< Hosea 2 >

1 “Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’
Say ye to your brothers, Ammi, and to your sisters, Ruhamah.
2 “Mkemeeni mama yenu, mkemeeni, kwa maana yeye si mke wangu, nami si mume wake. Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake na uzinzi kati ya matiti yake.
Contend with your mother. Contend, for she is not my wife, nor am I her husband. And let her put away her whoredoms from her face, and her adulteries from between her breasts,
3 Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa. Nitamfanya kama jangwa, nitamgeuza awe nchi ya kiu, nami nitamuua kwa kiu.
lest I strip her naked, and set her as in the day that she was born, and make her as a wilderness, and set her like a dry land, and kill her with thirst.
4 Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake, kwa sababu ni watoto wa uzinzi.
Yea, I will have no mercy upon her sons, for they are sons of whoredom,
5 Mama yao amekosa uaminifu na amewachukua mimba katika aibu. Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu, ambao hunipa chakula changu na maji yangu, sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu na kinywaji changu.’
for their mother has played the harlot. She who conceived them has done shamefully, for she said, I will go after my lovers, who give me my bread and my water, my wool and my flax, my oil and my drink.
6 Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake kwa vichaka vya miiba, nitamjengea ukuta ili kwamba asiweze kutoka.
Therefore, behold, I will hedge up thy way with thorns, and I will build a wall against her, that she shall not find her paths.
7 Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata; atawatafuta lakini hatawapata. Kisha atasema, ‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza, kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi kuliko sasa.’
And she shall follow after her lovers, but she shall not overtake them. And she shall seek them, but shall not find them. Then she shall say, I will go and return to my first husband, for it was better with me then than now.
8 Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta, niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia kwa kumtumikia Baali.
For she did not know that I gave her the grain, and the new wine, and the oil, and multiplied to her silver and gold, which they used for Baal.
9 “Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari. Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu iliyokusudiwa kufunika uchi wake.
Therefore I will take back my grain in the time of it, and my new wine in the season of it, and will pluck away my wool and my flax which should have covered her nakedness.
10 Basi sasa nitaufunua ufisadi wake mbele ya wapenzi wake; hakuna yeyote atakayemtoa mikononi mwangu.
And now I will uncover her lewdness in the sight of her lovers, and none shall deliver her out of my hand.
11 Nitakomesha furaha na macheko yake yote: sikukuu zake za mwaka, sikukuu za Miandamo ya Mwezi, siku zake za Sabato, sikukuu zake zote zilizoamriwa.
I will also cause all her mirth to cease, her feasts, her new moons, and her sabbaths, and all her solemn assemblies.
12 Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake, ambayo alisema yalikuwa malipo yake kutoka kwa wapenzi wake; nitaifanya kuwa kichaka, nao wanyama pori wataila.
And I will lay waste her vines and her fig trees, of which she has said, These are my hire that my lovers have given me. And I will make them a forest, and the beasts of the field shall eat them.
13 Nitamwadhibu kwa ajili ya siku alizowafukizia uvumba Mabaali; alipojipamba kwa pete na kwa vito vya thamani, na kuwaendea wapenzi wake, lakini mimi alinisahau,” asema Bwana.
And I will visit upon her the days of the Baalim, to which she burned incense when she decked herself with her earrings and her jewels, and went after her lovers, and forgot me, says Jehovah.
14 “Kwa hiyo sasa nitamshawishi; nitamwongoza hadi jangwani na kuzungumza naye kwa upole.
Therefore, behold, I will allure her, and bring her into the wilderness, and speak soothingly to her.
15 Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu, nami nitalifanya Bonde la Akori mlango wa matumaini. Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake, kama siku zile alizotoka Misri.
And I will give her her vineyards from there, and the valley of Achor for a door of hope. And she shall make answer there, as in the days of her youth, and as in the day when she came up out of the land of Egypt.
16 “Katika siku ile,” asema Bwana, “utaniita mimi ‘Mume wangu’; hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’
And it shall be at that day, says Jehovah, that thou shall call me Ishi, and shall no more call me Baali.
17 Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake, wala hataomba tena kwa majina yao.
For I will take away the names of the Baalim out of her mouth, and they shall no more be mentioned by their name.
18 Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani, na viumbe vile vitambaavyo ardhini. Upinde, upanga na vita, nitaondolea mbali katika nchi, ili kwamba wote waweze kukaa salama.
And in that day I will make a covenant for them with the beasts of the field, and with the birds of the heavens, and with the creeping things of the ground. And I will break the bow and the sword and the battle out of the land, and will make them to lie down safely.
19 Nitakuposa uwe wangu milele; nitakuposa kwa uadilifu na haki, kwa upendo na huruma.
And I will betroth thee to me forever. Yea, I will betroth thee to me in righteousness, and in justice, and in loving kindness, and in mercies.
20 Nitakuposa kwa uaminifu, nawe utamkubali Bwana.
I will even betroth thee to me in faithfulness, and thou shall know Jehovah.
21 “Katika siku ile nitajibu,” asema Bwana, “nitajibu kwa anga, nazo anga zitajibu kwa nchi;
And it shall come to pass in that day, I will answer, says Jehovah. I will answer the heavens, and they shall answer the earth,
22 nayo nchi itajibu kwa nafaka, divai mpya na mafuta, navyo vitajibu kwa Yezreeli.
and the earth shall answer the grain, and the new wine, and the oil, and they shall answer Jezreel.
23 Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe; nami nitaonyesha pendo langu kwake yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.’ Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’ ‘Ninyi ni watu wangu’; nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’”
And I will sow her to me in the earth. And I will have mercy upon her who had not obtained mercy. And I will say to those who were not my people, Thou are my people, and they shall say, My God.

< Hosea 2 >