< Ezekieli 39 >

1 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
Therefore, thou sonne of man, prophecie against Gog, and say, Thus sayeth the Lord God, Behold, I come against thee, O Gog, ye chiefe prince of Meshech and Tubal.
2 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukuburuta. Nitakuleta kutoka kaskazini ya mbali na kukupeleka wewe dhidi ya milima ya Israeli.
And I will destroy thee and leaue but the sixt part of thee, and will cause thee to come vp from the North partes and will bring thee vpon the mountaines of Israel:
3 Kisha nitaupiga upinde wako kutoka mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale ianguke kutoka mkono wako wa kuume.
And I will smite thy bowe out of thy left hand, and I will cause thine arrowes to fall out of thy right hand.
4 Utaanguka kwenye milima ya Israeli, wewe pamoja na vikosi vyako vyote na yale mataifa yaliyo pamoja nawe. Nitakutoa uwe chakula cha ndege wa aina zote walao nyama na cha wanyama wa mwituni.
Thou shalt fal vpon the mountaines of Israel, and all thy bands and the people, that is with thee: for I will giue thee vnto the birdes and to euery feathered foule and beast of the fielde to be deuoured.
5 Utaanguka katika uwanja, kwa kuwa nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
Thou shalt fall vpon the open fielde: for I haue spoken it, sayth the Lord God.
6 Nitatuma moto juu ya Magogu na kwa wale wanaoishi kwa salama huko pwani, nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
And I will sende a fire on Magog, and among them that dwell safely in the yles, and they shall knowe that I am the Lord.
7 “‘Nitalifanya Jina langu takatifu lijulikane miongoni mwa watu wangu Israeli. Sitaliacha tena Jina langu takatifu litiwe unajisi, nayo mataifa watajua kuwa Mimi Bwana ndimi Aliye Mtakatifu wa Israeli.
So will I make mine holy Name knowen in the middes of my people Israel, and I will not suffer them to pollute mine holy Name any more, and the heathen shall knowe that I am the Lord, the holy one of Israel.
8 Hili jambo linakuja! Hakika litatokea, asema Bwana Mwenyezi. Hii ndiyo siku ile niliyosema habari zake.
Beholde, it is come, and it is done, sayeth the Lord God: and this is the day whereof I haue spoken.
9 “‘Ndipo wale wanaoishi katika miji ya Israeli watakapotoka na kutumia hizo silaha kuwashia moto na kuziteketeza, yaani, kigao na ngao, pinde na mishale, rungu za vita na mikuki. Kwa miaka saba watavitumia kama kuni.
And they that dwell in the cities of Israel, shall goe forth, and shall burne and set fire vpon the weapons, and on the shieldes, and bucklers, vpon the bowes, and vpon the arrowes, and vpon the staues in their handes, and vpon the speares, and they shall burne them with fire seuen yeeres.
10 Hawatahitaji kukusanya kuni kutoka mashambani wala kukata kuni kutoka kwenye misitu, kwa sababu watatumia silaha kuwa kuni. Nao watawateka mateka wale waliowateka na kuchukua nyara mali za wale waliochukua mali zao nyara, asema Bwana Mwenyezi.
So that they shall bring no wood out of the fielde, neither cut downe any out of the forestes: for they shall burne the weapons with fire, and they shall robbe those that robbed them, and spoyle those that spoyled them, sayeth the Lord God.
11 “‘Siku ile nitampa Gogu mahali pa kuzikia katika Israeli, katika bonde la wale wasafirio upande wa mashariki kuelekea baharini. Jambo hili litazuia njia ya wasafiri kwa sababu Gogu na makundi yake yote ya wajeuri watazikwa huko. Kwa hiyo litaitwa Bonde la Hamon-Gogu.
And at the same time will I giue vnto Gog a place there for burial in Israel, euen the valley whereby men go towarde the East part of the sea: and it shall cause them that passe by, to stoppe their noses, and there shall they bury Gog with all his multitude: and they shall call it the valley of Hamon-Gog.
12 “‘Kwa miezi saba nyumba ya Israeli itakuwa ikiwazika ili kuisafisha nchi.
And seuen moneths long shall the house of Israel be burying of the, that they may clense the land.
13 Watu wote wa nchi watawazika, nayo siku nitakayotukuzwa itakuwa siku ya kumbukumbu kwa ajili yao, asema Bwana Mwenyezi.
Yea, all the people of the lande shall burie them, and they shall haue a name when I shall be glorified, saith the Lord God.
14 “‘Watu wataajiriwa mara kwa mara kuisafisha nchi. Baadhi yao watapita nchini kote na zaidi yao hao wengine, watawazika wale waliosalia juu ya uso wa nchi. Mwisho wa hiyo miezi saba wataanza upekuzi wao.
And they shall chuse out men to goe continually through the lande with them that trauaile, to bury those that remaine vpon ye ground, and clense it: they shall search to the ende of seuen moneths.
