< Isaya 10 >

1 Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
Woe to those who enact unjust laws and write unfair decrees.
2 kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
They deprive the needy of justice, rob the poor of my people of their rights, plunder widows, and make the fatherless their prey!
3 Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
What will you do on judgment day when the destruction comes from far away? To whom will you flee for help, and where will you leave your wealth?
4 Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Nothing remains, and you crouch among the prisoners or fall among the killed. In all these things, his anger does not subside; instead, his hand is still stretched out.
5 “Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
Woe to the Assyrian, the club of my anger, the rod by whom I wield my fury!
6 Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
I send him against an arrogant nation and against the people who bear my overflowing wrath. I order him to take the spoil, to take the prey, and to trample them like mud in the streets.
7 Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
But this is not what he intends, nor does he think this way. It is in his heart to destroy and eliminate many nations.
8 Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
For he says, “Are not all my princes kings?
9 Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
Is not Kalno like Carchemish? Is not Hamath like Arpad? Is not Samaria like Damascus?
10 Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
As my hand has overcome idolatrous kingdoms, whose carved figures were greater than those of Jerusalem and Samaria,
11 je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
just as I did to Samaria and her worthless idols, will I not also do the same to Jerusalem and to her idols?”
12 Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
When the Lord has finished his work on Mount Zion and on Jerusalem, I will punish the speech of the arrogant heart of the king of Assyria and his prideful looks.
13 Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
For he says, “By my strength and by my wisdom I acted. I have understanding, and I have removed the boundaries of the peoples. I have stolen their treasures, and like a bull I have brought down the inhabitants.
14 Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
My hand has seized, as from a nest, the wealth of nations, and as one gathers abandoned eggs, I gathered all the earth. None fluttered their wings or opened their mouth or chirped.”
15 Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
Will the ax boast about itself against the one who wields it? Will the saw praise itself more than the one who cuts with it? It is as if a rod could lift up those who raise it, or as if a wooden club could lift up a person.
16 Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
Therefore the Lord Yahweh of hosts will send emaciation among his elite warriors; and under his glory there will be kindled a burning like fire.
17 Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
The light of Israel will become a fire, and his Holy One a flame; it will burn and devour his thorns and briers in one day.
18 Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
Yahweh will consume the glory of his forest and of his fruitful land, both soul and body; it will be like when a sick man's life wastes away.
19 Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
The remnant of the trees of his forest will be so few, that a child could count them.
20 Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
On that day, the remnant of Israel, the family of Jacob that has escaped, will no longer rely on the one who defeated them, but will indeed depend on Yahweh, the Holy One of Israel.
21 Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
A remnant of Jacob will return to the mighty God.
22 Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
For though your people, Israel, are like the sand of the seashore, only a remnant of them will return. Destruction is decreed, as overflowing righteousness demands.
23 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
For the Lord Yahweh of hosts, is about to carry out the destruction determined throughout the land.
24 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
Therefore the Lord Yahweh of hosts says, “My people who live in Zion, do not fear the Assyrian. He will strike you with the rod and raise his staff against you, as the Egyptians did.
25 Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
Do not fear him, for in a very short time my anger against you will end, and my anger will lead to his destruction.”
26 Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
Then Yahweh of hosts will wield a whip against them, as when he defeated Midian at the rock of Oreb. He will raise his rod over the sea and lift it up as he did in Egypt.
27 Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
On that day, his burden is lifted from your shoulder and his yoke from off your neck, and the yoke will be destroyed because of fatness.
28 Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
The enemy has come to Aiath and has passed through Migron; at Michmash he has stored his provisions.
29 Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
They have crossed over the pass and they lodge at Geba. Ramah trembles and Gibeah of Saul has fled.
30 Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
Cry aloud, daughter of Gallim! Give attention, Laishah! You poor Anathoth!
31 Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
Madmenah is fleeing, and the inhabitants of Gebim run for safety.
32 Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
This very day he will halt at Nob and shake his fist at the mountain of the daughter of Zion, the hill of Jerusalem.
33 Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
Behold, the Lord Yahweh of hosts will lop off the boughs with a terrifying crash; the tallest trees will be cut down, and the lofty will be brought low.
34 Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.
He will chop down the thickets of the forest with an ax, and Lebanon in his majesty will fall.

< Isaya 10 >