< Isaya 22 >

1 Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
La charge de la vallée de vision. Qu'as-tu maintenant, que tu sois toute montée sur les toits,
2 Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
Toi pleine de tumulte, ville bruyante, ville qui ne demandais qu'à t'égayer? tes blessés à mort n'ont pas été blessés à mort par l'épée, et ils ne sont pas morts par la guerre.
3 Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
Tous tes conducteurs sont allés errant çà et là ensemble, ils ont été liés par les archers; tous ceux des tiens qui ont été trouvés ont été liés ensemble, s'en étant fuis loin.
4 Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
C'est pourquoi j'ai dit; retirez-vous de moi, je pleurerai amèrement. Ne vous empressez point de me consoler touchant le dégât de la fille de mon peuple.
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
Car c'est le jour de trouble, d'oppression, et de perplexité, de par le Seigneur, l'Eternel des armées, dans la vallée de vision; il s'en va démolir la muraille, et le cri en ira jusqu'à la montagne.
6 Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
Même Hélam a pris son carquois, [il y a] des hommes montés sur des chariots, et Kir a découvert le bouclier.
7 Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
Et il est arrivé que l'élite de tes vallées a été remplie de chariots, et les gens de cheval se sont tous rangés en bataille contre la porte.
8 ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
Et on a découvert ce qui couvrait Juda, et tu as regardé en ce jour-là vers les armes de la maison du parc.
9 mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
Et vous avez vu que les brèches de la cité de David étaient grandes; et vous avez assemblé les eaux du bas étang.
10 Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
Et vous avez fait le dénombrement des maisons de Jérusalem, et démoli les maisons pour fortifier la muraille.
11 Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
Vous avez aussi fait un réservoir d'eaux entre les deux murailles, pour les eaux du vieux étang; mais vous n'avez point regardé à celui qui l'a faite et formée dès longtemps.
12 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
Et le Seigneur, l'Eternel des armées, [vous] a appelés ce jour-là aux pleurs et au deuil, à vous arracher les cheveux, et à ceindre le sac;
13 Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
Et voici il y a de la joie et de l'allégresse; on tue des bœufs, on égorge des moutons, on en mange la chair, et on boit du vin; [puis on dit]; Mangeons et buvons; car demain nous mourrons.
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
Or l'Eternel des armées m'a déclaré, disant; si jamais cette iniquité vous est pardonnée, que vous n'en mouriez, a dit le Seigneur, l'Eternel des armées.
15 Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
Ainsi a dit le Seigneur, l'Eternel des armées; va, entre chez ce trésorier, chez Sebna maître d'hôtel [et lui dis];
16 Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
Qu'as-tu à faire ici? et qui [est] ici qui t'appartienne, que tu te sois taillé ici un sépulcre? Il taille un lieu éminent pour son sépulcre, et se creuse une demeure dans un rocher.
17 “Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
Voici, ô homme! l'Eternel te chassera loin, et te couvrira entièrement.
18 Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
Il te fera rouler fort vite comme une boule en un pays large et spacieux; tu mourras là, et là seront les chariots de ta gloire, [de toi qui es] la honte de la maison de ton Seigneur.
19 Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
Et je te jetterai hors de ton rang, et on te déposera de ton emploi.
20 “Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
Et il arrivera en ce jour-là que j'appellerai mon serviteur Eliakim, fils de Hilkija.
21 Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
Et je le vêtirai de ta casaque, je le ceindrai de ton baudrier, je mettrai ton autorité entre ses mains, et il sera pour père à ceux qui habitent dans Jérusalem, et à la maison de Juda.
22 Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
Et je mettrai la clef de la maison de David sur son épaule; et il ouvrira, et il n'y aura personne qui ferme; et il fermera, et il n'y aura personne qui ouvre.
23 Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
Et je le ficherai comme un croc en un lieu ferme; et il sera pour trône de gloire à la maison de son père.
24 Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
Et on y pendra toute la gloire de la maison de son père, de ses parents, et de celles qui lui appartiennent; tous les ustensiles des plus petites choses, depuis les ustensiles des tasses jusques à tous les ustensiles des musettes.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.
En ce jour-là, dit l'Eternel des armées, le croc qui avait été fiché en un lieu ferme, sera ôté; et étant retranché il tombera, et ce dont il était chargé sera retranché; car l'Eternel a parlé.

< Isaya 22 >