< Mwanzo 29 >

1 Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika kwenye nchi za mataifa ya mashariki.
Then Jacob went on his journey, and came to the land of the people of the east.
2 Huko akaona kisima katika shamba, pamoja na makundi matatu ya kondoo yamelala karibu na kisima hicho kwa sababu walikuwa wanakunywa maji kutoka kwenye kisimani hicho. Jiwe lililokuwa mdomoni mwa kisima lilikuwa kubwa.
He looked and saw a well in the field, and look, three flocks of sheep lying there by it. For out of that well they watered the flocks. The stone on the well's mouth was large.
3 Wakati kondoo wanapokuwa wamekusanyika hapo, wachungaji huvingirisha jiwe hilo kutoka kwenye mdomo wa kisima na kunywesha kondoo. Kisha hulirudisha jiwe mahali pake juu ya mdomo wa kisima.
Now all the flocks would be gathered there, and they would roll the stone from the well's mouth, and water the sheep, and put the stone again on the well's mouth in its place.
4 Yakobo aliwauliza wachungaji, “Ndugu zangu, ninyi mmetoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka Harani.”
Jacob said to them, "My brothers, where are you from?" They said, "We are from Haran."
5 Aliwaambia, “Je, mnamjua Labani, mjukuu wa Nahori?” Wakamjibu, “Ndiyo, tunamfahamu.”
He said to them, "Do you know Laban, the grandson of Nahor?" They said, "We know him."
6 Kisha Yakobo akawauliza, “Je, yeye ni mzima?” Wakasema, “Ndiyo, ni mzima, na hapa yuaja Raheli binti yake akiwa na kondoo.”
He said to them, "Is it well with him?" They said, "It is well. See, Rachel, his daughter, is coming with the sheep."
7 Akasema, “Tazama, jua bado liko juu, si wakati wa kukusanya mifugo. Nywesheni kondoo na mwarudishe malishoni.”
He said, "Look, it is still the middle of the day, not time to gather the livestock together. Water the sheep, and go, pasture them."
8 Walijibu, “Haiwezekani, mpaka kondoo wote wakusanyike na jiwe liwe limevingirishwa kutoka mdomo wa kisima. Ndipo tutanywesha kondoo.”
They said, "We can't, until all the flocks are gathered together, and they roll the stone from the well's mouth. Then we water the sheep."
9 Alipokuwa akizungumza nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa baba yake, kwa maana alikuwa mchunga kondoo.
While he was yet speaking with them, Rachel came with her father's sheep, for she was tending them.
10 Yakobo alipomwona Raheli binti Labani, ndugu wa mama yake, pamoja na kondoo wa Labani, alikwenda na kulivingirisha jiwe kutoka mdomoni mwa kisima na kuwanywesha kondoo wa mjomba wake.
It happened, when Jacob saw Rachel the daughter of Laban, his mother's brother, and the sheep of Laban, his mother's brother, that Jacob went over and rolled the stone from the well's mouth and watered the flock of Laban his mother's brother.
11 Kisha Yakobo akambusu Raheli na akaanza kulia kwa sauti.
Jacob kissed Rachel, and wept loudly.
12 Yakobo alikuwa amemwambia Raheli kuwa yeye alikuwa jamaa ya baba yake, na kwamba ni mwana wa Rebeka. Basi Raheli alikimbia na kumweleza baba yake.
Jacob told Rachel that he was her father's brother, and that he was Rebekah's son. She ran and told her father.
13 Mara Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo, mwana wa ndugu yake, aliharakisha kwenda kumlaki. Akamkumbatia na kumbusu, halafu akamleta nyumbani kwake, kisha Yakobo akamwambia mambo yote.
It happened, when Laban heard the news of Jacob, his sister's son, that he ran to meet Jacob, and embraced him, and kissed him, and brought him to his house. Jacob told Laban all these things.
14 Ndipo Labani akamwambia, “Wewe ni nyama yangu na damu yangu mwenyewe.” Baada ya Yakobo kukaa kwa Labani mwezi mzima,
Laban said to him, "Surely you are my bone and my flesh." He lived with him for a month.
15 Labani akamwambia, “Kwa vile wewe ni jamaa yangu, ndiyo sababu unifanyie kazi bila ujira? Niambie ujira wako utakuwa nini.”
Laban said to Jacob, "Because you are my brother, should you therefore serve me for nothing? Tell me what your wages should be?"
16 Labani alikuwa na binti wawili, binti mkubwa aliitwa Lea na binti mdogo aliitwa Raheli.
Laban had two daughters. The name of the older was Leah, and the name of the younger was Rachel.
