< Isaya 7 >

1 Wakati Ahazi mwana wa Yothamu, mwana wa Uzia, alipokuwa mfalme wa Yuda, Mfalme Resini wa Aramu, na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli walipanda kupigana dhidi ya Yerusalemu, lakini hawakuweza kuushinda.
Or il arriva, au temps d'Achaz, fils de Jotham, fils d'Ozias, roi de Juda, que Retsin, roi de Syrie, et Pékach, fils de Rémalia, roi d'Israël, montèrent contre Jérusalem pour l'assiéger; mais ils ne purent l'assiéger.
2 Wakati huu nyumba ya Daudi iliambiwa, “Aramu wameungana na Efraimu.” Kwa hiyo mioyo ya Ahazi na watu wake ilitikiswa, kama miti ya msituni inavyotikiswa na upepo.
Et l'on vint dire à la maison de David: Le Syrien campe en Éphraïm. Alors le cœur d'Achaz et le cœur de son peuple furent ébranlés, comme les arbres des forêts sont ébranlés par le vent.
3 Ndipo Bwana akamwambia Isaya, “Toka uende, wewe na mwanao Shear-Yashubu, mkutane na Ahazi huko mwisho wa mfereji wa Bwawa la Juu, kwenye barabara iendayo Shamba la Dobi.
Puis l'Éternel dit à Ésaïe: Sors au-devant d'Achaz, toi et Shéarjashub, ton fils, vers le bout de l'aqueduc du haut étang, vers la chaussée du champ du foulon.
4 Mwambie, ‘Uwe mwangalifu, utulie na usiogope. Usife moyo kwa ajili ya watu hawa wawili walio kama visiki vya kuni vifukavyo moshi, kwa ajili ya hasira kali ya Resini na Aramu na ya mwana wa Remalia.
Et dis-lui: Prends garde, et reste tranquille; ne crains rien, et que ton cœur ne s'alarme pas devant ces deux bouts de tisons fumants, devant l'ardente colère de Retsin, de la Syrie et du fils de Rémalia,
5 Aramu, Efraimu na mwana wa Remalia wamepanga shauri baya ili wakuangamize, wakisema,
Parce que la Syrie médite du mal contre toi, avec Éphraïm et le fils de Rémalia, et qu'ils disent:
6 “Tuishambulie Yuda, naam, tuirarue vipande vipande na kuigawa miongoni mwetu, na kumtawaza mwana wa Tabeeli awe mfalme juu yake.”
Montons contre Juda, frappons-le de terreur et battons la ville en brèche, et établissons-y roi le fils de Tabéal!
7 Lakini Bwana Mwenyezi asema hivi: “‘Jambo hili halitatendeka, halitatokea,
Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Cela n'aura point d'effet, cela ne se fera point.
8 kwa kuwa kichwa cha Aramu ni Dameski, na kichwa cha Dameski ni Resini peke yake. Katika muda wa miaka sitini na mitano, Efraimu atakuwa ameharibiwa kiasi kwamba hataweza tena kuwa taifa.
Car la tête de la Syrie, c'est Damas; et la tête de Damas, c'est Retsin; et dans soixante-cinq ans, Éphraïm sera mis en pièces et ne sera plus un peuple.
9 Kichwa cha Efraimu ni Samaria, na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia peke yake. Kama hamtasimama thabiti katika imani yenu, hamtaimarika kamwe.’”
Et la tête d'Éphraïm, c'est Samarie; et la tête de Samarie, le fils de Rémalia. Que si vous ne croyez pas, vous ne subsisterez pas.
10 Bwana akasema na Ahazi tena,
L'Éternel parla encore à Achaz, et lui dit:
11 “Mwombe Bwana Mungu wako ishara, iwe kwenye vina virefu sana, au kwenye vimo virefu sana.” (Sheol h7585)
Demande un signe à l'Éternel ton Dieu; demande-le soit dans les lieux bas, soit dans les lieux élevés. (Sheol h7585)
12 Lakini Ahazi akasema, “Sitaomba; sitamjaribu Bwana.”
Et Achaz dit: Je n'en demanderai point, et je ne tenterai point l'Éternel.
