< Isaya 4 >

1 Katika siku ile wanawake saba watamshika mwanaume mmoja wakisema, “Tutakula chakula chetu wenyewe na kuvaa nguo zetu wenyewe, ila wewe uturuhusu tu tuitwe kwa jina lako. Utuondolee aibu yetu!”
En ce jour-là, sept femmes saisiront un seul homme, et diront: Nous mangerons notre pain, et nous nous vêtirons de nos vêtements; seulement que nous portions ton nom; fais cesser notre opprobre!
2 Katika siku ile Tawi la Bwana litakuwa zuri na lenye utukufu, nalo tunda la nchi litakuwa fahari na utukufu wa wale Waisraeli watakaonusurika.
En ce jour-là, le germe de l'Éternel sera l'ornement et la gloire des réchappés d'Israël; le fruit de la terre sera leur orgueil et leur parure.
3 Wale watakaoachwa Sayuni, watakaobaki Yerusalemu, wataitwa watakatifu, wale wote ambao wameorodheshwa miongoni mwa walio hai huko Yerusalemu.
Et ceux qui resteront de Sion, ceux qui seront demeurés de reste à Jérusalem, seront appelés saints, tous ceux de Jérusalem qui seront inscrits parmi les vivants,
4 Bwana atausafisha uchafu wa wanawake wa Sayuni, atatakasa madoa ya damu kutoka Yerusalemu kwa Roho ya hukumu na Roho ya moto.
Quand le Seigneur aura lavé la souillure des filles de Sion, et enlevé le sang du milieu de Jérusalem, par l'esprit de justice et par l'esprit qui consume.
5 Kisha Bwana ataumba juu ya Mlima wote wa Sayuni, na juu ya wale wote wanaokusanyika hapo, wingu la moshi wakati wa mchana, na kungʼaa kwa miali ya moto wakati wa usiku, nako juu ya huo utukufu wote kutatanda kifuniko cha ulinzi.
Et sur toute l'étendue du mont de Sion, et sur ses assemblées, l'Éternel créera un nuage et une fumée pendant le jour, et pendant la nuit l'éclat d'un feu flamboyant. Car toute gloire sera mise à couvert.
6 Utakuwa sitara na kivuli kutokana na joto la mchana, na kuwa mahali pa kujificha kutokana na dhoruba na mvua.
Et il y aura un abri, qui donnera de l'ombrage le jour contre la chaleur, qui servira de refuge et d'asile contre la tempête et la pluie.

< Isaya 4 >