< Mwanzo 48 >

1 Baada ya muda Yosefu akaambiwa kwamba, “Baba yako ni mgonjwa.” Kwa hiyo akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu, pamoja naye.
Gdy to się stało, dano znać Józefowi: Oto twój ojciec zachorował. Wziął więc ze sobą swoich dwóch synów, Manassesa i Efraima.
2 Yakobo alipoambiwa, “Mwanao Yosefu amekujia kukuona,” Israeli akakusanya nguvu zake, akaketi kitandani.
I powiedziano Jakubowi: Oto twój syn Józef idzie do ciebie. A Izrael zebrał siłę i usiadł na łożu.
3 Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani, huko akanibariki,
Wtedy Jakub powiedział do Józefa: Bóg Wszechmogący ukazał mi się w Luz, w ziemi Kanaan, i błogosławił mi.
4 naye akaniambia, ‘Nitakufanya ustawi na kuongezeka hesabu yako, nitakufanya kuwa jamii ya mataifa, nami nitakupa nchi hii uimiliki milele wewe na wazao wako baada yako.’
I powiedział do mnie: Oto ja uczynię cię płodnym i rozmnożę cię, i wywiodę z ciebie wielki lud. I dam tę ziemię twemu potomstwu po tobie w wieczne dziedzictwo.
5 “Sasa basi, wanao wawili waliozaliwa kwako huku Misri kabla sijaja hapa kwako watahesabiwa kuwa ni wangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama vile Reubeni na Simeoni walivyo wangu.
Dlatego teraz twoi dwaj synowie, Efraim i Manasses, którzy urodzili ci się w ziemi Egiptu, zanim przyszedłem tu do ciebie do Egiptu, są moimi. Będą moi jak Ruben i Symeon.
6 Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Katika nchi watakayoirithi, watatambuliwa kwa jina la ndugu zao.
Ale twoje dzieci, które spłodzisz po nich, będą twoje; będą zwane w swych posiadłościach imieniem swoich braci.
7 Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani, katika huzuni yangu Raheli alifariki katika nchi ya Kanaani tulipokuwa tungali tukisafiri, tukiwa karibu kufika Efrathi. Kwa hiyo nilimzika huko, kando ya njia iendayo Efrathi” (yaani Bethlehemu).
A gdy wracałem z Paddan, umarła mi Rachela w ziemi Kanaan, w drodze, gdy byłem jeszcze w niewielkiej odległości od Efraty, i pogrzebałem ją tam przy drodze do Efraty, czyli Betlejem.
8 Wakati Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akauliza, “Hawa ni nani?”
A gdy Izrael zobaczył synów Józefa, zapytał: Czyi oni są?
9 Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wana ambao Mungu amenipa nikiwa huku.” Ndipo Israeli akasema, “Walete kwangu ili niwabariki.”
Józef odpowiedział swemu ojcu: To są moi synowie, których Bóg dał mi tutaj. A [on] powiedział: Proszę, przyprowadź ich do mnie, abym im błogosławił.
10 Basi macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee, naye aliona kwa shida. Kwa hiyo Yosefu akawaleta wanawe karibu na baba yake, Israeli akawabusu na akawakumbatia.
A oczy Izraela były tak słabe ze starości, że nie mógł widzieć. I przyprowadził ich do niego, a [Jakub] ich pocałował i uścisnął.
11 Israeli akamwambia Yosefu, “Kamwe sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini sasa Mungu ameniruhusu kuwaona watoto wako pia.”
Potem Izrael powiedział do Józefa: Nie spodziewałem się, że będę jeszcze oglądał twoją twarz, a oto Bóg dał mi widzieć nawet twoje potomstwo.
12 Ndipo Yosefu akawaondoa wanawe magotini mwa Israeli naye akasujudu hadi nchi.
Wtedy Józef odsunął ich od jego kolan i pokłonił się twarzą aż do ziemi.
