< Ezekieli 38 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
The word of Jehovah came to me, saying,
2 “Mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya Gogu, katika nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali, tabiri dhidi yake
"Son of man, set your face toward Gog, of the land of Magog, the chief prince of Meshech and Tubal, and prophesy against him,
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu, mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
and say, 'Thus says Jehovah: "Look, I am against you, Gog, chief prince of Meshech and Tubal:
4 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukutia ndoana kwenye mataya yako na kukutoa nje wewe pamoja na jeshi lako lote, yaani, farasi wako, wapanda farasi wako waliojiandaa tayari kwa vita, pamoja na kundi kubwa la wajeuri wakiwa na ngao na vigao, wote wakipunga panga zao.
and I will turn you around, and put hooks into your jaws, and I will bring you out, with all your army, horses and horsemen, all of them clothed in full armor, a great company with buckler and shield, all of them armed with swords;
5 Uajemi, Kushi na Putu watakuwa pamoja nao, wote wakiwa na ngao na kofia za chuma,
Persia, Ethiopia, and Put with them, all of them with shield and helmet;
6 pia Gomeri pamoja na vikosi vyake vyote, na Beth-Togarma kutoka kaskazini ya mbali pamoja na vikosi vyake vyote, mataifa mengi wakiwa pamoja nawe.
Gomer, and all his troops; the house of Togarmah in the uttermost parts of the north, and all his hordes; even many peoples with you.
7 “‘Jiandae, uwe tayari, wewe na makundi yako yote ya wajeuri yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe waamrishe.
"'"Be ready and stay ready, you and all your companies who are assembled to you, and be a guard to them.
8 Baada ya siku nyingi utaitwa vitani. Katika miaka ijayo, utaivamia nchi ile ambayo imepona kutoka vita, ambayo watu wake walikusanywa kutoka mataifa mengi kuja katika milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeachwa ukiwa. Wameletwa kutoka mataifa na sasa wote wanaishi katika hali ya salama.
After many days you shall be summoned: in the latter years you shall come to a land that is restored from war, a gathering from many peoples on the mountains of Israel, that had long been in ruins. Its people were brought out from the peoples, and all of them now live securely.
9 Wewe na vikosi vyako vyote na mataifa mengi yaliyo pamoja nawe mtapanda juu, mtawazoa kama tufani na kuifunika nchi kama wingu.
You shall advance, coming like a storm. You will be like a cloud covering the land, you, all your troops, and the many other peoples with you."
10 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mawazo yataingia moyoni mwako nawe utapanga mipango mibaya.
"'"Thus says Jehovah: "It shall happen on that day, that thoughts shall come into your mind, and you shall devise an an evil scheme:
11 Utasema, “Nitapigana vita na nchi ambayo vijiji vyake havina maboma. Nitawashambulia watu wanaoishi kwa amani na wasiotarajia vita: wote wanaishi bila maboma na bila malango na makomeo.
and you shall say, 'I will go up to the land of unwalled villages; I will go to those who who dwell securely, all of them dwelling without walls, and having neither bars nor gates;
12 Nitateka mateka na kuchukua nyara mali za wale waliorudi kuishi katika mahame na wale watu waliokusanywa kutoka kwa mataifa, ambao sasa wana mifugo na mali nyingi, wanaoishi katikati ya nchi.”
to seize spoil and carry off plunder; to turn my hand against the waste places that are now inhabited, acquired livestock and goods, who live at the center of the earth.'
13 Sheba na Dedani pamoja na wafanyabiashara wa Tarshishi na vijiji vyake vyote watakuambia, “Je, umekuja kuteka mateka? Je, umekusanya makundi yako ya wajeuri ili kuchukua nyara mali, kutwaa fedha na dhahabu, kutunyangʼanya mifugo na mali na kuteka nyara nyingi zaidi?”’
Sheba, and Dedan, and the merchants of Tarshish, with all its young warriors will say to you, 'Have you assembled your armies to carry off plunder, to carry away silver and gold, to take away cattle and goods, to to seize great spoil?'"'
14 “Kwa hiyo, mwanadamu, tabiri na umwambie Gogu: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile, watu wangu Israeli watakapokuwa wanaishi salama, Je, wewe mwenyewe hutalijua hilo?
"Therefore, son of man, prophesy, and tell Gog, 'Thus says Jehovah: "On that day when my people Israel are dwelling securely, you will take notice?
15 Utakuja kutoka kwako huko kaskazini ya mbali, ukiwa pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kundi kubwa, jeshi kuu.
You shall come from your place out of the uttermost parts of the north, you and many peoples with you, all of them riding on horses, a great company and a mighty army;
16 Utakuja dhidi ya watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Siku zijazo, ee Gogu, nitakuleta wewe dhidi ya nchi yangu, ili kwamba mataifa wapate kunijua Mimi nitakapojionyesha mtakatifu kwa kukupitia wewe mbele ya macho yao.
and you shall come up against my people Israel, as a cloud covering the land. But when this happens in future days, I will bring you against my land, so that the nations may know me, Gog, when through you I show my holiness in their sight."
17 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, wewe si yule niliyenena juu yako katika siku za zamani kwa kupitia kwa watumishi wangu manabii wa Israeli? Wakati ule walitabiri kwa miaka mingi kwamba ningekuleta upigane nao.
"'Thus says Jehovah: "Are you the one of whom I spoke in former days by my servants the prophets of Israel, who in those days prophesied for years that I would bring you against them?"
18 Hili ndilo litakalotokea katika siku ile: Gogu atakaposhambulia nchi ya Israeli, hasira yangu kali itaamka, asema Bwana Mwenyezi.
But it shall happen on that day, when Gog shall come against the land of Israel,' says Jehovah, 'that my hot anger will be aroused.
19 Katika wivu wangu na ghadhabu yangu kali ninasema kuwa wakati ule patakuwepo tetemeko kuu katika nchi ya Israeli.
For in my zeal, in the fire of my fury, I declare that on that day there shall be a great shaking in the land of Israel;
20 Samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kondeni, kila kiumbe kitambaacho ardhini, na watu wote walio juu ya uso wa nchi watatetemeka mbele zangu. Milima itapinduka, majabali yatapasuka na kila ukuta utaanguka chini.
so that the fish of the sea, and the birds of the sky, and the animals of the field, and all crawling creatures who crawl on the land, and all people who are on the face of the earth, shall shake at my presence. And the mountains shall be thrown down, and the cliffs shall fall, and every wall shall fall to the ground.
21 Nitaita upanga vita dhidi ya Gogu juu ya milima yangu yote, asema Bwana Mwenyezi. Upanga wa kila mtu utakuwa dhidi ya ndugu yake.
I will call for a sword against him on all my mountains,' says Jehovah: 'every man's sword shall be against his brother.
22 Nitatekeleza hukumu juu yake kwa tauni na kwa umwagaji wa damu. Nitaifanya mvua ya mafuriko kunyesha, mvua ya mawe na moto wa kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya mataifa mengi walio pamoja naye.
With pestilence and with bloodshed I will enter into judgment with him; and I will rain on him, and on his troops, and on the many peoples who are with him, torrential rains and hailstones, fire, and brimstone.
23 Nami hivyo ndivyo nitakavyoonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu, nami nitajijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
I will show my greatness and my holiness, and I will make myself known in the sight of many nations. Then they will know that I am Jehovah.'

< Ezekieli 38 >