< Mwanzo 11 >

1 Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
The whole earth was of one language and of one speech.
2 Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
As they travelled east, they found a plain in the land of Shinar, and they lived there.
3 Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
They said to one another, “Come, let’s make bricks, and burn them thoroughly.” They had brick for stone, and they used tar for mortar.
4 Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
They said, “Come, let’s build ourselves a city, and a tower whose top reaches to the sky, and let’s make a name for ourselves, lest we be scattered abroad on the surface of the whole earth.”
5 Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
The LORD came down to see the city and the tower, which the children of men built.
6 Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
The LORD said, “Behold, they are one people, and they all have one language, and this is what they begin to do. Now nothing will be withheld from them, which they intend to do.
7 Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
Come, let’s go down, and there confuse their language, that they may not understand one another’s speech.”
8 Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
So the LORD scattered them abroad from there on the surface of all the earth. They stopped building the city.
9 Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
Therefore its name was called Babel, because there the LORD confused the language of all the earth. From there, the LORD scattered them abroad on the surface of all the earth.
10 Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
This is the history of the generations of Shem: Shem was one hundred years old when he became the father of Arpachshad two years after the flood.
11 Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Shem lived five hundred years after he became the father of Arpachshad, and became the father of more sons and daughters.
12 Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
Arpachshad lived thirty-five years and became the father of Shelah.
13 Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Arpachshad lived four hundred and three years after he became the father of Shelah, and became the father of more sons and daughters.
14 Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
Shelah lived thirty years, and became the father of Eber.
15 Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Shelah lived four hundred and three years after he became the father of Eber, and became the father of more sons and daughters.
16 Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
Eber lived thirty-four years, and became the father of Peleg.
17 Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Eber lived four hundred and thirty years after he became the father of Peleg, and became the father of more sons and daughters.
18 Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
Peleg lived thirty years, and became the father of Reu.
19 Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Peleg lived two hundred and nine years after he became the father of Reu, and became the father of more sons and daughters.
20 Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
Reu lived thirty-two years, and became the father of Serug.
21 Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Reu lived two hundred and seven years after he became the father of Serug, and became the father of more sons and daughters.
22 Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
Serug lived thirty years, and became the father of Nahor.
23 Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Serug lived two hundred years after he became the father of Nahor, and became the father of more sons and daughters.
24 Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
Nahor lived twenty-nine years, and became the father of Terah.
25 Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Nahor lived one hundred and nineteen years after he became the father of Terah, and became the father of more sons and daughters.
26 Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
Terah lived seventy years, and became the father of Abram, Nahor, and Haran.
27 Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
Now this is the history of the generations of Terah. Terah became the father of Abram, Nahor, and Haran. Haran became the father of Lot.
28 Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
Haran died in the land of his birth, in Ur-Kasdim, while his father Terah was still alive.
29 Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
Abram and Nahor married wives. The name of Abram’s wife was Sarai, and the name of Nahor’s wife was Milcah, the daughter of Haran, who was also the father of Iscah.
30 Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
Sarai was barren. She had no child.
31 Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
Terah took Abram his son, Lot the son of Haran, his son’s son, and Sarai his daughter-in-law, his son Abram’s wife. They went from Ur-Kasdim, to go into the land of Canaan. They came to Haran and lived there.
32 Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.
The days of Terah were two hundred and five years. Terah died in Haran.

< Mwanzo 11 >