< Mwanzo 44 >

1 Kisha Yosefu akampa yule msimamizi wa nyumbani mwake maagizo haya: “Jaza magunia ya watu hawa kiasi cha chakula ambacho wanaweza kuchukua, na uweke fedha ya kila mtu kwenye mdomo wa gunia lake.
Wtedy [Józef] rozkazał zarządcy swego domu: Napełnij wory tych ludzi zbożem, ile tylko mogą unieść, a pieniądze każdego włóż na wierzch jego wora.
2 Kisha weka kikombe changu kile cha fedha kwenye mdomo wa gunia la yule mdogo wa wote pamoja na fedha zake ambazo angenunulia nafaka yake.” Naye akafanya kama Yosefu alivyosema.
Mój kielich też, kielich srebrny, włóż na wierzch wora najmłodszego razem z pieniędzmi za zboże. I zrobił według słów Józefa, jak mu rozkazał.
3 Kulipopambazuka, hao watu wakaruhusiwa kuondoka pamoja na punda zao.
O świcie wyprawiono tych ludzi razem z ich osłami.
4 Kabla hawajafika mbali kutoka mjini, Yosefu akamwambia mtumishi wake, “Wafuatilie wale watu mara moja, utakapowakuta, waambie, ‘Kwa nini mmelipiza wema kwa ubaya?
Gdy wyszli z miasta i byli niedaleko, Józef powiedział do zarządcy swego domu: Wstań, goń tych ludzi, a gdy ich dogonisz, powiedz do nich: Czemu oddaliście złem za dobro?
5 Je, kikombe hiki sicho anachonywea bwana wangu na pia hukitumia kwa kutabiri mambo yajayo? Hili ni jambo ovu mlilolitenda.’”
Czy to nie jest [kielich], z którego pija mój pan i z którego wróży? Źle postąpiliście, dopuszczając się tego.
6 Alipowafikia, akarudia maneno haya kwao.
[Ten] dogonił ich więc i powiedział do nich te słowa.
7 Lakini wakamwambia mtumishi, “Kwa nini bwana wangu anasema maneno kama haya? Liwe mbali na watumishi wako wasije wakafanya jambo kama hilo!
Ale [oni] mu odpowiedzieli: Dlaczego mój pan mówi takie słowa? Nie daj Boże, aby twoi słudzy mieli tak postąpić.
8 Hata hivyo tulikurudishia zile fedha kutoka nchi ya Kanaani ambazo tulizikuta kwenye midomo ya magunia yetu. Hivyo kwa nini tuibe fedha au dhahabu kutoka nyumbani kwa bwana wako?
Przecież pieniądze, które znaleźliśmy na wierzchu naszych worów, przynieśliśmy do ciebie z powrotem z ziemi Kanaan. Jakże mielibyśmy kraść z domu twego pana srebro lub złoto?
9 Ikiwa yeyote miongoni mwa watumishi wako atapatikana nacho, auawe, na sisi wengine tutakuwa watumwa wa bwana wangu.”
U którego z twoich sług to się znajdzie, niech umrze, a my będziemy niewolnikami mego pana.
10 Akajibu, “Vema sana; na iwe kama msemavyo. Yeyote atakayekutwa nacho atakuwa mtumwa wangu, lakini ninyi wengine mtakuwa hamna lawama.”
[On] powiedział: Niech będzie tak, jak mówicie. Przy którym znajdzie się kielich, ten będzie niewolnikiem, a wy będziecie niewinni.
11 Kila mmoja wao akafanya haraka kushusha gunia lake chini na kulifungua.
Wtedy każdy szybko zdjął swój wór na ziemię i rozwiązał go.
12 Ndipo msimamizi akaendelea kutafuta, akianzia kwa mkubwa wa wote na akaishia kwa mdogo wa wote. Basi kikombe kikapatikana katika gunia la Benyamini.
I szukał, zaczynając od starszego, a kończąc na najmłodszym. I znalazł kielich w worze Beniamina.
