< Isaya 66 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana, “Mbingu ni kiti changu cha enzi, nayo dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu. Iko wapi nyumba mtakayoijenga kwa ajili yangu? Mahali pangu pa kupumzikia patakuwa wapi?
Ainsi a dit l'Eternel; les cieux sont mon trône, et la terre est le marchepied de mes pieds: quelle maison me bâtiriez-vous, et quel serait le lieu de mon repos?
2 Je, mkono wangu haukufanya vitu hivi vyote, hivyo vikapata kuwepo?” asema Bwana. “Mtu huyu ndiye ninayemthamini: yeye ambaye ni mnyenyekevu na mwenye roho yenye toba, atetemekaye asikiapo neno langu.
Car ma main a fait toutes ces choses, et c'est par moi que toutes ces choses ont eu leur être, dit l'Eternel. Mais à qui regarderai-je? à celui qui est affligé, et qui a l'esprit brisé, et qui tremble à ma parole.
3 Lakini yeyote atoaye dhabihu ya fahali ni kama yeye auaye mtu, na yeyote atoaye sadaka ya mwana-kondoo, ni kama yule avunjaye shingo ya mbwa. Yeyote atoaye sadaka ya nafaka, ni kama yule aletaye damu ya nguruwe, na yeyote afukizaye uvumba wa kumbukumbu, ni kama yule aabuduye sanamu. Wamejichagulia njia zao wenyewe, nazo nafsi zao zinafurahia machukizo yao.
Celui qui égorge un bœuf, [c'est comme] qui tuerait un homme; celui qui sacrifie une brebis, c'est [comme] qui couperait le cou à un chien; celui qui offre un gâteau, [c'est comme qui offrirait] le sang d'un pourceau; celui qui fait un parfum d'encens, [c'est comme] qui bénirait une idole. Mais ils ont choisi leurs voies, et leur âme a pris plaisir en leurs abominations.
4 Hivyo, mimi pia nitawachagulia mapigo makali, nami nitaleta juu yao kile wanachokiogopa. Kwa maana nilipoita, hakuna yeyote aliyejibu, niliposema, hakuna yeyote aliyesikiliza. Walifanya maovu machoni pangu na kuchagua lile linalonichukiza.”
Moi aussi je ferai attention à leurs tromperies, et je ferai venir sur eux les choses qu'ils craignent; parce que j'ai crié, et qu'il n'y a eu personne qui répondît: que j'ai parlé, et qu'ils n'ont point écouté; parce qu'ils ont fait ce qui me déplaît, et qu'ils ont choisi les choses auxquelles je ne prends point de plaisir.
5 Sikieni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa neno lake: “Ndugu zenu wanaowachukia ninyi na kuwatenga ninyi kwa sababu ya Jina langu, wamesema, ‘Bwana na atukuzwe, ili tupate kuona furaha yenu!’ Hata sasa wataaibika.
Ecoutez la parole de l'Eternel, vous qui tremblez à sa parole; vos frères qui vous haïssent, et qui vous rejettent comme une chose abominable, à cause de mon Nom, ont dit; que l'Eternel montre sa gloire. Il sera donc vu à votre joie, mais eux seront honteux.
6 Sikieni hizo ghasia kutoka mjini, sikieni hizo kelele kutoka hekaluni! Ni sauti ya Bwana ikiwalipa adui zake yote wanayostahili.
Un son éclatant vient de la ville, un son vient du Temple, le son de l'Eternel, rendant la pareille à ses ennemis.
7 “Kabla hajasikia utungu, alizaa; kabla hajapata maumivu, alizaa mtoto mwanaume.
Elle a enfanté avant que de sentir le travail d'enfant; elle a été délivrée d'un enfant mâle, avant que les tranchées lui vinssent.
8 Ni nani amepata kusikia jambo kama hili? Ni nani amepata kuona mambo kama haya? Je, nchi yaweza kuzaliwa kwa siku moja, au taifa laweza kutokea mara? Mara Sayuni alipoona utungu, alizaa watoto wake.
Qui entendit jamais une telle chose, et qui en a jamais vu de semblables? Ferait-on qu'un pays fût enfanté en un jour? ou une nation naîtrait-elle tout d'un coup, que Sion ait enfanté ses fils aussitôt qu'elle a été en travail d'enfant?
9 Je, nilete mwana hadi wakati wa kuzaliwa na nisizalishe?” asema Bwana. “Je, nifunge tumbo la uzazi wakati mimi ndiye nizalishaye?” asema Mungu wako.
Moi qui fais enfanter les autres, ne ferais-je point enfanter [Sion]? a dit l'Eternel; Moi qui donne de la postérité aux autres, l'empêcherais-je [d'enfanter?] a dit ton Dieu.
10 “Shangilieni pamoja na Yerusalemu na mfurahi kwa ajili yake, ninyi nyote mnaompenda, shangilieni kwa nguvu pamoja naye, ninyi nyote mnaoomboleza juu yake.
Réjouissez-vous avec Jérusalem, et vous égayez en elle, vous tous qui l'aimez; vous tous qui meniez deuil sur elle, réjouissez-vous avec elle l'une grande joie.
11 Kwa kuwa mtanyonya na kutosheka katika faraja ya matiti yake; mtakunywa sana, na kuufurahia wingi wa mafuriko ya ustawi wake.”
Afin que vous soyez allaités, et que vous soyez rassasiés de la mamelle de ses consolations; afin que vous suciez [le lait], et que vous jouissiez à plaisir de toutes les sortes de sa gloire.
