< Ezra 7 >

1 Baada ya mambo haya, wakati wa utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Ezra mwana wa Seraya, mwana wa Azaria, mwana wa Hilkia,
Mutta näiden jälkeen Artahsastan Persian kuninkaan hallitessa oli Esra Serajan poika, Asarian pojan, Hilkian pojan,
2 mwana wa Shalumu, mwana wa Sadoki, mwana wa Ahitubu,
Sallumin pojan, Zadokin pojan, Ahitobin pojan,
3 mwana wa Amaria, mwana wa Azaria, mwana wa Merayothi,
Amarian pojan, Asarian pojan, Merajotin pojan,
4 mwana wa Zerahia, mwana wa Uzi, mwana wa Buki,
Serahian pojan, Ussin pojan, Bukkin pojan,
5 mwana wa Abishua, mwana wa Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani mkuu Aroni.
Abisuan pojan, Pinehaan pojan, Eleatsarin pojan, ylimmäisen papin Aaronin pojan.
6 Huyu Ezra alipanda kutoka Babeli. Alikuwa mwalimu mwenye ujuzi mzuri katika sheria ya Mose, ambayo Bwana, Mungu wa Israeli, alikuwa ametoa. Mfalme alikuwa amempa Ezra kila kitu alichoomba, kwa maana Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
Tämä Esra meni ylös Babelista, joka oli toimellinen kirjanoppinut Moseksen laissa, jonka Herra Israelin Jumala oli antanut. Ja kuningas antoi hänelle kaikki, mitä hän anoi, Herran hänen Jumalansa käden jälkeen, joka hänen ylitsensä oli.
7 Pia baadhi ya Waisraeli, wakiwemo makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu na watumishi wa Hekalu, nao walikuja Yerusalemu mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
Ja siinä meni muutamia Israelin lapsista ja papeista ja Leviläisistä, veisaajista, ovenvartioista ja Netinimeistä ylös Jerusalemiin, seitsemäntenä Artahsastan kuninkaan vuonna.
8 Ezra aliwasili Yerusalemu mwezi wa tano wa mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
Ja hän tuli Jerusalemiin viidentenä kuukautena, se oli seitsemäs kuninkaan vuosi.
9 Ezra alianza safari yake kutoka Babeli tangu siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, naye akawasili Yerusalemu siku ya kwanza ya mwezi wa tano, kwa maana mkono wa neema wa Mungu wake ulikuwa juu yake.
Sillä ensimäisenä päivänä ensimäistä kuuta alkoi hän lähteä Babelista, ja ensimäisenä päivänä viidennettä kuuta tuli hän Jerusalemiin, Jumalan hyvän käden kautta, joka hänen ylitsensä oli.
10 Kwa maana Ezra alikuwa amejitoa kwa moyo wote kujifunza na kushika sheria ya Bwana na kuwafundisha watu wa Israeli amri na sheria zake.
Sillä Esra oli valmistanut sydämensä etsimään Herran lakia, ja tekemään sitä ja opettamaan Israelille säätyjä ja oikeutta.
11 Hii ni nakala ya barua ambayo Mfalme Artashasta alikuwa amempa Ezra aliyekuwa kuhani na mwalimu, mtu aliyeelimika katika mambo yahusuyo maagizo na amri za Bwana kwa Israeli.
Ja näin on se kirja, jonka Artahsasta antoi papille Esralle, kirjanoppineelle, joka oli opettaja Herran käskysanoissa ja säädyissä Israelille:
12 Artashasta, mfalme wa wafalme, Kwa Ezra kuhani, mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni: Salamu.
Artahsasta kuningasten kuningas Esralle papille ja kirjanoppineelle taivaan Jumalan laissa: rauhaa tällä ajalla!
13 Sasa naamuru kwamba mtu yeyote Mwisraeli katika ufalme wangu, pamoja na makuhani na Walawi, ambaye anataka kwenda Yerusalemu pamoja nawe aweza kwenda.
Minä olen käskenyt, että kenenkä ikänä kelpaa minun valtakunnassani Israelin kansasta, papeista ja Leviläisistä mennä kanssas Jerusalemiin, niin menkään.
14 Unatumwa na mfalme na washauri wake saba kuchunguza kuhusu Yuda na Yerusalemu kulingana na Sheria ya Mungu wako, iliyoko mkononi mwako.
Sinä olet lähetetty kuninkaalta ja seitsemältä neuvonantajalta etsimään Juudaa ja Jerusalemia, sinun Jumalas lain jälkeen, joka käsissäs on;
15 Zaidi ya hayo, uchukue pamoja nawe fedha na dhahabu ambazo mfalme na washauri wake wamempa Mungu wa Israeli kwa hiari, Mungu ambaye maskani yake yako Yerusalemu,
Ja ettäs otat myötäs sen hopian ja kullan, minkä kuningas ja hänen neuvonantajansa hyvällä mielellä ovat uhranneet Israelin Jumalalle, jonka maja on Jerusalemissa.
16 pia fedha na dhahabu zote unazoweza kupata kutoka jimbo la Babeli, pamoja na sadaka za hiari watakazotoa watu na makuhani kwa ajili ya Hekalu la Mungu wao katika Yerusalemu.
Ja kaikkinaisen hopian ja kullan, minkä sinä saat koko Babelin maakunnasta, kuin kansa ja papit hyvällä mielellä antavat Jumalan huoneesen, joka on Jerusalemissa.
17 Hakikisha kwamba fedha hizi zimetumika kununua mafahali, kondoo dume na wana-kondoo pamoja na sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji, uvitoe dhabihu juu ya madhabahu ya Hekalu la Mungu wenu katika Yerusalemu.