13 Kwa jambo hili, wakararua nguo zao. Ndipo wote wakapakiza mizigo yao juu ya punda zao na kurudi mjini.
Wtedy rozdarli swoje szaty, każdy załadował swego osła i wrócili do miasta.
14 Yosefu alikuwa bado yuko nyumbani mwake wakati Yuda na kaka zake walipoingia, wote wakajitupa chini mbele yake.
Przyszedł więc Juda i jego bracia do domu Józefa, który tam jeszcze był. I upadli przed nim na ziemię.
15 Yosefu akawaambia, “Ni jambo gani hili mlilolifanya? Hamjui kuwa mtu kama mimi anaweza kufahamu mambo kwa njia ya kutabiri?”
I Józef zapytał ich: Co zrobiliście? Czy nie wiedzieliście, że [taki] człowiek jak ja potrafi wróżyć?
16 Yuda akajibu, “Tutaweza kusema nini kwa bwana wangu? Tutaweza kuzungumza nini? Tutawezaje kuthibitisha kwamba hatuna hatia? Mungu amefunua hatia ya watumishi wako. Sasa sisi tu watumwa wa bwana wangu, sisi wenyewe pamoja na yule aliyepatikana na kikombe.”
Wtedy Juda odpowiedział: Cóż możemy odpowiedzieć memu panu? Co możemy mówić i jak mamy się usprawiedliwić? Bóg znalazł nieprawość u twoich sług. Oto jesteśmy niewolnikami mego pana, zarówno my, jak i ten, u którego znalazł się kielich.
17 Lakini Yosefu alisema, “Liwe mbali nami kufanya jambo kama hili! Mtu yule tu aliyekutwa na kikombe ndiye atakayekuwa mtumwa wangu. Ninyi wengine, rudini kwa baba yenu kwa amani.”
A on odpowiedział: Nie daj Boże, abym miał tak uczynić. Człowiek, w którego ręku znaleziono kielich, będzie moim niewolnikiem. Wy zaś jedźcie w pokoju do waszego ojca.
18 Ndipo Yuda akamwendea na kumwambia: “Tafadhali bwana wangu, mruhusu mtumishi wako aseme neno kwa bwana wangu. Usimkasirikie mtumishi wako, ingawa wewe ni sawa na Farao mwenyewe.
Wtedy Juda podszedł do niego i powiedział: Mój panie! [Pozwól] twemu słudze mówić słowo do uszu mego pana, a niech nie zapala się twój gniew na twego sługę, gdyż ty jesteś jak sam faraon.
19 Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, ‘Mnaye baba au ndugu?’
Mój pan pytał swoich sług: Czy macie ojca albo brata?
20 Nasi tukakujibu, ‘Tunaye baba yetu ambaye ni mzee; pia yupo mwanawe mdogo aliyezaliwa katika uzee wake. Ndugu yake amekufa, na huyu mdogo ndiye mwana pekee kwa mama yake aliyebaki, naye baba yake anampenda.’
Wtedy odpowiedzieliśmy memu panu: Mamy ojca, starca, i chłopca małego [spłodzonego] w jego starości. Jego brat umarł i tylko on został [po] swej matce, i jego ojciec go kocha.
21 “Ndipo ulipowaambia watumishi wako, ‘Mleteni kwangu ili niweze kumwona kwa macho yangu mwenyewe.’
Potem mówiłeś [do nas], swoich sług: Przyprowadźcie go do mnie, abym mógł go zobaczyć własnymi oczyma.
22 Nasi tukamwambia bwana wangu, ‘Kijana hawezi kumwacha baba yake; akimwacha, baba yake atakufa.’
I mówiliśmy do mego pana: Chłopiec nie będzie mógł opuścić swego ojca, bo gdyby opuścił swego ojca, ten by umarł.
23 Lakini ukawaambia watumishi wako, ‘Ndugu yenu mdogo asiposhuka pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.’