13 Yosefu akachukua wale wana wawili, Efraimu kwenye mkono wake wa kuume akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kushoto akimwelekeza kwenye mkono wa kuume wa Israeli, akawaleta karibu na babu yao.
Potem Józef wziął obydwu i [postawił] Efraima po swojej prawej ręce, czyli po lewej stronie Izraela; a Manassesa po swojej lewej ręce, czyli po prawej stronie Izraela, i przyprowadził ich do niego.
14 Lakini Israeli akaupeleka mkono wake wa kuume, akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa ndiye mdogo, na mkono wake wa kushoto akaukatisha, akauweka juu ya kichwa cha Manase, ingawa Manase alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza.
Izrael wyciągnął swoją prawą rękę, położył ją na głowę Efraima, który był młodszy, a swoją lewą rękę na głowę Manassesa, umyślnie pokładając swoje ręce, choć pierworodny był Manasses.
15 Ndipo akambariki Yosefu akisema, “Mungu ambaye baba zangu Abrahamu na Isaki walimtii, Mungu ambaye amekuwa mchungaji wa maisha yangu yote mpaka leo hii,
I błogosławił Józefowi, mówiąc: Bóg, przed którego obliczem chodzili moi ojcowie, Abraham i Izaak, Bóg, który mnie żywił od mej młodości aż do dziś;
16 Malaika ambaye aliniokoa kutoka madhara yote, yeye na awabariki vijana hawa. Na waitwe kwa jina langu na kwa majina ya baba zangu Abrahamu na Isaki, wao na waongezeke kwa wingi katika dunia.”
Anioł, który wybawił mnie ze wszelkiego zła, niech błogosławi tym chłopcom i niech będą nazywani [od] mego imienia i od imienia moich ojców, Abrahama i Izaaka, i niech się rozmnożą na ziemi.
17 Yosefu alipoona baba yake akiweka mkono wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa, kwa hiyo akauchukua mkono wa baba yake kutoka kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase.
A gdy Józef zobaczył, że jego ojciec położył swoją prawą rękę na głowę Efraima, nie podobało mu się to. Wziął więc rękę swego ojca, aby ją przenieść z głowy Efraima na głowę Manassesa.
18 Yosefu akamwambia, “Hapana, baba yangu, huyu ndiye mzaliwa wa kwanza; uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”
I Józef powiedział do swego ojca: Nie tak, mój ojcze. Ten bowiem [jest] pierworodny, połóż swoją prawą rękę na jego głowę.
19 Lakini baba yake akakataa, akasema, “Ninajua, mwanangu, ninajua. Yeye pia atakuwa taifa, naye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, nao wazao wake watakuwa kundi la mataifa.”
Ale jego ojciec wzbraniał się i powiedział: Wiem, mój synu, wiem. Ten też stanie się ludem i on też urośnie, ale jego młodszy brat go przewyższy, a z jego potomstwa wyjdzie mnóstwo narodów.
20 Akawabarikia siku ile na kusema, “Kwa jina lenu Israeli watatamka baraka hii: ‘Mungu na awafanye kama Efraimu na Manase.’” Kwa hiyo akamtanguliza Efraimu mbele ya Manase.
Błogosławił im więc tego dnia, mówiąc: Przez ciebie Izrael będzie błogosławił, mówiąc: Niech Bóg cię uczyni jak Efraim i jak Manasses. Tak wyróżnił Efraima przed Manassesem.
21 Ndipo Israeli akamwambia Yosefu, “Mimi ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
Potem Izrael powiedział do Józefa: Oto ja umieram, ale Bóg będzie z wami i przywróci was do ziemi waszych ojców.
22 Kwako wewe, kama aliye juu ya ndugu zako, ninakupa sehemu moja zaidi ya ndugu zako, lile eneo nililoteka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”
Oto daję ci jedną część więcej niż twoim braciom, którą nabyłem moim mieczem i moim łukiem z ręki Amorytów.

< Mwanzo 48 >