< Isaya 57 >

1 Mwenye haki hupotea, wala hakuna hata mmoja awazaye hilo moyoni mwake; watu wanaomcha Mungu huondolewa, wala hakuna hata mmoja anayeelewa kuwa wenye haki wameondolewa ili wasipatikane na maovu.
Le juste meurt, et personne n'y prend garde; les gens de bien sont recueillis, sans que nul comprenne que le juste est recueilli devant le mal.
2 Wale waendao kwa unyofu huwa na amani; hupata pumziko walalapo mautini.
Il entre dans la paix. Ils se reposent sur leurs couches, ceux qui ont marché dans le droit chemin.
3 “Lakini ninyi: Njooni hapa, ninyi wana wa wachawi, ninyi wazao wa wazinzi na makahaba!
Mais vous, approchez ici, enfants de la devineresse, race de l'adultère et de la prostituée!
4 Mnamdhihaki nani? Ni nani mnayemcheka kwa dharau, na kumtolea ndimi zenu? Je, ninyi si watoto wa waasi, uzao wa waongo?
De qui est-ce que vous vous moquez? Contre qui ouvrez-vous une large bouche, et tirez-vous la langue? N'êtes-vous pas des enfants de rébellion, une race de mensonge;
5 Mnawaka tamaa katikati ya mialoni na chini ya kila mti uliotanda matawi; mnawatoa kafara watoto wenu kwenye mabonde na chini ya majabali yenye mianya.
S'échauffant auprès des chênes, sous tout arbre vert; égorgeant les enfants dans les vallons, sous les cavités des rochers?
6 “Sanamu zilizo katikati ya mawe laini ya mabondeni ndizo fungu lenu; hizo ndizo sehemu yenu. Naam, kwa hizo mmemimina sadaka za vinywaji, na kutoa sadaka za nafaka. Katika haya yote, niendelee kuona huruma?
Les pierres polies des torrents sont ton partage; voilà, voilà ton lot; c'est aussi à elles que tu fais des libations, que tu présentes l'offrande; pourrai-je me résigner à cela?
7 Umeweka kitanda chako juu kwenye kilima kirefu kilichoinuka, huko ulikwenda kutoa dhabihu zako.
Tu places ta couche sur une montagne haute et élevée, et tu montes là pour sacrifier.
8 Nyuma ya milango yako na miimo yako umeweka alama zako za kipagani. Kwa kuniacha mimi, ulifunua kitanda chako, umepanda juu yake na kukipanua sana; ulifanya patano na wale ambao unapenda vitanda vyao, nawe uliangalia uchi wao.
Tu places ton mémorial derrière la porte et le linteau; car tu me quittes pour te découvrir et pour monter là; tu élargis ton lit, et c'est avec ceux-là que tu t'allies; tu aimes leur commerce, tu te choisis une place.
9 Ulikwenda kwa Moleki ukiwa na mafuta ya zeituni, na ukaongeza manukato yako. Ukawatuma wajumbe wako mbali sana, ukashuka kwenye kaburi lenyewe! (Sheol h7585)
Tu te rends auprès du roi avec de l'huile, et tu multiplies les parfums; tu envoies tes messagers bien loin, et tu les fais descendre jusqu'au séjour des morts. (Sheol h7585)
10 Ulikuwa umechoshwa na njia zako zote, lakini hukusema, ‘Hakuna tumaini.’ Ulipata uhuisho wa nguvu zako, kwa sababu hiyo hukuzimia.
Tu te fatigues par la longueur du chemin; tu ne dis pas: C'est en vain! Tu trouves encore en ta main de la vigueur; c'est pourquoi tu ne t'abats point.
11 “Ni nani uliyemhofu hivyo na kumwogopa hata ukawa mwongo kwangu, wala hukunikumbuka au kutafakari hili moyoni mwako? Si ni kwa sababu nimekuwa kimya muda mrefu hata huniogopi?
Qui donc as-tu craint et redouté, pour être infidèle, pour ne pas te souvenir ni te soucier de moi? Je me taisais, n'est-ce pas? et depuis longtemps; c'est pourquoi tu ne me crains plus?
12 Nitaifunua haki yako na matendo yako, nayo hayatakufaidi.
Je ferai connaître ta justice, et tes œuvres, qui ne te profiteront pas.
13 Utakapolia kwa kuhitaji msaada, sanamu zako ulizojikusanyia na zikuokoe! Upepo utazipeperusha zote, pumzi peke yake itazipeperusha, Lakini mtu atakayenifanya kimbilio lake, atairithi nchi na kuumiliki mlima wangu mtakatifu.”
Quand tu crieras, qu'ils te délivrent, les dieux que tu as amassés! Voici, le vent les enlèvera tous, un souffle les emportera. Mais celui qui se retire vers moi, héritera le pays, et possédera ma montagne sainte.
14 Tena itasemwa: “Jengeni, jengeni, itengenezeni njia! Ondoeni vikwazo katika njia ya watu wangu.”
Et l'on dira: Aplanissez, aplanissez, préparez le chemin! Enlevez tout obstacle du chemin de mon peuple!
15 Kwa maana hili ndilo asemalo Aliye juu, yeye aliyeinuliwa sana, yeye aishiye milele, ambaye jina lake ni Mtakatifu: “Ninaishi mimi mahali palipoinuka na patakatifu, lakini pia pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na mwenye roho ya unyenyekevu, ili kuzihuisha roho za wanyenyekevu na kuihuisha mioyo yao waliotubu.
Car ainsi a dit le Très-Haut, qui habite une demeure éternelle, et dont le nom est saint: J'habite dans le lieu haut et saint, et avec l'homme abattu et humble d'esprit, pour ranimer l'esprit des humbles, pour ranimer le cœur de ceux qui sont abattus.
16 Sitaendelea kulaumu milele, wala sitakasirika siku zote, kwa kuwa roho ya mwanadamu ingezimia mbele zangu: yaani pumzi ya mwanadamu niliyemuumba.
Car je ne contesterai pas toujours, et je ne serai pas indigné à jamais; car l'esprit défaillirait devant ma face, et les âmes que j'ai créées.
17 Nilighadhibika na tamaa yake ya dhambi; nilimwadhibu, nikauficha uso wangu kwa hasira, na bado aliendelea katika njia zake za tamaa.
A cause de l'iniquité de ses gains, je me suis indigné et j'ai frappé; j'ai caché ma face, et je me suis indigné; et le rebelle a suivi le chemin de son cœur.
18 Nimeziona njia zake, lakini nitamponya, nitamwongoza na kumrudishia upya faraja,
J'ai vu ses voies, et je le guérirai; je le conduirai et lui donnerai des consolations, à lui et aux siens qui sont dans le deuil.
19 nikiumba sifa midomoni ya waombolezaji katika Israeli. Amani, amani, kwa wale walio mbali na kwa wale walio karibu,” asema Bwana. “Nami nitawaponya.”
C'est moi qui crée le fruit des lèvres: Paix, paix, à celui qui est loin et à celui qui est près! dit l'Éternel. Oui, je le guérirai.
20 Bali waovu ni kama bahari ichafukayo, ambayo haiwezi kutulia, mawimbi yake hutupa takataka na matope.
Mais les méchants sont comme la mer agitée, qui ne peut se calmer, dont les eaux rejettent de la vase et du limon.
21 Mungu wangu asema, “Hakuna amani kwa waovu.”
Il n'y a point de paix pour les méchants, dit mon Dieu.

< Isaya 57 >