Wtedy powiedziałeś do swoich sług: Jeśli nie przyjdzie z wami wasz najmłodszy brat, więcej nie zobaczycie mojej twarzy.
24 Tuliporudi nyumbani kwa mtumwa wako baba yangu, tulimwambia lile bwana wangu alilokuwa amesema.
Gdy więc przyszliśmy do twego sługi, mego ojca, powtórzyliśmy mu te słowa mego pana.
25 “Ndipo baba yetu aliposema, ‘Rudini Misri mkanunue chakula kingine.’
Wtedy nasz ojciec powiedział: Jedźcie znowu i kupcie nam trochę żywności.
26 Lakini tukamwambia, ‘Hatuwezi kushuka Misri mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi ndipo tutakapokwenda. Hatutaweza kuuona uso wa yule mtu mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi.’
I powiedzieliśmy: Nie możemy [tam] iść. Lecz jeśli [będzie] z nami nasz najmłodszy brat, wtedy pojedziemy. Bo nie będziemy mogli zobaczyć twarzy tego człowieka, jeśli nie będzie z nami naszego najmłodszego brata.
27 “Mtumwa wako baba yangu alituambia, ‘Mnajua mke wangu alinizalia wana wawili.
I twój sługa, mój ojciec, powiedział do nas: Wy wiecie, że moja żona urodziła mi dwóch [synów].
28 Mmojawapo alipotea, nami nikasema, “Hakika ameraruliwa vipande vipande.” Nami sijamwona tangu wakati huo.
Jeden wyszedł ode mnie i powiedziałem: Na pewno został rozszarpany [przez zwierzę] i nie widziałem go do dziś.
29 Ikiwa mtaniondolea huyu tena na akapatwa na madhara, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini nikiwa mwenye huzuni.’ (Sheol h7585)
A jeśli zabierzecie mi też tego i spotka go nieszczęście, wtedy w żalu doprowadzicie mnie, osiwiałego, do grobu. (Sheol h7585)
30 “Hivyo sasa, kama kijana hatakuwa pamoja nasi nitakaporudi kwa mtumishi wako baba yangu, na kama baba yangu, ambaye maisha yake yamefungamanishwa na uhai wa kijana huyu,
Dlatego jeśli przyjdę do twego sługi, mojego ojca, a nie będzie z nami chłopca, z którym jest bardzo związany;
31 akiona kijana hayupo nasi, atakufa. Watumishi wako watashusha kichwa chenye mvi cha baba yetu kaburini kwa huzuni. (Sheol h7585)
Stanie się tak, że jak tylko zobaczy, że chłopca nie ma, umrze. A twoi słudzy doprowadzą twego sługę, naszego ojca, osiwiałego, z żalu do grobu. (Sheol h7585)
32 Mtumwa wako alimhakikishia baba yangu usalama wa kijana. Nikamwambia, ‘Kama sikumrudisha kwako nitakuwa mwenye lawama mbele yako, baba yangu, maisha yangu yote!’
Bo twój sługa wziął na siebie odpowiedzialność przed ojcem i mówił: Jeśli go nie przyprowadzę, będę po wszystkie dni winien grzechu przeciw mojemu ojcu.
33 “Sasa basi, tafadhali mruhusu mtumishi abaki hapa kama mtumwa wa bwana wangu badala ya kijana, naye kijana umruhusu arudi na ndugu zake.
Teraz więc, proszę, niech twój sługa zostanie niewolnikiem mego pana zamiast tego chłopca, a niech chłopak idzie ze swymi braćmi.
34 Ninawezaje kurudi kwa baba yangu kama kijana hatakuwa pamoja nami? La hasha! Usiniache nikaone huzuni ile itakayompata baba yangu.”
Bo jak ja mam wrócić do mego ojca, gdy nie będzie ze mną tego chłopca? Nie chciałbym patrzeć na rozpacz, która by dotknęła mego ojca.

< Mwanzo 44 >