Sentähden osta nopiasti sillä rahalla mullia, oinaita ja karitsoita, ja ruokauhria ja juomauhria, ja uhraa ne teidän Jumalanne huoneen alttarilla, joka on Jerusalemissa.
18 Kisha wewe na Wayahudi ndugu zako mnaweza kufanya lolote linaloonekana jema sana kwa fedha na dhahabu zilizosalia, kulingana na mapenzi ya Mungu wenu.
Mutta mitä sinun ja sinun veljes siitä rahasta kelpaa tehdä, joka liiaksi on, se tehkäät teidän Jumalanne tahdon jälkeen.
19 Uvitoe kwa Mungu wa Yerusalemu vyombo vyote ulivyokabidhiwa kwa ajili ya ibada katika Hekalu la Mungu wako.
Ja astiat, jotka sinun haltuus ovat annetut sinun Jumalas huoneen palvelukseksi, anna ne pois Jumalan eteen Jerusalemiin.
20 Kitu kingine chochote kinachohitajika kwa ajili ya Hekalu la Mungu wenu ambacho unatakiwa kukitoa, waweza kukitoa kutoka hazina ya mfalme.
Ja mitä enempää tarvitaan sinun Jumalas huoneesen ja sinä kulutat, niin anna se kuninkaan tavarahuoneesta.
21 Mimi, Mfalme Artashasta, sasa naagiza watunza hazina wote wa Ngʼambo ya Mto Frati kutoa kwa bidii chochote kwa Ezra kuhani na mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni atakachohitaji kwenu,
Minä kuningas Artahsasta olen käskenyt veronhaltioille sillä puolella virtaa, että mitä ikänä Esra pappi ja kirjanoppinut taivaan Jumalan laissa teiltä anoo, se tehkäät nopiasti,
22 talanta 100 za fedha, ngano kori 100, divai bathi 100, mafuta ya zeituni bathi 100, na chumvi kiasi chochote.
Hamaan sataan leiviskään hopiaa, ja sataan koriin nisuja, ja sataan tynnyriin viinaa, ja sataan tynnyriin öljyä, ja suoloja ilman mittaa.
23 Chochote ambacho Mungu wa mbinguni ameagiza, kifanyike kwa ukamilifu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wa mbinguni. Kwa nini pawepo ghadhabu dhidi ya utawala wa mfalme na wanawe?
Kaikkia mitä taivaan Jumalan laki anoo, se pitää taivaan Jumalan huoneelle juuri nopiasti tehtämän, ettei hänen vihansa tulisi kuninkaan valtakunnan ja hänen lastensa päälle.
24 Pia ninyi fahamuni kuwa hamna mamlaka ya kuwatoza kodi, ushuru au ada makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, watumishi wa Hekalu au wafanyakazi wengine kwenye nyumba ya Mungu.
Ja se pitää oleman teille kaikille tiettävä, ettei teillä ole valtaa panna jotakin veroa, tullia eli ajastaikaista ulostekoa yhdenkään papin päälle, Leviläisen, veisaajan, ovenvartijan, Netinimin, tämän Jumalan huoneen palveliain päälle,
25 Nawe Ezra, kufuatana na hekima ya Mungu wenu uliyo nayo, weka mahakimu na waamuzi wote wanaozifahamu sheria za Mungu wenu ili watoe haki kwa watu wote wa Ngʼambo ya Mto Frati. Nawe inakupasa umfundishe yeyote ambaye hazifahamu.
Ja sinun, Esra, pitää Jumalas viisauden jälkeen, joka sinulla on, paneman tuomarit ja oikeuden tekiät, tuomitsemaan kaiken kansan, joka toisella puolella virtaa on, että kaikki taitaisivat sinun Jumalas lain; ja sitä, joka ei taida, pitää teidän opettaman.
26 Yeyote ambaye hataitii sheria ya Mungu wenu pia sheria ya mfalme, hakika lazima aadhibiwe kwa kuuawa, kuhamishwa, kunyangʼanywa mali au kufungwa gerezani.
Ja jokainen, joka ei tee visusti sinun Jumalas lakia ja kuninkaan lakia, hänen pitää saaman tuomionsa työnsä jälkeen, joko se on kuolemaan, eli maan kulkemukseen, eli rahasakkoon, taikka vankeuteen.
27 Sifa ziwe kwa Bwana, Mungu wa baba zetu, Mungu ambaye kwa njia hii ameweka ndani ya moyo wa mfalme kuipa heshima nyumba ya Bwana iliyoko Yerusalemu, kwa namna hii
Kiitetty olkoon Herra, meidän isäimme Jumala, joka tainkaltaisen asian on antanut kuninkaan sydämeen, että hän kaunistaa Herran huonetta Jerusalemissa!
28 ambaye ameniongezea kibali chake mbele ya mfalme, washauri wake na maafisa wote wa mfalme wenye uwezo. Kwa kuwa mkono wa Bwana Mungu wangu ulikuwa pamoja nami, nilijipa moyo nikakusanya watu walio viongozi kutoka Israeli wakwee pamoja nami.
Ja hän on kääntänyt laupiuden minun päälleni kuninkaan ja hänen neuvonantajainsa ja kaikkein kuninkaan voimallisten päämiesten edessä. Ja minä vahvistettiin Herran minun Jumalani kädellä, joka oli minun ylitseni, ja kokosin päämiehet Israelista menemään ylös minun kanssani.

< Ezra 7 >