< Mwanzo 42 >

1 Wakati Yakobo alipofahamu kuwa kuna nafaka huko Misri, akawaambia wanawe, “Mbona mnakaa tu hapa mnatazamana?”
Now Jacob learned that there was grain in Egypt, so Jacob said to his sons, "Why do you look at one another?"
2 Akaendelea kuwaambia, “Nimesikia kuwa huko Misri kuna nafaka. Telemkeni huko mkanunue chakula kwa ajili yetu, ili tuweze kuishi wala tusife.”
He said, "Look, I have heard that there is grain in Egypt. Go down there and buy some for us from there, so that we may live and not die."
3 Ndipo wale ndugu kumi wa Yosefu, wakateremka huko Misri kununua nafaka.
So Joseph's ten brothers went down to buy grain from Egypt.
4 Lakini Yakobo hakumtuma Benyamini, ndugu yake Yosefu, pamoja na wengine, kwa sababu aliogopa asije akapatwa na madhara.
But Jacob did not send Joseph's brother Benjamin with his brothers, for he said, "Some harm might happen to him."
5 Hivyo wana wa Israeli walikuwa miongoni mwa wale waliokwenda Misri kununua nafaka, kwani njaa ilikuwa katika nchi ya Kanaani pia.
So the sons of Israel went to buy among the other travelers, for the famine was in the land of Canaan.
6 Wakati huo Yosefu alikuwa mtawala wa nchi ya Misri, naye alikuwa ndiye aliwauzia watu wote nafaka. Kwa hiyo wakati ndugu zake Yosefu walipofika, wakamsujudia hadi nyuso zao zikagusa ardhi.
Now Joseph was the ruler over the country, and it was he who sold to all the people of the land. Joseph's brothers came and bowed themselves down to him with their faces to the ground.
7 Mara Yosefu alipowaona ndugu zake, akawatambua, lakini akajifanya mgeni na kuzungumza nao kwa ukali, akiwauliza, “Ninyi mnatoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka katika nchi ya Kanaani kuja kununua chakula.”
Joseph saw his brothers, and he recognized them, but he acted like he did not know them, and spoke harshly with them. And he said to them, "Where do you come from?" And they said, "From the land of Canaan to buy food."
8 Ingawa Yosefu aliwatambua ndugu zake, wao hawakumtambua.
So Joseph recognized his brothers, but they did not recognize him.
9 Ndipo Yosefu alipokumbuka ndoto zake kuwahusu wao, akawaambia, “Ninyi ni wapelelezi! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
Then Joseph remembered the dreams which he dreamed about them, and said to them, "You are spies. You have come to look for the vulnerabilities of the country."
10 Wakamjibu, “Sivyo bwana wangu. Watumishi wako wamekuja kununua chakula.
But they said to him, "No, my lord, but your servants have come to buy food.
11 Sisi sote ni wana wa baba mmoja. Watumishi wako ni watu waaminifu, wala sio wapelelezi.”
We are all sons of one man. We are honest men. Your servants are not spies."
12 Akawaambia, “La hasha! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
But he said to them, "No, but you have come to look for the vulnerabilities of the country."
13 Lakini wakamjibu, “Watumishi wako walikuwa kumi na wawili, wana wa mtu mmoja ambaye anaishi katika nchi ya Kanaani. Sasa mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu na mwingine alikufa.”
But they said, "We, your servants, are twelve brothers, the sons of one man in the land of Canaan; and look, the youngest is now with our father, and one is no more."
14 Yosefu akawaambia, “Ni sawa kabisa kama nilivyowaambia: Ninyi ni wapelelezi!
But Joseph said to them, "It is as I said to you, saying, 'You are spies.'
15 Na hivi ndivyo mtakavyojaribiwa: Hakika kama Farao aishivyo, hamtaondoka mahali hapa mpaka ndugu yenu mdogo aje hapa.
This is how you will be tested. By the life of Pharaoh, you will not leave from here until your youngest brother comes here.
16 Tumeni mmoja wenu akamlete huyo ndugu yenu, wengine mtawekwa gerezani, ili maneno yenu yajaribiwe kuona kama mnasema kweli. La sivyo, hakika kama Farao aishivyo ninyi ni wapelelezi!”
Send one of you, and let him get your brother, and you will stay in prison, so that your words can be tested, whether there is truth in you. Or else, by the life of Pharaoh, surely you are spies."
17 Akawaweka wote chini ya ulinzi kwa siku tatu.
So he put all of them together in prison for three days.
18 Siku ya tatu Yosefu akawaambia, “Fanyeni hili nanyi mtaishi, kwa maana namwogopa Mungu:
Then Joseph said to them the third day, "Do what I say, and live, for I fear God.
19 Ikiwa ninyi ni watu waaminifu, mmoja wa ndugu zenu na abaki kifungoni, nanyi wengine pelekeni nafaka kwa jamaa yenu wanaoteseka kwa njaa.
If you are honest, then let one of your brothers remain confined in your prison; but you go and carry grain for the hunger of your households.
20 Lakini ni lazima mniletee ndugu yenu mdogo hapa, ili maneno yenu yathibitike na kwamba msife.” Wakakubali kufanya hivyo.
But bring your youngest brother to me so that your words will be verified, and you won't die." To this they agreed.
21 Wakaambiana wao kwa wao, “Hakika tunaadhibiwa kwa sababu ya ndugu yetu. Tuliona jinsi alivyohuzunika alipokuwa anatusihi kuponya maisha yake, lakini hatukumsikiliza, hiyo ndiyo sababu dhiki hii imetupata.”
