< Mwanzo 14 >

1 Wakati huu Amrafeli mfalme wa Shinari, Arioko mfalme wa Elasari, Kedorlaoma mfalme wa Elamu, na Tidali mfalme wa Goimu
And it came to pass, in the days of Amraphel, king of Shinar, Arioch, king of Ellasar, —Chedorlaomer king of Elam, and Tidal king of Goim,
2 kwa pamoja walikwenda kupigana vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha mfalme wa Gomora, Shinabu mfalme wa Adma, Shemeberi mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari).
that they made war, with Bera, king of Sodom, and with Birsha, king of Gomorrah, —Shinab, king of Admah, and Shemeber, king of Zeboim, and the king of Bela—the same, is Zoar.
3 Hawa wote waliotajwa mwishoni waliunganisha majeshi yao kutoka Bonde la Sidimu (yaani Bahari ya Chumvi).
All these, joined together in the valley of the open fields, the same, is the Salt Sea.
4 Walikuwa wametawaliwa na Mfalme Kedorlaoma kwa miaka kumi na miwili, lakini mwaka wa kumi na tatu waliasi.
Twelve years, had they served Chedorlaomer, —but in the thirteenth year had they rebelled;
5 Mnamo mwaka wa kumi na nne, Mfalme Kedorlaoma na wafalme waliojiunga naye walikwenda kupigana na kuwashinda Warefai katika Ashtaroth-Kanaimu, Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe-Kiriathaimu,
and in the fourteenth year, had Chedorlaomer come in and the kings who were with him, so they smote the Rephaim in Ashteroth-karnaim, and the Zuzim in Ham, —and the Emim, in Shaveh-kiriathaim;
6 na Wahori katika nchi ya kilima cha Seiri, hadi El-Parani karibu na jangwa.
and the Horites in their Mount Seir, —as far as El-paran, which is by the desert.
7 Kisha wakarudi wakaenda En-Misfati (yaani Kadeshi), wakashinda nchi yote ya Waamaleki, pamoja na Waamori waliokuwa wakiishi Hasason-Tamari.
So they returned and came in unto En-mishpat, the same, is Kadish, and smote all the field of the Amalekites, —and the Amorites also that dwelt in Hazazon-tamar,
8 Ndipo mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari) wakatoka kupanga majeshi yao kwenye Bonde la Sidimu
Thus then went forth the King of Sodom and the king of Gomorrah, and the king of Admah and the king of Zeboim, and the king of Bela the same, is Zoar—and set themselves in array against them for battle, in the valley of the open fields:
9 dhidi ya Kedorlaoma, mfalme wa Elamu, Tidali mfalme wa Goimu, Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, yaani wafalme wanne dhidi ya wafalme watano.
against Chedorlaomer king of Elam, and Tidal king of Goim, and Amraphel king of Shinar, and Arioch king of Ellasar, —four kings against five.
10 Basi Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, nao wafalme wa Sodoma na wa Gomora walipokimbia, baadhi ya watu walitumbukia huko na wengine wakakimbilia vilimani.
Now, the valley of the open fields, had many pits of bitumen, so the king of Sodom and Gomorrah fled, and fell there, —while, they who remained, towards a mountain, fled.
11 Wale wafalme wanne wakateka mali yote ya Sodoma na Gomora pamoja na vyakula vyao vyote, kisha wakaenda zao.
And they took all the goods of Sodom and Gomorrah and all their food and went their way.
12 Pia walimteka Loti mwana wa ndugu yake Abramu pamoja na mali zake, kwa kuwa alikuwa akiishi Sodoma.
And they took Lot, Abram’s brother’s son with his goods, and went their way, —he, being a dweller in Sodom.
13 Mtu mmoja aliyekuwa ametoroka akaja kumpa Abramu Mwebrania taarifa. Wakati huu Abramu alikuwa anaishi karibu na mialoni ya Mamre Mwamori, aliyekuwa ndugu yake Eshkoli na Aneri, ambao wote walikuwa wameungana na Abramu.
Then came in a fugitive, and told Abram the Hebrew, —he, having his dwelling among the oaks of Mamre the Amorite brother of Eshcol and brother of Aner, they, also having a covenant with Abram.
14 Abramu alipopata habari kwamba jamaa yake amechukuliwa mateka, akawaita watu 318 wa nyumbani mwake waliokuwa wamefunzwa kupigana vita, wakawafuatilia hadi Dani.
So Abram, hearing that his brother had been taken captive, drew forth his trained men born in his house three hundred and eighteen, and pursued as far as Dan.
15 Wakati wa usiku Abramu aliwagawa watu wake katika vikosi ili awashambulie, na akawafuatilia, akawafukuza hadi Hoba, kaskazini ya Dameski.
And he divided himself against them by night, he, and his servants, and smote them, —and pursued them as far as Hobah, which was on the left of Damascus.
16 Akarudisha mali zote, na akamrudisha Loti jamaa yake na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.
So he brought back all the goods, —yea Lot also his brother with his goods, did he bring back, and the women also, and the people.
17 Abramu aliporudi baada ya kumshinda Mfalme Kedorlaoma na wale wafalme waliojiunga naye, mfalme wa Sodoma akatoka kwenda kumlaki katika Bonde la Shawe (yaani Bonde la Mfalme).
Then came forth the king of Sodom to meet him, after his return from the smiting of Chedorlaomer, and the kings who were with him, —into the vale of Shaveh the same, was the vale of the king.
18 Ndipo Melkizedeki mfalme wa Salemu alipoleta mkate na divai. Alikuwa kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana.
Now Melchizedek king of Salem, had brought forth bread and wine, —he, being priest of GOD Most High.
19 Naye akambariki Abramu, akisema, “Abarikiwe Abramu na Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na nchi.
So he blessed him and said, —Blessed be Abram of GOD Most High, possessor of [the] heavens and earth;
20 Abarikiwe Mungu Aliye Juu Sana, ambaye amewaweka adui zako mkononi mwako.” Ndipo Abramu akampa Melkizedeki sehemu ya kumi ya kila kitu.
And blessed be GOD Most High, who hath delivered thine enemies into thy hand. So he gave unto him a tenth of all.
21 Mfalme wa Sodoma akamwambia Abramu, “Nipe hao watu na hizo mali uchukue wewe mwenyewe.”
Then said the king of Sodom unto Abram, —Give unto me the persons, but the goods, take thou for thyself.
22 Lakini Abramu akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua mkono wangu kwa Bwana, Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na dunia, na nimeapa
And Abram said unto the king of Sodom, —I have lifted up my hand unto Yahweh GOD Most High, possessor of [the] heavens and earth:
23 kwamba sitapokea kitu chochote kilicho chako, hata kama ni uzi au gidamu ya kiatu, ili kamwe usije ukasema, ‘Nimemtajirisha Abramu.’
That not from a thread even unto a sandal-thong, —will I take, anything, that is thine, —Lest thou shouldst say, I, enriched Abram!
24 Sitapokea chochote, ila kile tu watu wangu walichokula na sehemu ambayo ni fungu la watu waliokwenda pamoja nami, ambao ni Aneri, Eshkoli na Mamre. Wao na wapewe fungu lao.”
Save only what the young men have eaten, and the share of the men who went with me, Aner, Eshcol, and Mamre, they may take their share.

< Mwanzo 14 >