< Isaya 1 >

1 Maono kuhusu Yuda na Yerusalemu ambayo Isaya mwana wa Amozi aliyaona wakati wa utawala wa Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda.
La vision d'Esaïe, fils d'Amots, laquelle il a vue touchant Juda et Jérusalem, aux jours de Hozias, de Jotham, d'Achas, et d'Ezéchias, Rois de Juda.
2 Sikieni, enyi mbingu! Sikilizeni, enyi dunia! Kwa maana Bwana amesema: “Nimewalisha watoto na kuwalea, lakini wameniasi mimi.
Cieux écoutez, et toi Terre prête l'oreille, car l'Eternel a parlé, [disant]; j'ai nourri des enfants, je les ai élevés, mais ils se sont rebellés contre moi.
3 Ngʼombe anamjua bwana wake, naye punda anajua hori la mmiliki wake, lakini Israeli hajui, watu wangu hawaelewi.”
Le bœuf connaît son possesseur, et l'âne la crèche de son maître; [mais] Israël n'a point de connaissance, mon peuple n'a point d'intelligence.
4 Lo! Taifa lenye dhambi, watu waliolemewa na uovu, uzao wa watenda mabaya, watoto waliozoelea upotovu! Wamemwacha Bwana, Wamemkataa kwa dharau yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli na kumgeuzia kisogo.
Ha! nation pécheresse, peuple chargé d'iniquité, race de gens malins, enfants qui ne font que se corrompre; ils ont abandonné l'Eternel, ils ont irrité par leur mépris le Saint d'Israël, ils se sont retirés en arrière.
5 Kwa nini mzidi kupigwa? Kwa nini kudumu katika uasi? Kichwa chako chote kimejeruhiwa, moyo wako wote ni mgonjwa.
Pourquoi seriez-vous encore battus? vous ajouterez la révolte; toute tête est en douleur, et tout cœur est languissant.
6 Kutoka wayo wako wa mguu hadi kwenye utosi wa kichwa chako hakuna uzima: ni majeraha matupu na makovu na vidonda vitokavyo damu, havikusafishwa au kufungwa wala kulainishwa kwa mafuta.
Depuis la plante du pied jusqu'à la tête il n'y a rien d'entier en lui; il [n'y a que] blessure, meurtrissure, et plaie pourrie, qui n'ont point été nettoyées, ni bandées, et dont aucune n'a été adoucie d'huile.
7 Nchi yenu imekuwa ukiwa, miji yenu imeteketezwa kwa moto; nchi yenu imeachwa tupu na wageni mbele ya macho yenu, imeharibiwa kama vile imepinduliwa na wageni.
Votre pays n'est que désolation, et vos villes sont en feu; les étrangers dévorent votre terre en votre présence, et cette désolation est comme un bouleversement fait par des étrangers.
8 Binti Sayuni ameachwa kama kipenu katika shamba la mizabibu, kama kibanda katika shamba la matikitimaji, kama mji uliohusuriwa.
Car la fille de Sion restera comme une cabane dans une vigne; comme une loge dans un champ de concombres; comme une ville serrée de près.
9 Kama Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asingelituachia walionusurika, tungelikuwa kama Sodoma, tungelifanana na Gomora.
Si l'Eternel des armées ne nous eût laissé des gens de reste, qui sont même bien peu, nous eussions été comme Sodome, nous eussions été semblables à Gomorrhe.
10 Sikieni neno la Bwana, ninyi watawala wa Sodoma; sikilizeni sheria ya Mungu wetu, enyi watu wa Gomora!
Ecoutez la parole de l'Eternel, Conducteurs de Sodome, prêtez l'oreille à la Loi de notre Dieu, peuple de Gomorrhe!
11 Bwana anasema, “Wingi wa sadaka zenu, ni kitu gani kwangu? Ninazo sadaka za kuteketezwa nyingi kupita kiasi, za kondoo dume na mafuta ya wanyama walionona. Sipendezwi na damu za mafahali wala za wana-kondoo na mbuzi.
Qu'ai-je à faire, dit l'Eternel, de la multitude de vos sacrifices? je suis rassasié d'holocaustes de moutons, et de la graisse de bêtes grasses, je ne prends point de plaisir au sang des taureaux, ni des agneaux, ni des boucs.
12 Mnapokuja kujihudhurisha mbele zangu, ni nani aliyewataka ninyi mfanye hivyo, huku kuzikanyaga nyua zangu?
Quand vous entrez pour vous présenter devant ma face; qui a requis cela de vos mains, que vous fouliez de [vos pieds] mes parvis?
13 Acheni kuniletea sadaka zisizokuwa na maana! Uvumba wenu ni chukizo kwangu. Miandamo ya Mwezi, Sabato na makusanyiko ya ibada: siwezi kuvumilia makusanyiko yenu maovu.
Ne continuez plus à m'apporter des oblations de néant; le parfum m'est en abomination; quant aux nouvelles Lunes, et aux Sabbats, et à la publication de [vos] convocations, je n'en puis [plus] supporter l'ennui, ni de [vos] assemblées solennelles.
14 Sikukuu zenu za Miandamo ya Mwezi, na sikukuu zenu zilizoamriwa: moyo wangu unazichukia. Zimekuwa mzigo kwangu, nimechoka kuzivumilia.