Then they said to one another, "We are certainly guilty concerning our brother, because we saw how distressed he was when he pleaded with us, and we wouldn't listen. Therefore this distress has come upon us."
22 Reubeni akawajibu, “Sikuwaambieni msitende dhambi dhidi ya kijana? Lakini hamkunisikiliza! Sasa ni lazima tuadhibiwe kwa ajili ya damu yake.”
Reuben answered them, saying, "Did I not tell you, saying, 'Do not sin against the boy,' but you wouldn't listen? Therefore, look, now comes a reckoning for his blood."
23 Hawakujua kuwa Yosefu angewaelewa, kwa sababu alitumia mkalimani.
Now they did not know that Joseph could understand them, since he was speaking through an interpreter.
24 Yosefu akajitenga nao akaanza kulia, kisha akawarudia na kuzungumza nao tena. Akataka Simeoni akamatwe na kufungwa mbele yao.
He stepped away from them and wept. Then he returned to them and talked with them. Then he took Simeon from them and bound him in front of them.
25 Yosefu akatoa amri ya kujaza magunia yao nafaka na kuweka fedha ya kila mmoja ndani ya gunia lake, kisha wapewe mahitaji ya njiani. Baada ya kufanyiwa hayo yote,
Then Joseph gave orders to fill their bags with grain, and to restore every man's silver into his sack, and to give them food for the journey. And it was done for them.
26 wakapakiza nafaka juu ya punda zao, wakaondoka.
They loaded their donkeys with their grain, and departed from there.
27 Walipofika mahali pa kulala huko njiani mmoja wao akafungua gunia lake ili amlishe punda wake, akakuta fedha yake kwenye mdomo wa gunia lake.
As one of them opened his sack to give his donkey food at the lodging place, he saw his silver. Look, it was in the mouth of his sack.
28 Akawaambia ndugu zake, “Fedha yangu imerudishwa. Iko ndani ya gunia langu.” Mioyo yao ikazimia, na kila mmoja akamgeukia mwenzake wakitetemeka, wakaulizana, “Ni nini hiki Mungu alichotufanyia?”
He said to his brothers, "My silver has been returned. Look, it is in my sack." And they were dismayed, and they turned trembling to one another, saying, "What is this that God has done to us?"
29 Walipofika kwa Yakobo baba yao katika nchi ya Kanaani, wakamweleza mambo yote yaliyowapata. Wakasema,
Then they returned to their father Jacob to the land of Canaan, and told him all that had happened to them, saying,
30 “Huyo mtu ambaye ndiye bwana katika nchi hiyo alisema nasi kwa ukali, akatutendea kana kwamba sisi tulikuwa tunaipeleleza nchi.
"The man, the lord of the country, spoke harshly to us, and he put us in custody as spies of the country.
31 Lakini tulimwambia, ‘Sisi ni watu waaminifu, sio wapelelezi.
But we said to him, 'We are honest men. We are not spies.
32 Tulizaliwa ndugu kumi na wawili, wana wa baba mmoja. Mmoja alikufa, na mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu huko Kanaani.’
We are twelve brothers, sons of our father; one is no more, and the youngest is now with our father in the land of Canaan.'
33 “Ndipo huyo mtu aliye bwana katika nchi hiyo alipotuambia, ‘Hivi ndivyo nitafahamu kuwa ninyi ni watu waaminifu: Mwacheni mmoja wa ndugu zenu pamoja nami hapa, kisha nendeni mpeleke chakula kwa ajili ya jamaa yenu inayoteseka kwa njaa.
The man, the lord of the country, said to us, 'By this I will know that you are honest men: leave one of your brothers with me, and take grain for the hunger of your households, and go your way.
34 Lakini mleteni huyo ndugu yenu mdogo kwangu, ndipo nitajua kuwa ninyi sio wapelelezi, ila ni watu waaminifu. Kisha nitamrudisha ndugu yenu, nanyi mtaweza kufanya biashara katika nchi hii.’”
Bring your youngest brother to me. Then I will know that you are not spies, but that you are honest men. So I will deliver your brother to you, and you may travel in the land.'"
35 Walipokuwa wanamimina nafaka kutoka kwenye magunia yao, ndani ya gunia la kila mtu kulikuwa na mfuko wa fedha! Wakati wao na baba yao walipoona mifuko ya fedha, wakaogopa.
Then it happened as they emptied their sacks, that look, every man's bag of silver was in his sack. When they and their father saw their bags of silver, they were afraid.
36 Yakobo baba yao akawaambia, “Ninyi mmenipokonya watoto wangu. Yosefu hayupo na Simeoni hayupo tena na sasa mnataka kumchukua Benyamini. Kila kitu ni kinyume nami!”
Then their father Jacob said to them, "You have deprived me of my children. Joseph is no more, Simeon is no more, and you want to take Benjamin away. All this has come against me."
37 Ndipo Reubeni akamwambia baba yake, “Waweza kuwaua wanangu wote wawili, ikiwa sitamrudisha Benyamini kwako. Mkabidhi Benyamini katika uangalizi wangu, nami nitamrudisha.”
Reuben spoke to his father, saying, "Kill my two sons if I do not bring him to you. Put him in my care, and I will bring him back to you."
38 Lakini Yakobo akasema, “Mwanangu hatashuka huko pamoja nanyi; ndugu yake amekufa naye ndiye peke yake aliyebaki. Ikiwa atapatwa na madhara katika safari mnayoiendea, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini kwa masikitiko.” (Sheol h7585)
But he said, "My son will not go down with you, for his brother is dead, and he alone is left. If harm should happen to him on the journey you are taking, then you will bring down my gray hairs with sorrow to Sheol." (Sheol h7585)

< Mwanzo 42 >