13 Ndipo Isaya akasema, “Sikia sasa, ewe nyumba ya Daudi! Je, haitoshi kujaribu uvumilivu wa wanadamu? Je, mtaujaribu uvumilivu wa Mungu wangu pia?
Alors Ésaïe dit: Écoutez, ô maison de David! Est-ce trop peu pour vous de lasser les hommes, que vous lassiez aussi mon Dieu?
14 Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara: Bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, na ataitwa Imanueli.
C'est pourquoi le Seigneur lui-même vous donnera un signe: Voici, la vierge sera enceinte; elle enfantera un fils, et lui donnera le nom d'Emmanuel (Dieu avec nous).
15 Atakula jibini na asali atakapokuwa ameweza kukataa mabaya na kuchagua mema.
Il mangera de la crème et du miel, jusqu'à ce qu'il sache rejeter le mal et choisir le bien.
16 Lakini kabla mtoto hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, nchi ya wafalme hao wawili unaowaogopa itafanywa ukiwa.
Mais, avant que l'enfant sache rejeter le mal et choisir le bien, le pays dont tu redoutes les deux rois, sera abandonné.
17 Bwana ataleta juu yako, juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako wakati ambao haujawahi kuwako tangu Efraimu alipojitenga na Yuda: yeye atawaleteeni mfalme wa Ashuru.”
L'Éternel fera venir sur toi, sur ton peuple et sur la maison de ton père, des jours tels qu'il n'y en a pas eu de semblables, depuis le jour qu'Éphraïm se sépara d'avec Juda, savoir le roi d'Assyrie.
18 Katika siku ile Bwana atawapigia filimbi mainzi kutoka vijito vya mbali vya Misri, na nyuki kutoka nchi ya Ashuru.
En ce jour-là, l'Éternel sifflera pour appeler les mouches qui sont au bout des fleuves d'Égypte, et les guêpes du pays d'Assur.
19 Wote watakuja na kukaa kwenye mabonde yenye miteremko, na kwenye nyufa za miamba, kwenye vichaka vyote vyenye miiba, na kwenye mashimo yote ya maji.
Elles viendront et se poseront toutes dans les vallées désertes, dans les fentes des rochers, dans tous les buissons et dans tous les pâturages.
20 Katika siku ile Bwana atatumia wembe ulioajiriwa kutoka ngʼambo ya Mto, yaani mfalme wa Ashuru, kunyoa nywele za kichwa chako na malaika ya miguu yako, na kuziondoa ndevu zako pia.
En ce jour-là, le Seigneur rasera avec un rasoir qu'il aura loué au-delà du fleuve (avec le roi d'Assyrie), la tête et les poils des pieds, et il enlèvera aussi la barbe.
21 Katika siku ile, mtu atahifadhi hai ndama mmoja na kondoo wawili.
En ce jour-là, chacun nourrira une jeune vache et deux brebis;
22 Kwa ajili ya wingi wa maziwa watakayotoa, atapata jibini ya kula. Wote watakaobakia katika nchi watakula jibini na asali.
Et elles produiront tant de lait qu'il mangera de la crème; car tous ceux qui seront laissés de reste dans le pays, mangeront de la crème et du miel.
23 Katika siku ile, kila mahali palipokuwa na mizabibu elfu moja yenye thamani ya shekeli 1,000 za fedha, patakuwa na michongoma na miiba tu.
En ce jour-là, tout lieu qui contiendra mille ceps de vigne, valant mille sicles d'argent, sera réduit en ronces et en épines.
24 Watu watakwenda huko wakiwa na upinde na mshale, kwa maana nchi itafunikwa na michongoma na miiba.
On y viendra avec la flèche et avec l'arc; car tout le pays ne sera que ronces et épines.
25 Kuhusu vilima vyote vilivyokuwa vikilimwa kwa jembe, hamtakwenda huko tena kwa ajili ya hofu ya michongoma na miiba. Patakuwa mahali ambapo ngʼombe wataachiwa huru, na kondoo kukimbia kimbia.
Et dans toutes les montagnes que l'on cultivait à la bêche, on ne viendra plus, par crainte des ronces et des épines; mais on y mettra les bœufs en pâture, et elles seront foulées par les brebis.

< Isaya 7 >