< Yeremia 13 >

1 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ununue mkanda wa kitani, ujivike kiunoni mwako, lakini usiuache uguse maji.”
Thus says Jehovah to me, "Go, and buy yourself a linen belt, and put it on your waist, and do not put it in water."
2 Kwa hiyo nikanunua mkanda, kama Bwana alivyoniagiza, nikajivika kiunoni.
So I bought a belt according to the word of Jehovah, and put it on my waist.
3 Ndipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili:
The word of Jehovah came to me the second time, saying,
4 “Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.”
"Take the belt that you have bought, which is on your waist, and arise, go to the Perath, and hide it there in a cleft of the rock."
5 Ndipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.
So I went, and hid it by the Perath, as Jehovah commanded me.
6 Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”
It happened after many days, that Jehovah said to me, "Arise, go to the Perath, and take the belt from there, which I commanded you to hide there."
7 Hivyo nikaenda Frati na kuuchimbua ule mkanda kutoka pale nilipokuwa nimeuficha, lakini sasa ulikuwa umeharibika na haufai tena kabisa.
Then I went to the Perath, and dug, and took the belt from the place where I had hidden it; and look, the belt was marred, it was profitable for nothing.
8 Ndipo neno la Bwana likanijia:
Then the word of Jehovah came to me, saying,
9 “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Vivyo hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikuu cha Yerusalemu.
"Thus says Jehovah, 'In this way I will mar the pride of Judah, and the great pride of Jerusalem.
10 Watu hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wafuatao ukaidi wa mioyo yao na kufuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu, watakuwa kama mkanda huu ambao haufai kabisa!
This evil people, who refuse to hear my words, who walk in the stubbornness of their heart, and are gone after other gods to serve them, and to worship them, shall even be as this belt, which is profitable for nothing.
11 Kwa maana kama vile mkanda ufungwavyo kiunoni mwa mtu, ndivyo nilivyojifunga nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda,’ asema Bwana, ‘ili wawe watu wangu kwa ajili ya utukufu wangu, sifa na heshima yangu. Lakini hawajasikiliza.’
For as the belt clings to the waist of a man, so have I caused to cling to me the whole house of Israel and the whole house of Judah,' says Jehovah; 'that they might be my people, for a name, for praise, and for glory. But they would not listen.
12 “Waambie: ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo.’ Kama wao wakikuambia, ‘Kwani hatujui kwamba kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo?’
Therefore you shall speak to them this word: 'Thus says Jehovah, the God of Israel, "Every jar shall be filled with wine."' And if they shall say to you, 'Do we not certainly know that every jar shall be filled with wine?'
13 Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: nitawajaza ulevi wote waishio katika nchi hii, pamoja na wafalme waketio juu ya kiti cha enzi cha Daudi, makuhani, manabii na wale wote waishio Yerusalemu.
Then you shall tell them, 'Thus says Jehovah, "Look, I will fill all the inhabitants of this land, even the kings who sit on David's throne, and the priests, and the prophets, and all the inhabitants of Jerusalem, with drunkenness.
14 Nitawagonganisha kila mmoja na mwenzake, baba na wana wao, asema Bwana. Sitawarehemu wala kuwahurumia ili niache kuwaangamiza.’”
I will dash them one against another, even the fathers and the sons together, says Jehovah. I will not pity, nor spare, nor have compassion, that I should not destroy them."'"
15 Sikieni na mzingatie, msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amenena.
"Hear, and give ear; do not be proud; for Jehovah has spoken.
16 Mpeni utukufu Bwana Mungu wenu, kabla hajaleta giza, kabla miguu yenu haijajikwaa juu ya vilima vitakavyotiwa giza. Mlitarajia nuru, lakini ataifanya kuwa giza nene na kuibadili kuwa huzuni kubwa.
Give glory to Jehovah your God, before he causes darkness, and before your feet stumble on the dark mountains, and, while you look for light, he turns it into the shadow of death, and makes it gross darkness.
17 Lakini kama hamtasikiliza, nitalia sirini kwa ajili ya kiburi chenu; macho yangu yatalia kwa uchungu, yakitiririka machozi, kwa sababu kundi la kondoo la Bwana litachukuliwa mateka.
But if you will not hear it, my soul shall weep in secret for your pride; and my eye shall weep bitterly, and run down with tears, because Jehovah's flock is taken captive."
18 Mwambie mfalme na mamaye, “Shukeni kutoka kwenye viti vyenu vya enzi, kwa kuwa taji zenu za utukufu zitaanguka kutoka vichwani mwenu.”
"Say to the king and to the queen mother, 'Take a lowly seat, for your glorious crowns have come down from your heads.
19 Miji iliyoko Negebu itafungwa, wala hapatakuwa na mtu wa kuifungua. Watu wa Yuda wote watapelekwa uhamishoni, wakichukuliwa kabisa waende mbali.
The cities toward the Negev are shut, and there is no one to open them: Judah is carried away into exile, all of it; it is wholly carried away into exile.'"
20 Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini. Liko wapi lile kundi ulilokabidhiwa, kondoo wale uliojivunia?
"Lift up your eyes, and see those who come from the north: where is the flock that was given you, your beautiful flock?
21 Utasema nini Bwana atakapowaweka juu yako wale ulioungana nao kama marafiki wako maalum? Je, hutapatwa na utungu kama mwanamke aliye katika utungu wa kuzaa?
What will you say, when he shall set over you as head those whom you have yourself taught to be friends to you? Shall not sorrows take hold of you, as of a woman in travail?
22 Nawe kama ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi ndipo marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.
If you say in your heart, 'Why are these things come on me?' for the greatness of your iniquity are your skirts uncovered, and your heels suffer violence.
23 Je, Mkushi aweza kubadili ngozi yake au chui kubadili madoadoa yake? Vivyo hivyo nawe huwezi kufanya mema wewe uliyezoea kutenda mabaya.
Can the Ethiopian change his skin, or the leopard his spots? Then may you also do good, who are accustomed to do evil.
24 “Nitawatawanya kama makapi yapeperushwayo na upepo wa jangwani.
'therefore I will scatter them, as the stubble that passes away, by the wind of the wilderness.
25 Hii ndiyo kura yako, fungu nililokuamuria,” asema Bwana, “kwa sababu umenisahau mimi na kuamini miungu ya uongo.
This is your lot, the portion measured to you from me,' says Jehovah; 'because you have forgotten me, and trusted in falsehood.
26 Nitayafunua marinda yako mpaka juu ya uso wako ili aibu yako ionekane:
therefore I will also uncover your skirts on your face, and your shame shall appear.
27 uzinzi wako na kulia kwako kama farasi kulikojaa tamaa, ukahaba wako usio na aibu! Nimeyaona matendo yako ya machukizo juu ya vilima na mashambani. Ole wako, ee Yerusalemu! Utaendelea kuwa najisi mpaka lini?”
I have seen your abominations, even your adulteries, and your neighing, the lewdness of your prostitution, on the hills in the field. Woe to you, Jerusalem. You will not be made clean; how long shall it yet be?'"

< Yeremia 13 >