Mon âme hait vos nouvelles Lunes, et vos fêtes solennelles; elles me sont fâcheuses, je suis las de les supporter.
15 Mnaponyoosha mikono yenu katika maombi, nitaficha macho yangu nisiwaone; hata mkiomba maombi mengi sitasikiliza. Mikono yenu imejaa damu;
C'est pourquoi quand vous étendrez vos mains, je cacherai mes yeux de vous, et quand vous multiplierez vos prières, je ne les exaucerai point; vos mains sont pleines de sang.
16 jiosheni na mkajitakase. Yaondoeni matendo yenu maovu mbele zangu! Acheni kutenda mabaya,
Lavez-vous, nettoyez-vous, ôtez de devant mes yeux la malice de vos actions; cessez de mal faire.
17 jifunzeni kutenda mema! Tafuteni haki, watieni moyo walioonewa. Teteeni shauri la yatima, wateteeni wajane.
Apprenez à bien faire; recherchez la droiture; redressez celui qui est foulé, faites justice à l'orphelin, défendez la cause de la veuve.
18 “Njooni basi tuhojiane,” asema Bwana. “Ingawa dhambi zenu ni kama rangi nyekundu, zitakuwa nyeupe kama theluji; ingawa ni nyekundu sana kama damu, zitakuwa nyeupe kama sufu.
Venez maintenant, dit l'Eternel, et débattons nos droits; quand vos péchés seraient comme le cramoisi, ils seront blanchis comme la neige; et quand ils seraient rouges comme le vermillon, ils seront [blanchis] comme la laine.
19 Kama mkikubali na kutii, mtakula mema ya nchi,
Si vous obéissez volontairement, vous mangerez le meilleur du pays.
20 lakini kama mkikataa na kuasi, mtaangamizwa kwa upanga.” Kwa kuwa kinywa cha Bwana kimenena.
Mais si vous refusez [d'obéir], et si vous êtes rebelles, vous serez consumés par l'épée; car la bouche de l'Eternel a parlé.
21 Tazama jinsi mji uliokuwa mwaminifu umekuwa kahaba! Mwanzoni ulikuwa umejaa unyofu, haki ilikuwa inakaa ndani yake, lakini sasa ni wauaji!
Comment s'est prostituée la cité fidèle? elle était pleine de droiture, et la justice logeait en elle, mais maintenant elle est pleine de meurtriers.
22 Fedha yenu imekuwa takataka, divai yenu nzuri imechanganywa na maji.
Ton argent est devenu de l'écume, et ton breuvage est mêlé d'eau.
23 Watawala wenu ni waasi, rafiki wa wevi, wote wanapenda rushwa na kukimbilia hongo. Hawatetei yatima, shauri la mjane haliletwi mbele yao lisikilizwe.
Les Principaux de ton peuple sont revêches, et compagnons de larrons; chacun d'eux aime les présents, ils courent après les récompenses; ils ne font point droit à l'orphelin, et la cause de la veuve ne vient point devant eux.
24 Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mwenye Nguvu wa Israeli, asema hivi: “Lo, nitapata faraja kutoka kwa adui zangu na kujilipizia kisasi juu ya watesi wangu.
C'est pourquoi le Seigneur, l'Eternel des armées, le Puissant d'Israël dit; Ha! je me satisferai [en punissant] mes adversaires, et je me vengerai de mes ennemis.
25 Nitauelekeza mkono wangu dhidi yenu, nitawasafisha takataka zenu zote na kuwaondolea unajisi wenu wote.
Et je remettrai ma main sur toi, et je refondrai au net ton écume, et j'ôterai tout ton étain.
26 Nitawarudishia waamuzi wenu kama ilivyokuwa siku za zamani, nao washauri wenu kama ilivyokuwa mwanzoni. Baadaye utaitwa, Mji wa Haki, Mji Mwaminifu.”
Mais je rétablirai tes Juges, tels qu'[ils étaient] la première fois, et tes Conseillers, tels que du commencement; et après cela on t'appellera, Cité de justice, ville fidèle.
27 Sayuni itakombolewa kwa haki, wale waliomo ndani yake waliotubu kwa uaminifu.
Sion sera rachetée par le jugement, et ceux qui y retourneront [seront rachetés] par la justice.
28 Lakini waasi na wenye dhambi wote wataangamizwa, nao wanaomwacha Bwana wataangamia.
Mais les rebelles, et les pécheurs seront froissés ensemble; et ceux qui ont abandonné l'Eternel, seront consumés.
29 “Mtaaibika kwa sababu ya hiyo mialoni ambayo mlifurahia, mtafadhaika kwa sababu ya bustani mlizozichagua.
Car on sera honteux à cause des chênes que vous avez désirés; et vous rougirez à cause des jardins que vous avez choisis.
30 Mtakuwa kama mwaloni wenye majani yanayonyauka, kama bustani isiyokuwa na maji.
Car vous serez comme le chêne dont la feuille tombe, et comme le jardin qui n'a point d'eau.
31 Mtu mwenye nguvu atatoweka kama majani makavu yawakayo moto, na kazi yake kama cheche ya moto; vyote vitaungua pamoja, wala hakuna wa kuuzima huo moto.”
Et le fort sera de l'étoupe, et son œuvre une étincelle; et tous deux brûleront ensemble, et il n'y aura personne qui éteigne [le feu].

< Isaya 1 >