< Mwanzo 8 >

1 Mungu akamkumbuka Noa na wanyama wote wa porini na wa kufugwa waliokuwa naye ndani ya safina, akatuma upepo ukavuma katika dunia, nayo maji yakaondoka.
And God remembered Noah, and every living animal, and all the cattle that [were] with him in the ark: and God made a wind to pass over the earth, and the waters were checked.
2 Zile chemchemi zilizo chini sana ya ardhi pamoja na malango ya mafuriko ya mbinguni yakawa yamefungwa nayo mvua ikawa imekoma kunyesha kutoka angani.
The fountains also of the deep, and the windows of heaven were stopped, and the rain from heaven was restrained;
3 Maji yakaendelea kupungua taratibu katika nchi. Kunako mwisho wa siku ya 150, maji yalikuwa yamepungua,
And the waters returned from off the earth continually: and after the end of the hundred and fifty days the waters were abated.
4 katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa saba, safina ikatua katika milima ya Ararati.
And the ark rested in the seventh month, on the seventeenth day of the month, upon the mountains of Ararat.
5 Maji yakaendelea kupungua hadi mwezi wa kumi, na siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, vilele vya milima vikaonekana.
And the waters decreased continually, till the tenth month: in the tenth [month], on the first [day] of the month, were the tops of the mountains seen.
6 Baada ya siku arobaini Noa akafungua dirisha alilokuwa amelifanya katika safina
And it came to pass at the end of forty days, that Noah opened the window of the ark which he had made:
7 na akamtoa kunguru, akawa akiruka kwenda na kurudi mpaka maji yalipokwisha kukauka juu ya nchi.
And he sent forth a raven, which went forth to and fro, till the waters were dried from off the earth.
8 Kisha akamtoa hua ili aone kama maji yameondoka juu ya uso wa ardhi.
Also he sent forth a dove from him, to see if the waters were abated from off the face of the ground;
9 Lakini hua hakupata mahali pa kutua kwa kuwa maji yalienea juu ya uso wa dunia yote, kwa hiyo akarudi kwa Noa ndani ya safina. Noa akanyoosha mkono akamchukua yule hua akamrudisha ndani ya safina.
But the dove found no rest for the sole of her foot, and she returned to him into the ark; for the waters [were] on the face of the whole earth. Then he put forth his hand, and took her, and pulled her in to him into the ark.
10 Noa akangojea siku saba zaidi kisha akamtoa tena hua kutoka safina.
And he stayed yet other seven days, and again he sent forth the dove out of the ark;
11 Wakati hua aliporejea kwa Noa jioni, alikuwa amechukua katika mdomo wake jani bichi la mzeituni, lililochumwa wakati ule ule! Ndipo Noa akajua ya kuwa maji yameondoka juu ya uso wa dunia.
And the dove came in to him in the evening, and lo, in her mouth [was] an olive-leaf plucked off: So Noah knew that the waters were abated from off the earth.
12 Akangojea siku saba zaidi na akamtuma tena hua, lakini wakati huu hua hakurudi tena kwa Noa.
And he stayed yet other seven days, and sent forth the dove; which returned not again to him any more.
13 Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka 601, wa kuishi kwake Noa, maji yalikuwa yamekauka duniani. Kisha Noa akafungua mlango wa safina akaona ya kuwa uso wa ardhi ulikuwa umekauka.
And it came to pass in the six hundredth and first year, in the first [month], the first [day] of the month, the waters were dried from off the earth: and Noah removed the covering of the ark, and looked, and behold, the face of the ground was dry.
14 Katika siku ya ishirini na saba ya mwezi wa pili dunia ilikuwa imekauka kabisa.
And in the second month, on the seven and twentieth day of the month, was the earth dried.
15 Ndipo Mungu akamwambia Noa,
And God spoke to Noah, saying,
16 “Toka ndani ya safina, wewe na mkeo na wanao na wake zao.
Go forth from the ark, thou, and thy wife, and thy sons, and thy sons' wives with thee.
17 Utoe nje kila aina ya kiumbe hai aliye pamoja nawe: Ndege, wanyama na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi, ili wakazae, na kuongezeka na kuijaza tena dunia.”
Bring forth with thee every living animal that [is] with thee, of all flesh, of fowl, and of cattle, and of every creeping animal that creepeth upon the earth; that they may breed abundantly on the earth, and be fruitful, and multiply upon the earth.
18 Kwa hiyo Noa akatoka nje pamoja na mkewe, wanawe na wake zao.
And Noah went forth, and his sons, and his wife, and his sons' wives with him:
19 Wanyama wote na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi na ndege wote, kila kitu kiendacho juu ya nchi, aina moja baada ya nyingine vikatoka katika safina, kila aina ya kiumbe, kimoja baada ya kingine.
Every beast, every creeping animal, and every fowl, [and] whatsoever creepeth upon the earth, after their kinds, went out of the ark.
20 Kisha Noa akamjengea Bwana madhabahu, akachukua baadhi ya wale wanyama na ndege wote walio safi, akatoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.
And Noah built an altar to the LORD, and took of every clean beast, and of every clean fowl, and offered burnt-offerings on the altar.
21 Bwana akasikia harufu nzuri ya kupendeza, naye akasema moyoni mwake, “Kamwe sitailaani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, hata ingawa kila mwelekeo wa moyo wake ni mbaya tangu ujana. Kamwe sitaangamiza tena viumbe hai vyote kama nilivyofanya.
And the LORD smelled a sweet savor; and the LORD said in his heart, I will not again curse the ground any more for man's sake; for the imagination of man's heart [is] evil from his youth: neither will I again smite any more every living animal as I have done.
22 “Kwa muda dunia idumupo, wakati wa kupanda na wa kuvuna, wakati wa baridi na wa joto, wakati wa kiangazi na wa masika, usiku na mchana kamwe havitakoma.”
While the earth remaineth, seed-time and harvest, and cold and heat, and summer and winter, and day and night shall not cease.

< Mwanzo 8 >

A Dove is Sent Forth from the Ark
A Dove is Sent Forth from the Ark