15 Wakati wanapopita nchini kote na mmoja wao akaona mfupa wa mwanadamu, ataweka alama kando yake mpaka wachimba kaburi wawe wameuzika katika Bonde la Hamon-Gogu.
And the trauailers that passe through the land, if any see a mans bone, then shall he set vp a signe by it, till the buriers haue buried it, in the valley of Hamon-Gog.
16 (Pia mji uitwao Hamona utakuwa humo.) Hivyo ndivyo watakavyoisafisha nchi.’
And also the name of the citie shalbe Hamonah: thus shall they clense the land.
17 “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ita kila aina ya ndege na wanyama wote wa mwituni, waambie: ‘Kusanyikeni mje pamoja kutoka pande zote kwa ajili ya dhabihu ninayowaandalia, dhabihu kuu katika milima ya Israeli. Huko mtakula nyama na kunywa damu.
And thou sonne of man, thus sayeth the Lord God, Speake vnto euery feathered foule, and to all the beastes of the fielde, Assemble your selues, and come gather your selues on euery side to my sacrifice: for I do sacrifice a great sacrifice for you vpon the mountaines of Israel, that ye may eate flesh, and drinke blood.
18 Mtakula nyama za watu mashujaa na kunywa damu za wakuu wa dunia kana kwamba ni za kondoo dume na kondoo wake, mbuzi na mafahali, wote walionona kutoka Bashani.
Ye shall eate the flesh of the valiant, and drink the blood of the princes of the earth, of the weathers, of the lambes, and of the goates, and of bullockes, euen of all fat beastes of Bashan.
19 Katika dhabihu ninayoandaa kwa ajili yenu, mtakula mafuta mpaka mkinai na kunywa damu mpaka mlewe.
And ye shall eate fat till you be full, and drinke blood, till ye be drunken of my sacrifice, which I haue sacrificed for you.
20 Kwenye meza yangu watajishibisha kwa farasi na wapanda farasi, watu mashujaa na askari wa kila aina,’ asema Bwana Mwenyezi.
Thus you shalbe filled at my table with horses and chariots, with valiant men, and with al men of warre, sayth the Lord God.
21 “Nitauonyesha utukufu wangu miongoni mwa mataifa, nayo mataifa yote wataiona adhabu nitakayotoa na mkono wangu nitakaouweka juu yao.
And I wil set my glory among the heathe, and all the heathen shall see my iudgement, that I haue executed, and mine hand, which I haue layed vpon them.
22 Kuanzia siku ile na kuendelea nyumba ya Israeli itajua kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wao.
So the house of Israel shall knowe, that I am the Lord their God from that day and so forth.
23 Na mataifa watajua kuwa nyumba ya Israeli walikwenda utumwani kwa ajili ya dhambi yao, kwa sababu hawakuwa waaminifu kwangu. Hivyo niliwaficha uso wangu na kuwatia mikononi mwa adui zao, nao wote wakaanguka kwa upanga.
And the heathen shall knowe, that ye house of Israel went into captiuitie for their iniquitie, because they trespassed against me: therefore hid I my face from them, and gaue them into ye hand of their enemies: so fell they all by the sword.
24 Niliwatendea sawasawa na uchafu wao na makosa yao, nami nikawaficha uso wangu.
According to their vncleannes, and according to their transgressions haue I done vnto the, and hid my face from them.
25 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Sasa nitamrudisha Yakobo kutoka utumwani, nami nitawahurumia watu wote wa Israeli, nami nitakuwa na wivu kwa ajili ya Jina langu takatifu.
Therefore thus sayth the Lord God, Nowe will I bring againe the captiuitie of Iaakob, and haue compassion vpon the whole house of Israel, and wil be ielous for mine holy Name,
26 Wataisahau aibu yao na jinsi walivyoonyesha kutokuwa waaminifu kwangu mimi wakati waliishi salama katika nchi yao, bila kuwa na mtu yeyote wa kuwatia hofu.
After that they haue borne their shame, and all their transgression, whereby they haue transgressed against me, whe they dwelt safely in their land, and without feare of any.
27 Nitakapokuwa nimewarudisha kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka nchi za adui zao, mimi nitajionyesha kuwa mtakatifu kwa kupitia kwao machoni mwa mataifa mengi.
When I haue brought them againe from the people, and gathered them out of their enemies landes, and am sanctified in them in the sight of many nations,
28 Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wao, ingawa niliwapeleka uhamishoni miongoni mwa mataifa, nitawakusanya tena katika nchi yao wenyewe, bila kumwacha yeyote nyuma.
Then shall they know, that I am the Lord their God, which caused them to be led into captiuitie among the heathen: but I haue gathered them vnto their owne land, and haue left none of them any more there,
29 Sitawaficha tena uso wangu, kwa maana nitamimina Roho wangu juu ya nyumba ya Israeli, asema Bwana Mwenyezi.”
Neither wil I hide my face any more from them: for I haue powred out my Spirit vpon the house of Israel, sayth the Lord God.

< Ezekieli 39 >