< Mwanzo 10 >

1 Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
Now these are the generations of the sons of Noah and of Shem, Ham, and Japheth. Sons were born to them after the flood.
2 Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
The sons of Japheth: Gomer, Magog, Madai, Javan, Tubal, Meshech, and Tiras.
3 Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
The sons of Gomer: Ashkenaz, Riphath, and Togarmah.
4 Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
The sons of Javan: Elishah, Tarshish, Kittim, and Rodanim.
5 (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
From these, the coastlands of the nations separated into their territories, every one according to its language, according to their families, in their nations.
6 Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
The sons of Ham: Cush, Mizraim, Put, and Canaan.
7 Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
The sons of Cush: Seba, Havilah, Sabtah, Raamah, and Sabteca. The sons of Raamah: Sheba and Dedan.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
Cush became the father of Nimrod. He began to be a mighty one on the earth.
9 Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
He was a mighty hunter before God. Therefore it is said, "Like Nimrod, a mighty hunter before God."
10 Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
And the beginning of his kingdom was Babel, and Erech, and Akkad, and Calneh, in the land of Shinar.
11 Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
Out of that land he went forth into Assyria, and built Nineveh, and Rehoboth Ir, and Calah,
12 na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
and Resen, between Nineveh and the great city of Calah.
13 Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
And Mizraim became the father of Ludim, and Anamim, and Lehabim, and Naphtuhim,
14 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
And Pathrusim, and Casluhim, which the Philistines descended from, and Caphtorim.
15 Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
And Canaan became the father of Sidon, his firstborn, and Heth,
16 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
and the Jebusites, and the Amorites, and the Girgashites,
17 Wahivi, Waariki, Wasini,
and the Hivites, and the Arkites, and the Sinites,
18 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
and the Arvadites, and the Zemarites, and the Hamathites. Afterward the families of the Canaanites were spread abroad.
19 na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
And the border of the Canaanites was from Sidon, as you go toward Gerar, to Gaza; as you go toward Sodom, and Gomorrah, and Admah, and Zeboiim, to Lasha.
20 Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
These are the sons of Ham, after their families, after their languages, in their lands, in their nations.
21 Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
To Shem, the father of all the children of Eber, the elder brother of Japheth, to him also were children born.
22 Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
The sons of Shem: Elam, and Asshur, and Arpachshad, and Lud, and Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
The sons of Aram: Uz, and Hul, and Gether, and Mash.
24 Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
And Arpachshad became the father of Kenan. And Kenan became the father of Shelah. And Shelah became the father of Eber.
25 Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
To Eber were born two sons. The name of the one was Peleg, for in his days the earth was divided. His brother's name was Joktan.
26 Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
And Joktan became the father of Almodad, and Sheleph, and Hazarmaveth, and Jerah,
27 Hadoramu, Uzali, Dikla,
and Hadoram, and Uzal, and Diklah,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
and Obal, and Abimael, and Sheba,
29 Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
and Ophir, and Havilah, and Jobab. All these were the sons of Joktan.
30 Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
Their dwelling was from Mesha, as you go toward Sephar, the mountain of the east.
31 Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
These are the sons of Shem, after their families, after their languages, in their lands, after their nations.
32 Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.
These are the families of the sons of Noah, after their generations, in their nations, and from these the nations branched out on the earth after the flood.

< Mwanzo 10 >