< Mwanzo 5 >

1 Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
QUESTA è la descrizione delle generazioni di Adamo. Nel giorno che Iddio creò l'uomo, egli lo fece alla sua somiglianza.
2 Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
Egli li creò maschio e femmina, e li benedisse, e pose loro nome UOMO, nel giorno che furono creati.
3 Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
Ora Adamo, essendo vivuto centotrent'anni, generò [un figliuolo] alla sua somiglianza, secondo la sua immagine; e gli pose nome Set.
4 Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
E il tempo che visse Adamo, dopo ch'ebbe generato Set, fu ottocent'anni; e generò figliuoli e figliuole.
5 Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
Così tutto il tempo che visse Adamo fu novecentrent'anni; poi morì.
6 Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
E Set, essendo vivuto centocinque anni, generò Enos.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
E Set, dopo che ebbe generato Enos, visse ottocensette anni, e generò figliuoli e figliuole.
8 Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
Così tutto il tempo che visse Set fu novecendodici anni; poi morì.
9 Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
Ed Enos, essendo vivuto novant'anni, generò Chenan.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Ed Enos, dopo ch'ebbe generato Chenan, visse ottocenquindici anni, e generò figliuoli e figliuole.
11 Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
Così tutto il tempo che visse Enos fu novecencinque anni; poi morì.
12 Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
E Chenan, essendo vivuto settant'anni, generò Mahalaleel.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
E Chenan, dopo ch'ebbe generato Mahalaleel, visse ottocenquarant'anni, e generò figliuoli e figliuole.
14 Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
Così tutto il tempo che Chenan visse fu novecendieci anni; poi morì.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
E Mahalaleel, essendo vivuto sessantacinque anni, generò Iared.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
E Mahalaleel, dopo ch'ebbe generato Iared, visse ottocentrent'anni, e generò figliuoli e figliuole.
17 Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
Così tutto il tempo che Mahalaleel visse fu ottocennovantacinque anni; poi morì.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
E Iared, essendo vivuto censessantadue anni, generò Enoc.
19 Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
E Iared, dopo ch'ebbe generato Enoc, visse ottocent'anni, e generò figliuoli e figliuole.
20 Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
Così tutto il tempo che Iared visse fu novecensessantadue anni; poi morì.
21 Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
Ed Enoc essendo vivuto sessantacinque anni, generò Metusela.
22 Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Ed Enoc, dopo ch'ebbe generato Metusela, camminò con Dio per lo spazio di trecent'anni e generò figliuoli e figliuole.
23 Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
Così, tutto il tempo che Enoc visse fu trecensessantacinque anni.
24 Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
E dopo che Enoc fu camminato con Dio, non [si vide] più; perciocchè Iddio lo prese.
25 Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
E Metusela, essendo vivuto centottantasette anni, generò Lamec.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
E Metusela, dopo ch'ebbe generato Lamec, visse settecentottantadue anni, e generò figliuoli e figliuole.
27 Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
Così, tutto il tempo che Metusela visse fu novecensessantanove anni; poi morì.
28 Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
E Lamec, essendo vivuto centottantadue anni, generò un figliuolo.
29 Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
E gli pose nome Noè, dicendo: Costui ci consolerà della nostra opera, e della fatica delle nostre mani, [la quale portiamo] per cagion della terra che il Signore ha maladetta.
30 Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
E Lamec, dopo ch'ebbe generato Noè, visse cinquecennovantacinque anni, e generò figliuoli e figliuole.
31 Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
Così tutto il tempo che Lamec visse fu settecensettantasette anni; poi morì.
32 Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.
E Noè, essendo di età di cinquecent'anni, generò Sem, Cam e Iafet.

< Mwanzo 5 >