< Mwanzo 48 >

1 Baada ya muda Yosefu akaambiwa kwamba, “Baba yako ni mgonjwa.” Kwa hiyo akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu, pamoja naye.
And it came about after these things that someone said to Joseph, "Look, your father is sick." And taking with him his two sons, Manasseh and Ephraim, he went to Jacob.
2 Yakobo alipoambiwa, “Mwanao Yosefu amekujia kukuona,” Israeli akakusanya nguvu zake, akaketi kitandani.
And someone reported to Jacob, and said, "Look, your son Joseph has come to you." Then Israel strengthened himself and sat up in the bed.
3 Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani, huko akanibariki,
And Jacob said to Joseph, "El Shaddai appeared to me at Luz in the land of Canaan and blessed me,
4 naye akaniambia, ‘Nitakufanya ustawi na kuongezeka hesabu yako, nitakufanya kuwa jamii ya mataifa, nami nitakupa nchi hii uimiliki milele wewe na wazao wako baada yako.’
and said to me, 'Look, I will make you fruitful and multiply you, and I will make of you a company of peoples, and will give this land to your descendants after you as an everlasting possession.'
5 “Sasa basi, wanao wawili waliozaliwa kwako huku Misri kabla sijaja hapa kwako watahesabiwa kuwa ni wangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama vile Reubeni na Simeoni walivyo wangu.
And now your two sons, who were born to you in the land of Egypt before I came to you into Egypt, are mine; Ephraim and Manasseh will be mine, as Reuben and Simeon are.
6 Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Katika nchi watakayoirithi, watatambuliwa kwa jina la ndugu zao.
And your offspring born to you after them will be yours. But in their inheritance they are to be called after the names of their brothers.
7 Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani, katika huzuni yangu Raheli alifariki katika nchi ya Kanaani tulipokuwa tungali tukisafiri, tukiwa karibu kufika Efrathi. Kwa hiyo nilimzika huko, kando ya njia iendayo Efrathi” (yaani Bethlehemu).
But as for me, when I came from Paddan Aram, Rachel died, in my sorrow, in the land of Canaan on the journey, when there was still some distance to go to Ephrath. And I buried her there on the way to Ephrath (that is, Bethlehem)."
8 Wakati Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akauliza, “Hawa ni nani?”
Then Israel saw Joseph's sons, and said, "Who are these?"
9 Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wana ambao Mungu amenipa nikiwa huku.” Ndipo Israeli akasema, “Walete kwangu ili niwabariki.”
And Joseph said to his father, "They are my sons, whom God has given me here." And he said, "Please bring them to me, so that I can bless them."
10 Basi macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee, naye aliona kwa shida. Kwa hiyo Yosefu akawaleta wanawe karibu na baba yake, Israeli akawabusu na akawakumbatia.
Now the eyes of Israel were failing because of his age, so that he couldn't see. Then he brought them near to him, and he kissed them and embraced them.
11 Israeli akamwambia Yosefu, “Kamwe sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini sasa Mungu ameniruhusu kuwaona watoto wako pia.”
And Israel said to Joseph, "I did not expect to see your face, but look, God has let me see your offspring as well."
12 Ndipo Yosefu akawaondoa wanawe magotini mwa Israeli naye akasujudu hadi nchi.
Then Joseph brought them out from between his knees, and he bowed himself with his face to the ground.
13 Yosefu akachukua wale wana wawili, Efraimu kwenye mkono wake wa kuume akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kushoto akimwelekeza kwenye mkono wa kuume wa Israeli, akawaleta karibu na babu yao.
And Joseph took them both, Ephraim in his right hand toward Israel's left hand, and Manasseh in his left hand toward Israel's right hand, and brought them near to him.
14 Lakini Israeli akaupeleka mkono wake wa kuume, akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa ndiye mdogo, na mkono wake wa kushoto akaukatisha, akauweka juu ya kichwa cha Manase, ingawa Manase alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza.
And Israel stretched out his right hand and placed it on Ephraim's head, who was the younger, and his left hand on Manasseh's head, crossing his hands, although Manasseh was the firstborn.
15 Ndipo akambariki Yosefu akisema, “Mungu ambaye baba zangu Abrahamu na Isaki walimtii, Mungu ambaye amekuwa mchungaji wa maisha yangu yote mpaka leo hii,
Then he blessed Joseph, and said, "The God before whom my fathers Abraham and Isaac walked, the God who has been my shepherd all my life to this day,
16 Malaika ambaye aliniokoa kutoka madhara yote, yeye na awabariki vijana hawa. Na waitwe kwa jina langu na kwa majina ya baba zangu Abrahamu na Isaki, wao na waongezeke kwa wingi katika dunia.”
the Angel who has redeemed me from all evil, bless the boys. And may my name be carried on in them, and the names of my fathers Abraham and Isaac. And may they grow into a multitude upon the earth."
17 Yosefu alipoona baba yake akiweka mkono wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa, kwa hiyo akauchukua mkono wa baba yake kutoka kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase.
When Joseph saw that his father placed his right hand on the head of Ephraim, it displeased him, and he grasped his father's hand to move it from Ephraim's head to Manasseh's head.
18 Yosefu akamwambia, “Hapana, baba yangu, huyu ndiye mzaliwa wa kwanza; uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”
And Joseph said to his father, "Not so, my father, for this one is the firstborn. Put your right hand on his head."
19 Lakini baba yake akakataa, akasema, “Ninajua, mwanangu, ninajua. Yeye pia atakuwa taifa, naye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, nao wazao wake watakuwa kundi la mataifa.”
But his father refused, and said, "I know, my son, I know. He also will become a people, and he also will be great. However, his younger brother will be greater than he, and his descendants will become a multitude of nations."
20 Akawabarikia siku ile na kusema, “Kwa jina lenu Israeli watatamka baraka hii: ‘Mungu na awafanye kama Efraimu na Manase.’” Kwa hiyo akamtanguliza Efraimu mbele ya Manase.
So he blessed them that day, saying, "By you Israel will pronounce blessing, saying, 'God make you as Ephraim and as Manasseh.'" Thus he put Ephraim before Manasseh.
21 Ndipo Israeli akamwambia Yosefu, “Mimi ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
Then Israel said to Joseph, "Look, I am about to die, but God will be with you, and God will bring you back from this land to the land of your fathers.
22 Kwako wewe, kama aliye juu ya ndugu zako, ninakupa sehemu moja zaidi ya ndugu zako, lile eneo nililoteka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”
Moreover, I give to you one portion more than your brothers, which I took out of the hand of the Amorites with my sword and with my bow."

< Mwanzo 48 >