< Ezra 3 >

1 Mwezi wa saba ulipowadia baada ya Waisraeli kukaa katika miji yao, watu wote walikusanyika huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
Le septième mois approchant, et les enfants d'Israël étant dans leurs villes, le peuple s'assembla à Jérusalem, comme un seul homme.
2 Yeshua mwana wa Yosadaki na makuhani wenzake, Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na wenzake walianza kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli ili kumtolea dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake, kulingana na ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu.
Alors Jéshua, fils de Jotsadak, se leva avec ses frères les sacrificateurs, et Zorobabel, fils de Salathiel, avec ses frères; et ils bâtirent l'autel du Dieu d'Israël, pour y offrir les holocaustes ainsi qu'il est écrit dans la loi de Moïse, homme de Dieu.
3 Ingawa waliwaogopa watu waliowazunguka, walijenga madhabahu juu ya ule msingi wake, wakamtolea Bwana dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake za asubuhi na za jioni.
Et ils redressèrent l'autel sur ses fondements, car ils étaient sous la crainte des populations du pays; et ils y offrirent des holocaustes à l'Éternel, les holocaustes du matin et du soir.
4 Kisha kulingana na kile kilichoandikwa, wakaiadhimisha Sikukuu ya Vibanda wakitoa idadi ya sadaka za kuteketezwa kama ilivyohitajika kila siku sawasawa na ilivyoagizwa.
Ils célébrèrent ensuite la fête des tabernacles, ainsi qu'il est écrit, et ils offrirent des holocaustes chaque jour, autant qu'il en fallait selon que l'ordinaire de chaque jour le demandait.
5 Baada ya hayo, walitoa sadaka za kuteketezwa za kawaida, sadaka za Mwezi Mwandamo na dhabihu zote za sikukuu takatifu za Bwana zilizoamriwa, pamoja na zile sadaka za hiari zilizotolewa kwa Bwana.
Après cela, ils offrirent l'holocauste continuel, ceux des nouvelles lunes et de toutes les solennités consacrées à l'Éternel, et ceux que chacun présentait volontairement à l'Éternel.
6 Ingawa bado msingi wa Hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.
Dès le premier jour du septième mois, ils commencèrent à offrir des holocaustes à l'Éternel, bien que le temple de l'Éternel ne fût pas encore fondé.
7 Kisha watu wakawapa mafundi wa uashi na useremala fedha, wakawapa watu wa Sidoni na Tiro vyakula, vinywaji na mafuta ili waweze kuleta magogo ya mierezi kwa njia ya bahari kutoka Lebanoni hadi Yafa, kama alivyoagiza Koreshi mfalme wa Uajemi.
Mais ils donnèrent de l'argent aux tailleurs de pierres et aux charpentiers; ils donnèrent aussi à manger et à boire, ainsi que de l'huile, aux Sidoniens et aux Tyriens, afin qu'ils amenassent du bois de cèdre, du Liban à la mer de Japho, selon la permission que Cyrus, roi de Perse, leur en avait donnée.
8 Katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kufika kwenye nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zao wengine (makuhani, Walawi na wote waliorejea Yerusalemu kutoka uhamishoni) walianza kazi, wakiteua Walawi wenye umri kuanzia miaka ishirini au zaidi kusimamia ujenzi wa nyumba ya Bwana.
Et la seconde année depuis leur arrivée à la maison de Dieu, à Jérusalem, au second mois, Zorobabel, fils de Salathiel, Jéshua, fils de Jotsadak, et le reste de leurs frères, les sacrificateurs, et les Lévites, et tous ceux qui étaient venus de la captivité à Jérusalem, commencèrent; et ils établirent des Lévites, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, pour présider à l'ouvrage de la maison de l'Éternel.
9 Yeshua na wanawe, pamoja na ndugu zake, Kadmieli na wanawe (wazao wa Hodavia), wana wa Henadadi na wana wao na ndugu zao, Walawi wote walijiunga pamoja kusimamia wale waliofanya kazi katika nyumba ya Mungu.
Et Jéshua assistait avec ses fils et ses frères, et Kadmiel avec ses fils, enfants de Juda, comme un seul homme, pour diriger ceux qui faisaient l'ouvrage de la maison de Dieu, ainsi que les fils de Hénadad, avec leurs fils et leurs frères, Lévites.
10 Wajenzi walipoweka msingi wa Hekalu la Bwana, makuhani wakiwa wamevalia mavazi yao wakiwa na tarumbeta na Walawi (wana wa Asafu) wakiwa na matoazi, walishika nafasi zao za kumtukuza Bwana, kama ilivyoagizwa na Daudi mfalme wa Israeli.
Or, lorsque ceux qui bâtissaient jetèrent les fondements du temple de l'Éternel, on y fit assister les sacrificateurs en costume, avec les trompettes, et les Lévites, fils d'Asaph, avec les cymbales, pour louer l'Éternel, selon l'institution de David, roi d'Israël.
11 Waliimba nyimbo za sifa na za shukrani kwa Bwana hivi: “Yeye ni mwema; upendo wake kwa Israeli wadumu milele.” Watu wote wakapaza sauti kubwa za sifa kwa Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana ulikuwa umewekwa.
Et en louant et en célébrant l'Éternel, ils s'entre-répondaient ainsi: Car il est bon, car sa miséricorde demeure à toujours sur Israël! Et tout le peuple jetait de grands cris de joie, en louant l'Éternel, parce qu'on posait les fondements de la maison de l'Éternel.
12 Lakini wengi wa makuhani wazee, Walawi na viongozi wa jamaa waliokuwa wameona Hekalu la mwanzoni, walilia kwa sauti walipoona msingi wa Hekalu hili ukiwekwa, huku wengine wengi wakipiga kelele kwa furaha.
Mais plusieurs des sacrificateurs, et des Lévites, et des chefs des pères, qui étaient âgés, et qui avaient vu la première maison sur son fondement, en se représentant cette maison-ci, pleuraient à haute voix; tandis que beaucoup d'autres élevaient leurs voix avec des cris de réjouissance et avec joie.
13 Hakuna mtu ambaye angeweza kutofautisha sauti hizo za furaha na za kilio, kwa sababu watu walipiga kelele sana. Nayo hiyo sauti ikasikika mbali.
Et l'on ne pouvait discerner la voix des cris de joie d'avec la voix des pleurs du peuple; car le peuple jetait de grands cris, de sorte que leur voix fut entendue bien loin.

< Ezra 3 >