< Mwanzo 5 >

1 Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
This is the book of the generations of Adam. In the day that God created humankind, he made him in God's likeness.
2 Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
He created them male and female, and blessed them, and called their name "humankind" on the day when they were created.
3 Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
Adam lived two hundred and thirty years, and became the father of a son in his own likeness, after his image, and named him Seth.
4 Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
The days of Adam after he became the father of Seth were seven hundred years, and he became the father of sons and daughters.
5 Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
All the days that Adam lived were nine hundred and thirty years, then he died.
6 Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
Seth lived two hundred and five years, and became the father of Enosh.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Seth lived after he became the father of Enosh seven hundred and seven years, and fathered sons and daughters.
8 Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
All the days of Seth were nine hundred and twelve years, then he died.
9 Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
Enosh lived one hundred and ninety years, and became the father of Kenan.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Enosh lived after he became the father of Kenan, seven hundred and fifteen years, and fathered sons and daughters.
11 Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
All the days of Enosh were nine hundred and five years, then he died.
12 Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
Kenan lived one hundred and seventy years, and became the father of Mahalalel.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Kenan lived after he became the father of Mahalalel seven hundred and forty years, and fathered sons and daughters
14 Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
and all the days of Kenan were nine hundred and ten years, then he died.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
Mahalalel lived one hundred and sixty-five years, and became the father of Jared.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Mahalalel lived after he became the father of Jared seven hundred and thirty years, and fathered sons and daughters.
17 Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
All the days of Mahalalel were eight hundred and ninety-five years, then he died.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
Jared lived one hundred and sixty-two years, and became the father of Enoch.
19 Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Jared lived after he became the father of Enoch eight hundred years, and fathered sons and daughters.
20 Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
All the days of Jared were nine hundred and sixty-two years, then he died.
21 Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
Enoch lived one hundred and sixty-five years, and became the father of Methuselah.
22 Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Enoch walked with God after he became the father of Methuselah two hundred years, and fathered sons and daughters.
23 Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
All the days of Enoch were three hundred and sixty-five years.
24 Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
Enoch walked with God, and then he was not there, for God took him.
25 Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
Methuselah lived one hundred and eighty-seven years, and became the father of Lamech.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Methuselah lived after he became the father of Lamech seven hundred and eighty-two years, and fathered sons and daughters.
27 Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
All the days of Methuselah were nine hundred and sixty-nine years, then he died.
28 Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
Lamech lived one hundred and eighty-two years, and became the father of a son,
29 Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
and he named him Noah, saying, "This one will comfort us in our labor and in the hard work of our hands, because of the ground which God has cursed."
30 Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Lamech lived after he became the father of Noah five hundred and ninety-five years, and fathered sons and daughters.
31 Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
All the days of Lamech were seven hundred and seventy-seven years, then he died.
32 Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.
Noah was five hundred years old, and Noah became the father of Shem, Ham, and Japheth.

< Mwanzo 5 >