la femme qui enfante?
22 Nawe kama ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi ndipo marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.
Et si tu dis en ton cœur: Pourquoi cela m'arrive-t-il? C'est à cause de la grandeur de ton iniquité, que les pans de tes habits sont relevés, et que tes talons sont maltraités.
23 Je, Mkushi aweza kubadili ngozi yake au chui kubadili madoadoa yake? Vivyo hivyo nawe huwezi kufanya mema wewe uliyezoea kutenda mabaya.
Un more changerait-il sa peau, ou un léopard ses taches? Alors aussi vous pourriez faire le bien, vous qui êtes dressés à faire le mal.
24 “Nitawatawanya kama makapi yapeperushwayo na upepo wa jangwani.
Je les disperserai comme du chaume emporté par le vent du désert.
25 Hii ndiyo kura yako, fungu nililokuamuria,” asema Bwana, “kwa sababu umenisahau mimi na kuamini miungu ya uongo.
Tel est ton sort, la portion que je te mesure, dit l'Éternel, parce que tu m'as oublié et que tu as mis ta confiance dans le mensonge.
26 Nitayafunua marinda yako mpaka juu ya uso wako ili aibu yako ionekane:
Moi donc aussi je relèverai tes pans sur ton visage, et ta honte paraîtra.
27 uzinzi wako na kulia kwako kama farasi kulikojaa tamaa, ukahaba wako usio na aibu! Nimeyaona matendo yako ya machukizo juu ya vilima na mashambani. Ole wako, ee Yerusalemu! Utaendelea kuwa najisi mpaka lini?”
Tes adultères et tes hennissements, l'énormité de tes prostitutions sur les collines et dans la campagne, tes abominations, je les ai vues. Malheur à toi, Jérusalem! Combien de temps encore seras-tu impure?

< Yeremia 13 >