12 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Nitamwongezea amani kama mto, nao utajiri wa mataifa kama kijito kifurikacho; utanyonya na kuchukuliwa mikononi mwake na kubembelezwa magotini pake.
Car ainsi a dit l'Eternel; voici, je m'en vais faire couler vers elle la paix comme un fleuve, et la gloire des nations comme un torrent débordé; et vous serez allaités, portés sur les côtés, et on vous fera jouer sur les genoux.
13 Kama mama anavyomfariji mtoto wake, ndivyo nitakavyokufariji wewe, nawe utafarijiwa huko Yerusalemu.”
Je vous caresserai pour vous apaiser, comme quand une mère caresse son enfant pour l'apaiser; car vous serez consolés en Jérusalem.
14 Wakati mtakapoona jambo hili, mioyo yenu itashangilia, nanyi mtastawi kama majani; mkono wa Bwana utajulikana kwa watumishi wake, bali ghadhabu yake kali itaonyeshwa kwa adui zake.
Et vous le verrez, et votre cœur se réjouira, et vos os germeront comme l'herbe; et la main de l'Eternel sera connue envers ses serviteurs; mais il sera ému à indignation contre ses ennemis.
15 Tazama, Bwana anakuja na moto, magari yake ya vita ni kama upepo wa kisulisuli, atateremsha hasira yake kwa ghadhabu kali, na karipio lake pamoja na miali ya moto.
Car voici, l'Eternel viendra avec le feu, et ses chariots seront comme la tempête, afin qu'il tourne sa colère en fureur, et sa menace en flamme de feu.
16 Kwa maana kwa moto na kwa upanga wake Bwana atatekeleza hukumu juu ya watu wote, nao wengi watakuwa ni wale waliouawa na Bwana.
Car l'Eternel exercera jugement contre toute chair par le feu, et avec son épée, et le nombre de ceux qui seront mis à mort par l'Eternel, sera grand.
17 “Watu wote wanaojiweka wakfu na kujitakasa wenyewe ili kwenda bustanini, wakimfuata aliye katikati ya wale ambao hula nyama za nguruwe na panya pamoja na vitu vingine vilivyo machukizo, watafikia mwisho wao pamoja,” asema Bwana.
Ceux qui se sanctifient et se purifient au milieu des jardins, l'un après l'autre, qui mangent de la chair de pourceau, et des choses abominables, [comme] des souris, seront ensemble consumés, a dit l'Eternel.
18 “Nami, kwa sababu ya matendo yao na mawazo yao, niko karibu kuja na kukusanya mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.
Mais pour moi, [voyant] leurs œuvres, et leurs pensées, [le temps] vient d'assembler toutes les nations et les langues; ils viendront, et verront ma gloire.
19 “Nitaweka ishara katikati yao, nami nitapeleka baadhi ya hao walionusurika kwa mataifa, hadi Tarshishi, kwa Puli na Waludi (wanaojulikana kama wapiga upinde), kwa Tubali na Uyunani, hadi visiwa vya mbali ambavyo havijasikia juu ya sifa zangu au kuuona utukufu wangu. Watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.
Car je mettrai une marque en eux, et j'enverrai ceux d'entre eux qui seront réchappés, vers les nations, en Tarsis, en Pul, en Lud, gens tirant de l'arc, en Tubal, et en Javan, [et vers] les Iles éloignées qui n'ont point entendu ma renommée, et qui n'ont point vu ma gloire, et ils annonceront ma gloire parmi les nations.
20 Nao watawaleta ndugu zenu wote, kutoka mataifa yote, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu katika Yerusalemu kama sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, katika magari ya vita na magari makubwa, juu ya nyumbu na ngamia,” asema Bwana. “Watawaleta, kama Waisraeli waletavyo sadaka zao za nafaka, katika Hekalu la Bwana, katika vyombo safi kwa kufuata desturi za ibada.
Et ils amèneront tous vos frères, d'entre toutes les nations, sur des chevaux, sur des chariots, et dans des litières, sur des mulets, et sur des dromadaires, pour offrande à l'Eternel, à la montagne de ma sainteté, à Jérusalem, a dit l'Eternel, comme lorsque les enfants d'Israël apportent l'offrande dans un vaisseau net, à la maison de l'Eternel.
21 Nami nitachagua baadhi yao pia wawe makuhani na Walawi,” asema Bwana.
Et même j'en prendrai d'entre eux pour Sacrificateurs, [et] pour Lévites, a dit l'Eternel.
22 “Kama vile mbingu mpya na nchi mpya ninazozifanya zitakavyodumu mbele zangu,” asema Bwana, “ndivyo jina lenu na wazao wenu watakavyodumu.
Car comme les nouveaux cieux et la nouvelle terre que je m'en vais faire, seront établis devant moi, dit l'Eternel; ainsi sera établie votre postérité, et votre nom.
23 Kutoka Mwezi Mpya hata mwingine, na kutoka Sabato hadi nyingine, wanadamu wote watakuja na kusujudu mbele zangu,” asema Bwana.
Et il arrivera que depuis une nouvelle lune jusqu'à l'autre, et d'un Sabbat à l'autre, toute chair viendra se prosterner devant ma face, a dit l'Eternel.
24 “Nao watatoka nje na kuona maiti za wale walioniasi mimi. Funza wao hawatakufa, wala moto wao hautazimika, nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa wanadamu wote.”
Et ils sortiront dehors, et verront les corps morts des hommes qui auront péché contre moi; car leur ver ne mourra point, et leur feu ne sera point éteint; et ils seront méprisés de tout le monde.

< Isaya 66 >