< Ezekieli 5 >

1 “Mwanadamu, sasa chukua upanga mkali na uutumie kama wembe wa kinyozi ili kunyolea nywele za kichwa chako na ndevu zako. Kisha uchukue mizani ya kupimia ukazigawanye nywele hizo.
And thou, sone of man, take to thee a scharp swerd, schauynge heeris; and thou schalt take it, and schalt leede it bi thin heed, and bi thi berd. And thou schalt take to thee a balaunce of weiyte, and thou schalt departe tho.
2 Wakati siku zako za kuzingirwa zitakapokwisha, choma theluthi moja ya hizo nywele zako kwa moto ndani ya mji. Chukua theluthi nyingine ya hizo nywele uzipige kwa upanga kuuzunguka mji wote na theluthi nyingine ya mwisho utaitawanya kwa upepo. Kwa kuwa nitawafuatia kwa upanga uliofutwa.
Thou schalt brenne the thridde part with fier in the myddis of the citee, bi the fillyng of daies of bisegyng. And thou schalt take the thridde part, and schalt kitte bi swerd in the cumpas therof. But thou schalt scatere `the tother thridde part in to the wynd; and Y schal make nakid a swerd aftir hem.
3 Lakini chukua nywele chache uzifungie ndani ya pindo la vazi lako.
And thou schalt take therof a litil noumbre, and thou schalt bynde tho in the hiynesse of thi mentil.
4 Tena chukua nywele nyingine chache uzitupe motoni uziteketeze. Moto utaenea kutoka humo na kufika katika nyumba yote ya Israeli.
And eft thou schalt take of hem, and thou schalt caste forth hem in to the myddis of the fier. And thou schalt brenne hem in fier; and fier schal go out of that in to al the hous of Israel.
5 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Huu ndio Yerusalemu ambao nimeuweka katikati ya mataifa ukiwa umezungukwa na nchi pande zote.
The Lord God seith these thingis, This is Jerusalem; Y haue sette it in the myddis of hethene men, and londis in the cumpas therof.
6 Lakini katika uovu wake umeasi sheria na amri zangu kuliko mataifa na nchi zinazouzunguka. Umeasi sheria zangu wala haukufuata amri zangu.
And it dispiside my domes, that it was more wickid than hethene men; and it dispiside my comaundementis more than londis that ben in the cumpas therof. For thei han cast awei my domes, and thei yeden not in my comaundementis.
7 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninyi mmekuwa wakaidi kuliko mataifa yanayowazunguka na hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu. Wala hamkuweza hata kuzifuata kawaida za mataifa yanayowazunguka.
Therfor the Lord God seith these thingis, For ye `han passid hethene men that ben in youre cumpas, and ye yeden not in my comaundementis, and ye diden not my domes, and ye wrouyten not bi the domes of hethene men that ben in youre cumpas;
8 “Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo, Mimi mwenyewe, niko kinyume nanyi Yerusalemu, nitawapiga kwa adhabu yangu mbele ya mataifa.
therfor the Lord God seith these thingis, Lo! Y to thee, and Y my silf schal make domes in the myddis of thee, bifor the iyen of hethene men; and Y schal do thingis in thee,
9 Kwa ajili ya sanamu zenu zote za machukizo, nitawafanyia kile ambacho kamwe sijawafanyia kabla wala kamwe sitawafanyia tena.
whiche Y dide not, and to whiche Y schal no more make lijk thingis, for alle thin abhomynaciouns.
10 Kwa hiyo katikati yenu baba watakula watoto wao na watoto watakula baba zao. Nitawapiga kwa adhabu, nami nitawatawanya watu wenu walionusurika pande zote za dunia.
Therfor fadris schulen ete sones in the myddis of thee, and sones schulen ete her fadris; and Y schal make domes in thee, and Y schal wyndewe alle thin remenauntis in to ech wynd.
11 Kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa kuwa mmenajisi mahali pangu patakatifu kwa sanamu zenu mbaya sana na desturi zenu za machukizo, mimi mwenyewe nitaondoa fadhili zangu kwenu.
Therfor Y lyue, seith the Lord God, no but for that that thou defoulidist myn hooli thing in alle thin offenciouns, and in alle thin abhomynaciouns; and Y schal breke, and myn iye schal not spare, and Y schal not do merci.
12 Theluthi ya watu wako watakufa kwa tauni au kwa njaa humu ndani yako, theluthi nyingine itaanguka kwa upanga nje ya kuta zako, nayo theluthi nyingine nitaitawanya kwenye pande nne kuwafuatia kwa upanga uliofutwa.
The thridde part of thee schal die bi pestilence, and schal be wastid bi hungur in the middis of thee; and the thridde part of thee schal falle doun bi swerd in thi cumpas; forsothe Y schal scatere thi thridde part in to ech wynd, and Y schal drawe out a swerd after hem.
13 “Ndipo hasira yangu itakapokoma na ghadhabu yangu dhidi yao itatulia, nami nitakuwa nimelipiza kisasi. Baada ya kuimaliza ghadhabu yangu juu yao, watajua kuwa mimi Bwana nimenena katika wivu wangu.
And Y schal fille my stronge veniaunce, and Y schal make myn indignacioun to reste in hem, and Y schal be coumfortid. And thei schulen wite, that Y the Lord spak in my feruent loue, whanne Y schal fille al myn indignacioun in hem.
14 “Nitakuangamiza na kukufanya kitu cha kudharauliwa miongoni mwa mataifa yanayokuzunguka, machoni pa watu wote wapitao karibu nawe.
And Y schal yyue thee in to desert, in to schenschipe to hethene men that ben in thi cumpas, in the siyt of ech that passith forth.
15 Utakuwa kitu cha kudharauliwa na cha aibu, cha dhihaka, ovyo na kitu cha kutisha kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapokupiga kwa adhabu yangu katika hasira na ghadhabu yangu kwa kukukemea kwa ukali. Mimi Bwana nimesema.
And thou schalt be schenschipe `and blasfemye, ensaumple and wondryng, among hethene men that ben in thi cumpas, whanne Y schal make domes in thee, in strong veniaunce, and indignacioun, and in blamyngis of ire.
16 Nitakapokupiga kwa mishale yangu ya kufisha na yenye kuharibu ya njaa, nitaipiga ili kukuangamiza. Nitaleta njaa zaidi na zaidi juu yako na kukomesha upatikanaji wa chakula kwako.
Y the Lord haue spoke, whanne Y schal sende in to hem the worste arowis of hungur, that schulen bere deth; and whiche Y schal sende, that Y leese you. And Y schal gadere hungur on you, and Y schal al to-breke in you the sadnesse of breed.
17 Nitapeleka njaa na wanyama wa mwituni dhidi yenu, navyo vitawaacha bila watoto. Tauni na umwagaji wa damu utapita katikati yenu, nami nitaleta upanga juu yenu. Mimi Bwana nimenena haya.”
And Y schal sende in to you hungur, and worste beestis, til to the deth; and pestilence and blood schulen passe bi thee, and Y schal bringe in swerd on thee; Y the Lord spak.

< Ezekieli 5 >