17 Lea alikuwa na macho dhaifu, lakini Raheli alikuwa na umbo la kupendeza na mzuri wa sura.
Leah looked rather plain, but Rachel was beautiful in form and beautiful in appearance.
18 Yakobo akampenda Raheli, akamwambia Labani, “Nitakutumikia kwa miaka saba kwa ajili ya kumpata Raheli binti yako mdogo.”
Jacob loved Rachel. He said, "I will serve you seven years for Rachel, your younger daughter."
19 Labani akasema, “Ni bora zaidi nikupe Raheli kuliko kumpa mtu mwingine yeyote. Kaa pamoja na mimi hapa.”
Laban said, "It is better that I give her to you, than that I should give her to another man. Stay with me."
20 Kwa hiyo Yakobo akatumika miaka saba ili kumpata Raheli, lakini ilionekana kwake kama siku chache tu kwa sababu ya upendo wake kwa Raheli.
Jacob served seven years for Rachel, and it seemed only a few days to him because of his love for her.
21 Ndipo Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu. Muda wangu umekamilika, nami nataka nikutane naye kimwili.”
Jacob said to Laban, "Give me my wife, for my time is completed, so that I may sleep with her."
22 Basi Labani akaalika watu wote wa mahali pale na akafanya karamu.
Laban gathered together all the people of the place, and gave a feast.
23 Lakini ilipofika jioni, akamchukua Lea binti yake akampa Yakobo, naye Yakobo akakutana naye kimwili.
It happened in the evening, that he took Leah his daughter and brought her to him, and he slept wit her.
24 Naye Labani akamtoa Zilpa, mtumishi wake wa kike, kuwa mtumishi wa Lea, binti yake.
Laban gave Zilpah his female servant to his daughter Leah as a servant.
25 Kesho yake asubuhi, Yakobo akagundua kuwa amepewa Lea! Basi Yakobo akamwambia Labani, “Ni jambo gani hili ulilonitendea? Nilikutumikia kwa ajili ya Raheli, sivyo? Kwa nini umenidanganya?”
It happened in the morning that, look, it was Leah. He said to Laban, "What is this you have done to me? Did I not work for you to have Rachel? Why then have you deceived me?"
26 Labani akajibu, “Si desturi yetu kumwoza binti mdogo kabla ya kumwoza binti mkubwa.
Laban said, "It is not our custom here to give the younger before the firstborn.
27 Maliza juma la arusi ya binti huyu, kisha pia nitakupa huyu binti mdogo, kwa kutumika miaka mingine saba.”
Finish the week of this one, and I will give you the other also in exchange for the work which you are to serve with me for another seven years."
28 Naye Yakobo akafanya hivyo. Akamaliza juma na Lea, kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
Then Jacob did so, and fulfilled her week. He gave him Rachel his daughter as wife.
29 Labani akamtoa Bilha mtumishi wake wa kike kwa Raheli ili kuwa mtumishi wake.
Laban gave to Rachel his daughter Bilhah, his female servant, to be her servant.
30 Pia Yakobo akakutana na Raheli kimwili, naye akampenda Raheli zaidi kuliko Lea. Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka mingine saba.
So he slept with Rachel also, and he loved Rachel more than Leah. And he worked with him another seven years.
31 Bwana alipoona kwamba Lea hapendwi, akampa watoto, lakini Raheli alikuwa tasa.
Jehovah saw that Leah was unloved, so he made her fertile, but Rachel was barren.
32 Lea akapata mimba akazaa mwana. Akamwita Reubeni, kwa maana alisema, “Ni kwa sababu Bwana ameona huzuni yangu. Hakika mume wangu sasa atanipenda.”
Leah conceived, and bore a son, and she named him Reuben. For she said, "Because God has looked at my affliction, and given me a son. For now my husband will love me."
33 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Kwa sababu Bwana alisikia kwamba sipendwi, amenipa tena huyu mwana.” Kwa hiyo akamwita Simeoni.
She conceived again, and bore a son, and said, "Because God has heard that I am unloved, he has therefore given me this son also." So she named him Simeon.
34 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Sasa afadhali mume wangu ataambatana na mimi, kwa sababu nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akamwita Lawi.
She conceived again, and bore a son. She said, "Now this time my husband will become attached to me, since I have given him three sons." Therefore he was named Levi.
35 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Wakati huu nitamsifu Bwana.” Kwa hiyo akamwita Yuda. Kisha akaacha kuzaa watoto.
She conceived again, and bore a son. She said, "This time will I praise Jehovah." Therefore she named him Judah. Then she stopped bearing.

< Mwanzo 29 >