< Isaya 22 >

1 Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
Prophétie sur la vallée des visions. Qu'as-tu donc, que tu sois tout entière montée sur les toits,
2 Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
Ville bruyante, pleine de clameurs, cité joyeuse? Tes morts n'ont pas été frappés par l'épée, ils ne sont pas tués en combattant.
3 Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
Tous ses chefs s'étaient enfuis ensemble, devant les archers; ils sont faits prisonniers; tous ceux des siens que l'on trouve, sont faits prisonniers ensemble, quand ils s'enfuyaient au loin.
4 Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
C'est pourquoi je dis: Détournez les yeux de moi, que je pleure amèrement! N'insistez pas pour me consoler du désastre de la fille de mon peuple.
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
Car c'est un jour de trouble, de destruction et de consternation, le jour du Seigneur, l'Éternel des armées, dans la vallée des visions. On démolit la muraille, des cris de détresse retentissent sur la montagne.
6 Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
Élam porte le carquois, avec des chars pleins d'hommes et des cavaliers; Kir découvre le bouclier.
7 Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
Les plus belles vallées sont remplies de chars, et les cavaliers se rangent en bataille devant les portes.
8 ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
Le voile de Juda est levé, et en ce jour tu portes tes regards vers les armes du palais de la forêt.
9 mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
Vous voyez les brèches nombreuses faites à la ville de David, et vous amassez les eaux du bas étang;
10 Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
Vous comptez les maisons de Jérusalem, vous démolissez les maisons pour fortifier la muraille;
11 Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
Vous faites aussi un réservoir entre les deux murailles pour les eaux du vieil étang. Mais vous ne regardez pas à Celui qui a fait ceci, vous ne voyez pas Celui qui l'a préparé dès longtemps.
12 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
Et tandis que le Seigneur, l'Éternel des armées, vous appelait en ce jour à pleurer, à gémir, à vous raser la tête et à ceindre le sac,
13 Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
Voici de l'allégresse et de la joie; on tue des bœufs, on égorge des moutons, on mange de la chair, et on boit du vin: Mangeons et buvons, car demain nous mourrons!
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
Mais voici ce que l'Éternel des armées m'a fait entendre: Jamais cette iniquité ne vous sera pardonnée, que vous n'en mouriez, dit le Seigneur, l'Éternel des armées.
15 Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel des armées: Va, rends-toi vers ce favori du roi, vers Shebna, le préfet du palais:
16 Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
Qu'as-tu ici et qui as-tu ici, que tu te sois creusé ici un tombeau? Il se creuse un tombeau sur la hauteur; il se taille une demeure dans le roc!
17 “Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
Voici, l'Éternel va te lancer au loin, comme avec un bras vigoureux; il t'enveloppera de toutes parts;
18 Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
Il te fera rouler, rouler comme une boule, vers un pays large et spacieux. Là tu mourras, là iront tes chars magnifiques, ô honte de la maison de ton seigneur!
19 Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
Je te chasserai de ton poste, et tu seras ôté de ta place!
20 “Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
En ce jour-là, j'appellerai mon serviteur Éliakim, fils de Hilkija;
21 Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
Je le vêtirai de ta tunique, et le ceindrai de ta ceinture; je mettrai ton autorité entre ses mains, et il sera le père des habitants de Jérusalem et de la maison de Juda.
22 Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
Je mettrai sur son épaule la clef de la maison de David; il ouvrira, et nul ne fermera; il fermera, et nul n'ouvrira.
23 Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
Je le fixerai comme un clou en lieu sûr; il sera comme un trône de gloire pour la maison de son père.
24 Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
Toute la gloire de la maison de son père, les rejetons grands et petits, reposeront sur lui; tous les petits ustensiles, depuis la vaisselle des bassins, jusqu'à tous les instruments de musique.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.
En ce jour-là, dit l'Éternel des armées, le clou fixé dans un lieu sûr cédera; il sera coupé, il tombera, et la charge qu'il portait sera retranchée. Car l'Éternel a parlé.

< Isaya 22 >