< Mwanzo 36 >

1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).
Now these are the generations of Esau (that is, Edom).
2 Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi,
Esau took his wives from the daughters of Canaan: Adah the daughter of Elon, the Hethite; and Oholibamah the daughter of Anah, the daughter of Zibeon, the Hivite;
3 pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.
and Basemath, Ishmael's daughter, sister of Nebaioth.
4 Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli,
Adah bore to Esau Eliphaz. Basemath bore Reuel.
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.
Oholibamah bore Jeush, and Jalam, and Korah. These are the sons of Esau, who were born to him in the land of Canaan.
6 Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake.
Esau took his wives, his sons, his daughters, and all the people of his household, with his livestock, all his animals, and all of the property he had acquired in the land of Canaan, and went out from the land of Canaan away from the presence of his brother Jacob.
7 Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao.
For their possessions were too great for them to remain together, and the land in which they were traveling could not support them because of their livestock.
8 Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.
And Esau (also known as Edom) settled in the hill country of Seir.
9 Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.
These are the generations of Esau the father of the Edomites in the hill country of Seir:
10 Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.
these are the names of Esau's sons: Eliphaz, the son of Adah, the wife of Esau; and Reuel, the son of Basemath, the wife of Esau.
11 Wana wa Elifazi ni: Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.
The sons of Eliphaz were Teman, Omar, Zepho, and Gatam, and Kenaz.
12 Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.
Timna was the secondary wife to Eliphaz, Esau's son; and she bore to Eliphaz Amalek. These are the sons of Adah, Esau's wife.
13 Wana wa Reueli ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.
These are the sons of Reuel: Nahath, and Zerah, Shammah, and Mizzah. These were the sons of Basemath, Esau's wife.
14 Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni: Yeushi, Yalamu na Kora.
These were the sons of Oholibamah, the daughter of Anah, the daughter of Zibeon, Esau's wife: she bore to Esau Jeush, and Jalam, and Korah.
15 Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau: Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni: Temani, Omari, Sefo, Kenazi,
These are the chiefs of the sons of Esau: the sons of Eliphaz the firstborn of Esau: chief Teman, chief Omar, chief Zepho, chief Kenaz,
16 Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.
chief Korah, chief Gatam, chief Amalek: these are the chiefs who came of Eliphaz in the land of Edom; these are the sons of Adah.
17 Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.
These are the sons of Reuel, Esau's son: chief Nahath, chief Zerah, chief Shammah, chief Mizzah: these are the chiefs of Reuel in the land of Edom; these are the sons of Basemath, Esau's wife.
18 Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni: Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.
These are the sons of Oholibamah, Esau's wife: chief Jeush, chief Jalam, chief Korah: these are the chiefs who came of Oholibamah the daughter of Anah, Esau's wife.
19 Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.
These are the sons of Esau (also known as Edom), and these are their chiefs.
20 Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
These are the sons of Seir the Horite, the inhabitants of the land: Lotan, and Shobal, and Zibeon, and Anah,
21 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.
and Dishon, and Ezer, and Dishan. These are the chiefs of the Horites, the sons of Seir in the land of Edom.
22 Wana wa Lotani walikuwa: Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.
The sons of Lotan were Hori and Hemam. Lotan's sister was Timna.
23 Wana wa Shobali walikuwa: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.
These are the sons of Shobal: Alvan, and Manahath, and Ebal, Shepho, and Onam.
24 Wana wa Sibeoni walikuwa: Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.
These are the sons of Zibeon: Aiah and Anah. This is the Anah who found the hot springs in the desert as he pastured the donkeys of his father Zibeon.
25 Watoto wa Ana walikuwa: Dishoni na Oholibama binti wa Ana.
These are the children of Anah: Dishon, and Oholibamah the daughter of Anah.
26 Wana wa Dishoni walikuwa: Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.
These are the children of Dishon: Hemdan, and Eshban, and Ithran, and Keran.
27 Wana wa Eseri walikuwa: Bilhani, Zaavani na Akani.
These are the sons of Ezer: Bilhan, and Zaavan, and Akan.
28 Wana wa Dishani walikuwa: Usi na Arani.
These are the sons of Dishan: Uz and Aran.
29 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
These are the chiefs of the Horites: chief Lotan, chief Shobal, chief Zibeon, chief Anah,
30 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.
chief Dishon, chief Ezer, and chief Dishan: these are the chiefs who came of the Horites, according to their chiefs in the land of Seir.
31 Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:
These are the kings who reigned in the land of Edom, before any king reigned over the children of Israel.
32 Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.
Bela the son of Beor reigned in Edom. The name of his city was Dinhabah.
33 Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.
When Bela died, and Jobab, the son of Zerah of Bozrah reigned in his place.
34 Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.
And Jobab died, and Husham of the land of the Temanites reigned in his place.
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.
And Husham died, and Hadad the son of Bedad who struck Midian in the field of Moab reigned in his place. The name of his city was Avith.
36 Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.
And Hadad died, and Samlah of Masrekah reigned in his place.
37 Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.
And Samlah died, and Shaul of Rehoboth-on-the-River reigned in his place.
38 Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.
And Shaul died, and Baal Hanan the son of Achbor reigned in his place.
39 Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.
And Baal Hanan the son of Achbor died, and Hadad reigned in his place. The name of his city was Pau. His wife's name was Mehetabel, the daughter of Matred, the daughter of Me-Zahab.
40 Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao: Timna, Alva, Yethethi,
These are the names of the chiefs who came from Esau, according to their families, according to their places, and by their names: chief Timna, chief Alvah, chief Jetheth,
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
chief Oholibamah, chief Elah, chief Pinon,
42 Kenazi, Temani, Mibsari,
chief Kenaz, chief Teman, chief Mibzar,
43 Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki. Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.
chief Magdiel, and chief Iram. These are the chiefs of Edom, according to their settlements in the land they possessed. This is Esau the father of Edom.

< Mwanzo 36 >