< Hosea 8 >

1 “Wekeni tarumbeta midomoni mwenu! Tai yuko juu ya nyumba ya Bwana kwa sababu watu wamevunja Agano langu, wameasi dhidi ya sheria yangu.
Set the trumpet to your mouth. He shall come as an eagle against the house of the LORD, because they have transgressed my covenant, and trespassed against my law.
2 Israeli ananililia, ‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’
Israel shall cry to me, My God, we know you.
3 Lakini Israeli amekataa lile lililo jema, adui atamfuatia.
Israel has cast off the thing that is good: the enemy shall pursue him.
4 Wanaweka wafalme bila idhini yangu, wamechagua wakuu bila kibali changu. Kwa fedha zao na dhahabu wamejitengenezea sanamu kwa ajili ya maangamizi yao wenyewe.
They have set up kings, but not by me: they have made princes, and I knew it not: of their silver and their gold have they made them idols, that they may be cut off.
5 Ee Samaria, tupilieni mbali sanamu yenu ya ndama! Hasira yangu inawaka dhidi yao. Watakuwa najisi mpaka lini?
Your calf, O Samaria, has cast you off; my anger is kindled against them: how long will it be before they attain to innocence?
6 Zimetoka katika Israeli! Ndama huyu: ametengenezwa na fundi, si Mungu. Atavunjwa vipande vipande, yule ndama wa Samaria.
For from Israel was it also: the workman made it; therefore it is not God: but the calf of Samaria shall be broken in pieces.
7 “Wanapanda upepo na kuvuna upepo wa kisulisuli. Bua halina suke, halitatoa unga. Kama lingetoa nafaka, wageni wangeila yote.
For they have sown the wind, and they shall reap the whirlwind: it has no stalk; the bud shall yield no meal: if so be it yield, the strangers shall swallow it up.
8 Israeli amemezwa; sasa yupo miongoni mwa mataifa kama kitu kisicho na thamani.
Israel is swallowed up: now shall they be among the Gentiles as a vessel wherein is no pleasure.
9 Kwa kuwa wamepanda kwenda Ashuru kama punda-mwitu anayetangatanga peke yake. Efraimu amejiuza mwenyewe kwa wapenzi.
For they are gone up to Assyria, a wild ass alone by himself: Ephraim has hired lovers.
10 Ingawa wamejiuza wenyewe miongoni mwa mataifa, sasa nitawakusanya pamoja. Wataanza kudhoofika chini ya uonevu wa mfalme mwenye nguvu.
Yes, though they have hired among the nations, now will I gather them, and they shall sorrow a little for the burden of the king of princes.
11 “Ingawa Efraimu alijenga madhabahu nyingi kwa ajili ya sadaka za dhambi, hizi zimekuwa madhabahu za kufanyia dhambi.
Because Ephraim has made many altars to sin, altars shall be to him to sin.
12 Nimeandika kwa ajili yao mambo mengi kuhusu sheria yangu, lakini wameziangalia kama kitu cha kigeni.
I have written to him the great things of my law, but they were counted as a strange thing.
13 Wanatoa dhabihu nilizopewa mimi nao wanakula hiyo nyama, lakini Bwana hapendezwi nao. Sasa ataukumbuka uovu wao na kuadhibu dhambi zao: Watarudi Misri.
They sacrifice flesh for the sacrifices of my offerings, and eat it; but the LORD accepts them not; now will he remember their iniquity, and visit their sins: they shall return to Egypt.
14 Israeli amemsahau Muumba wake na kujenga majumba ya kifalme, Yuda amejengea miji mingi ngome. Lakini nitatuma moto kwenye miji yao utakaoteketeza ngome zao.”
For Israel has forgotten his Maker, and builds temples; and Judah has multiplied fenced cities: but I will send a fire on his cities, and it shall devour the palaces thereof.

< Hosea 8 >