< Ezekieli 47 >

1 Yule mtu akanirudisha mpaka kwenye ingilio la Hekalu, nami nikaona maji yakitoka chini ya kizingiti cha Hekalu yakitiririkia upande wa mashariki (kwa maana upande wa mbele wa Hekalu ulielekea mashariki). Maji yalikuwa yakitoka chini upande wa kusini wa Hekalu, kusini mwa madhabahu.
Then the man took me back to the entrance to the temple, and there was water flowing out from under the temple threshold of the house toward the east—for the front of the temple faced east—and the water was flowing down the south side of the temple, to the right of the altar.
2 Ndipo akanitoa nje kupitia lango la kaskazini na kunizungusha mpaka kwenye lango la nje linaloelekea mashariki, nayo maji yalikuwa yakitiririka kutoka upande wa kusini.
So he brought me out through the northern gate and led around to the gate facing east, and there the water was flowing from this gate on its south side.
3 Mtu yule alipokwenda upande wa mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake, akapima dhiraa 1,000 kisha akanipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kwenye vifundo vya miguu.
As the man was going toward the east, there was a measuring line in his hand; he measured off one thousand cubits and brought me through the water to ankle-deep water.
4 Akapima dhiraa 1,000 nyingine na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika magotini. Akapima dhiraa nyingine 1,000 na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kiunoni.
Then he measured one thousand cubits again and brought me through the water to knee-deep water; and he measured another thousand cubits and brought me to hip-deep water.
5 Akapima tena dhiraa 1,000 nyingine, lakini wakati huu yalikuwa mto ambao sikuweza kuvuka, kwa kuwa maji yalikuwa na kina kirefu ambacho ni cha kuogelea, mto ambao hakuna mtu yeyote ambaye angeweza kuvuka.
Next he measured off another thousand cubits, but it was a river that I could not cross through because the water had risen and was deep enough to swim in—it was a river that could not be crossed.
6 Akaniuliza, “Je, mwanadamu, unaona hili?” Kisha akanirudisha mpaka kwenye ukingo wa huo mto.
The man said to me, “Son of man, do you see this?” and he brought me out and had me walk back along the riverbank.
7 Nilipofika pale, nikaona idadi kubwa ya miti kila upande wa ule mto.
As I walked back, there the riverbank had many trees on this side and also the other side.
8 Akaniambia, “Haya maji yanatiririka kuelekea nchi ya mashariki na kushuka mpaka Araba, ambapo huingia Baharini. Yanapomwagikia kwenye hiyo Bahari, maji yaliyoko humo huponywa na kuwa safi.
The man said to me, “This water is going out to the eastern territory and down to the Arabah; this water flows into the Salt Sea and will make it fresh.
9 Popote mto huu uendapo kila kiumbe hai kinachoyaparamia hayo maji kitaishi, nako kutakuwa na samaki wengi mno, mara maji haya yafikapo huko. Maji hayo yatakuwa hai na kila kitu kitakachoishi kule mto uendako.
It will be that every living creature that swarms will live where the water goes; there will be many fish, for these waters flow there. It will make the salt water fresh. Everything will live wherever the river goes.
10 Wavuvi watasimama kando ya bahari, kuanzia En-Gedi hadi En-Eglaimu huko patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki. Samaki watakuwa wa aina nyingi, kama samaki wa Bahari Kuu
Then it will happen that fishermen of En Gedi will stand by the water, and there will be a place to dry out the fishing nets by En Eglaim. There will be many kinds of fish in the Salt Sea, like the fish in the Great Sea for their abundance.
11 Lakini madimbwi yake na mabwawa yake hayatakuwa na maji yanayofaa kunywa, bali yatabakia kuwa maji ya chumvi.
But the Salt Sea's swamps and marshes will not be made fresh; they will be for providing salt.
12 Miti ya matunda ya kila aina itaota kwenye kingo zote mbili za mto huu. Majani yake hayatanyauka wala haitaacha kuwa na matunda katika matawi yake. Kila mwezi kutakuwa na matunda, kwa sababu maji yatokayo patakatifu yanaitiririkia. Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatakuwa dawa.”
