< Mwanzo 35 >

1 Kisha Mungu akamwambia Yakobo, “Panda uende Betheli ukakae huko na ukamjengee Mungu madhabahu huko, Yeye aliyekutokea ulipokuwa unamkimbia Esau ndugu yako.”
And God said to Jacob, Arise, go up to Bethel, and dwell there: and make there an altar to God, that appeared to you when you fled from the face of Esau your brother.
2 Hivyo Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake pamoja na wote waliokuwa naye, “Iondoeni miungu ya kigeni ile iliyoko katikati yenu, jitakaseni na mkabadilishe nguo zenu.
Then Jacob said to his household, and to all that were with him, Put away the strange gods that are among you, and be clean, and change your garments:
3 Kisha njooni, twende Betheli, mahali nitakapomjengea Mungu madhabahu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, ambaye amekuwa pamoja nami popote nilipokwenda.”
And let us arise, and go up to Bethel; and I will make there an altar to God, who answered me in the day of my distress, and was with me in the way which I went.
4 Kwa hiyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni waliyokuwa nayo, pamoja na pete zilizokuwa masikioni mwao. Yakobo akavizika chini ya mti wa mwaloni huko Shekemu.
And they gave to Jacob all the strange gods which were in their hand, and all their earrings which were in their ears; and Jacob hid them under the oak which was by Shechem.
5 Kisha wakaondoka, na hofu ya Mungu ikawapata miji yote iliyowazunguka. Kwa hiyo hakuna aliyewafuatia wana wa Yakobo.
And they journeyed: and the terror of God was on the cities that were round about them, and they did not pursue after the sons of Jacob.
6 Yakobo na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafika Luzu (ndio Betheli), katika nchi ya Kanaani.
So Jacob came to Luz, which is in the land of Canaan, that is, Bethel, he and all the people that were with him.
7 Huko akajenga madhabahu na akapaita mahali pale El-Betheli, kwa sababu mahali pale ndipo Mungu alipojifunua kwake alipokuwa akimkimbia ndugu yake.
And he built there an altar, and called the place Elbethel: because there God appeared to him, when he fled from the face of his brother.
8 Wakati huu Debora, mlezi wa Rebeka, akafa na akazikwa chini ya mti wa mwaloni ulioko chini ya Betheli. Kwa hiyo pakaitwa Alon-Bakuthi.
But Deborah Rebekah’s nurse died, and she was buried beneath Bethel under an oak: and the name of it was called Allonbachuth.
9 Baada ya Yakobo kurudi kutoka Padan-Aramu, Mungu alimtokea tena na kumbariki.
And God appeared to Jacob again, when he came out of Padanaram, and blessed him.
10 Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini hutaitwa tena Yakobo, jina lako utakuwa Israeli.” Kwa hiyo akamwita Israeli.
And God said to him, Your name is Jacob: your name shall not be called any more Jacob, but Israel shall be your name: and he called his name Israel.
11 Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu Mwenyezi, ukazae na kuongezeka. Taifa na jamii ya mataifa itatoka kwako, nao wafalme watatoka viunoni mwako.
And God said to him, I am God Almighty: be fruitful and multiply; a nation and a company of nations shall be of you, and kings shall come out of your loins;
12 Nchi niliyowapa Abrahamu na Isaki nakupa wewe pia, nami nitawapa wazao wako baada yako.”
And the land which I gave Abraham and Isaac, to you I will give it, and to your seed after you will I give the land.
13 Kisha Mungu akapanda juu kutoka kwake mahali pale alipozungumza naye.
And God went up from him in the place where he talked with him.
14 Yakobo akasimamisha nguzo ya jiwe mahali pale Mungu alipozungumza naye, akamimina sadaka ya kinywaji juu yake, pia akamimina mafuta juu yake.
And Jacob set up a pillar in the place where he talked with him, even a pillar of stone: and he poured a drink offering thereon, and he poured oil thereon.
15 Yakobo akapaita mahali pale Mungu alipozungumza naye Betheli.
And Jacob called the name of the place where God spoke with him, Bethel.
16 Kisha wakaondoka Betheli. Walipokuwa umbali fulani kabla ya kufika Efrathi, Raheli akaanza kusikia uchungu na alipata shida kuu.
And they journeyed from Bethel; and there was but a little way to come to Ephrath: and Rachel travailed, and she had hard labor.
17 Alipokuwa katika shida hii katika kujifungua, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwa sababu umempata mwana mwingine.”
And it came to pass, when she was in hard labor, that the midwife said to her, Fear not; you shall have this son also.
18 Hapo alipopumua pumzi yake ya mwisho, kwa maana alikuwa akifa, akamwita mwanawe Benoni. Lakini babaye akamwita Benyamini.
And it came to pass, as her soul was in departing, (for she died) that she called his name Benoni: but his father called him Benjamin.
19 Kwa hiyo Raheli akafa, akazikwa kando ya njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu).
And Rachel died, and was buried in the way to Ephrath, which is Bethlehem.
20 Juu ya kaburi lake, Yakobo akasimamisha nguzo, ambayo mpaka leo inatambulisha kaburi la Raheli.
And Jacob set a pillar on her grave: that is the pillar of Rachel’s grave to this day.
21 Israeli akaendelea tena na safari yake na kupiga hema mbele mnara wa Ederi.
And Israel journeyed, and spread his tent beyond the tower of Edar.
22 Wakati Israeli alipokuwa akiishi katika nchi ile, Reubeni mwanawe alikutana kimwili na suria wa baba yake aitwaye Bilha, naye Israeli akasikia jambo hili. Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili:
And it came to pass, when Israel dwelled in that land, that Reuben went and lay with Bilhah his father’s concubine: and Israel heard it. Now the sons of Jacob were twelve:
23 Wana wa Lea walikuwa: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuloni.
The sons of Leah; Reuben, Jacob’s firstborn, and Simeon, and Levi, and Judah, and Issachar, and Zebulun:
24 Wana wa Raheli walikuwa: Yosefu na Benyamini.
The sons of Rachel; Joseph, and Benjamin:
25 Wana waliozaliwa na Bilha mtumishi wa kike wa Raheli walikuwa: Dani na Naftali.
And the sons of Bilhah, Rachel’s handmaid; Dan, and Naphtali:
26 Wana waliozaliwa na Zilpa mtumishi wa kike wa Lea walikuwa: Gadi na Asheri. Hawa walikuwa wana wa Yakobo, waliozaliwa kwake akiwa Padan-Aramu.
And the sons of Zilpah, Leah’s handmaid: Gad, and Asher: these are the sons of Jacob, which were born to him in Padanaram.
27 Yakobo akarudi nyumbani kwa baba yake Isaki huko Mamre, karibu na Kiriath-Arba (yaani Hebroni), ambapo walikuwa wameishi Abrahamu na Isaki.
And Jacob came to Isaac his father to Mamre, to the city of Arbah, which is Hebron, where Abraham and Isaac sojourned.
28 Isaki aliishi miaka 180.
And the days of Isaac were an hundred and fourscore years.
29 Kisha Isaki akapumua pumzi yake ya mwisho akafa, akakusanywa pamoja na watu wake akiwa mzee wa miaka mingi. Nao wanawe Esau na Yakobo wakamzika.
And Isaac gave up the ghost, and died, and was gathered to his people, being old and full of days: and his sons Esau and Jacob buried him.

< Mwanzo 35 >