Beside this river on its banks, on both sides, all kinds of trees will grow that bear food. Their leaves will not wither and their fruit will never fail to grow. Each month the trees will bear fruit, because the water from the sanctuary flows to them. Their fruit will be for food, and their leaves will be for healing.
13 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “Hii ndiyo mipaka ambayo kwayo mtagawanya hiyo nchi kuwa urithi miongoni mwa hayo makabila kumi na mawili ya Israeli, pamoja na mafungu mawili ya Yosefu.
The Lord Yahweh says this: This will be the way that you divide the land up for the twelve tribes of Israel: Joseph will have two portions.
14 Mtagawa kwa usawa miongoni mwao. Kwa sababu niliapa kwa mkono ulioinuliwa kuwapa baba zenu, nchi hii itakuwa urithi wenu.
You are to divide equally what I lifted up my hand and swore to give to your fathers. This land will come to you as an inheritance.
15 “Huu ndio utakuwa mpaka wa hiyo nchi: “Upande wa kaskazini utaanzia Bahari Kuu kwa njia ya Hethloni kupitia Lebo-Hamathi hadi maingilio ya Sedadi.
This will be the boundary of the land on the north side from the Great Sea by way of Hethlon, and then to Zedad.
16 Berotha na Sibraimu (ambao uko kwenye mpaka kati ya Dameski na Hamathi), hadi kufikia Haser-Hatikoni, ambao uko katika mpaka wa Haurani.
Then the boundary will go to Berothah, to Sibraim, which is between Damascus and Hamath, and then to Hazer Hattikon, which is beside the boundary of Hauran.
17 Hivyo mpaka utaendelea kuanzia Baharini hadi Hasar-Enoni, ukiambaa na mpaka wa kaskazini wa Dameski, pamoja na mpaka wa Hamathi upande wa kaskazini. Huu utakuwa ndio mpaka wa kaskazini.
So the boundary will go from the sea to Hazar Enan on the border with Damascus and Hamath to the north. This will be the north side.
18 Upande wa mashariki mpaka utapita kati ya Haurani na Dameski, kuambaa Yordani na kati ya Gileadi na nchi ya Israeli, hadi bahari ya mashariki na kufika Tamari. Huu utakuwa ndio mpaka wa mashariki.
On the east side the boundary will run between Hauran and Damascus, along the Jordan River between Gilead and the land of Israel. You will measure from the border to the eastern sea. This will be the eastern border.
19 Upande wa kusini utaanzia Tamari hadi kufikia maji ya Meriba-Kadeshi, kisha utaambaa na Kijito cha Misri hadi Bahari Kuu. Huu utakuwa ndio mpaka wa kusini.
Then on the south side the boundary will run from Tamar as far as the waters of Meribah Kadesh, then along the brook of Egypt to the Great Sea. This will be the boundary on the south side.
20 Upande wa magharibi, Bahari Kuu itakuwa ndio mpaka hadi kwenye sehemu mkabala na Lebo-Hamathi. Huu utakuwa ndio mpaka wa magharibi.
Then the boundary on the west side will be the Great Sea to a point opposite Lebo Hamath. This will be the west side.
21 “Mtagawanya nchi hii miongoni mwenu kufuatana na makabila ya Israeli.
In this way you will divide this land for yourselves, for the tribes of Israel.
22 Mtaigawanya kuwa urithi kwa ajili yenu na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwenu na ambao wana watoto. Wao watakuwa kwenu kama wenyeji wazawa wa Israeli, pamoja na ninyi watagawiwa urithi miongoni mwa makabila ya Israeli.
So you will distribute the inheritances for yourselves and for the foreigners in your midst, those who have given birth to children in your midst and who are, with you, like the native born people of Israel. You will cast lots for inheritances among the tribes of Israel.
23 Katika kabila lolote mgeni atakapoishi hapo ndipo mtakapompatia urithi wake,” asema Bwana Mwenyezi.
Then it will happen that the foreigner will be with the tribe among whom he is living. You must give him an inheritance—this is the Lord Yahweh's declaration.”

< Ezekieli 47 >