< Ezekieli 35 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
Moreover the word of Jehovah came to me, saying,
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake
"Son of man, set your face against Mount Seir, and prophesy against it,
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume nawe, ee mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa na usiyekaliwa na watu wala kulimika.
and tell it, 'Thus says Jehovah: "Look, I am against you, Mount Seir, and I will stretch out my hand against you, and I will make you a desolation and an astonishment.
4 Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
I will lay your cities waste, and you shall be desolate; and you shall know that I am Jehovah.
5 “‘Kwa sababu ulificha moyoni uadui wa siku nyingi nawe ukawatoa Waisraeli wauawe kwa upanga wakati wa maafa yao, wakati adhabu yake ilipofikia kilele chake,
"'"Because you have had a perpetual enmity, and have given over the children of Israel to the power of the sword in the time of their calamity, in the time of the iniquity of the end;
6 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutia katika umwagaji damu nao utakufuatia. Kwa kuwa hakuchukia kumwaga damu, kumwaga damu kutakufuatia.
therefore, as I live," says Jehovah, "I will prepare you for blood, and blood shall pursue you: since you have not hated blood, therefore blood shall pursue you.
7 Nitaufanya Mlima Seiri ukiwa na usiokaliwa na watu wala kulimika na kuukatilia mbali na wote wanaokuja na wanaokwenda.
Thus will I make Mount Seir an astonishment and a desolation; and I will cut off from it him who passes through and him who returns.
8 Nitaijaza milima yenu kwa watu wake waliouawa, wale waliouawa kwa upanga wataanguka juu ya vilima vyako na katika mabonde yako na katika makorongo yako yote.
I will fill its mountains with its slain: in your hills and in your valleys and in all your watercourses shall they fall who are slain with the sword.
9 Nitakufanya ukiwa milele, watu hawataishi katika miji yako. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
I will make you a perpetual desolation, and your cities shall not be inhabited; and you shall know that I am Jehovah.
10 “‘Kwa sababu umesema, “Mataifa haya mawili na nchi hizi zitakuwa zetu nasi tutazimiliki,” ingawa hata mimi Bwana nilikuwa huko,
"'"Because you have said, 'These two nations and these two countries shall be mine, and we will possess it'; whereas Jehovah was there:
11 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutenda kwa kadiri ya hasira na wivu uliouonyesha katika chuki yako juu yao nami nitafanya nijulikane miongoni mwao wakati nitakapokuhukumu.
therefore, as I live," says Jehovah, "I will do according to your anger, and according to your envy which you have shown out of your hatred against them; and I will make myself known among them, when I shall judge you.
12 Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema dhidi ya milima ya Israeli. Ulisema, “Wamefanyika ukiwa na kutiwa mikononi mwetu tuwararue.”
You shall know that I, Jehovah, have heard all your insults which you have spoken against the mountains of Israel, saying, They are laid desolate, they have been given us to devour.
13 Ulijigamba dhidi yangu na kusema maneno dhidi yangu bila kujizuia, nami nikayasikia.
You have magnified yourselves against me with your mouth, and have multiplied your words against me: I have heard it."
14 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati dunia yote inashangilia nitakufanya ukiwa.
Thus says Jehovah: "When the whole earth rejoices, I will make you desolate.
15 Kwa sababu ulishangilia wakati urithi wa nyumba ya Israeli ulipofanyika ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea. Utakuwa ukiwa, ee mlima Seiri, wewe na Edomu yote. Kisha ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
As you rejoiced over the inheritance of the house of Israel, because it was desolate, so will I do to you: you shall be desolate, Mount Seir, and all Edom, even all of it; and they shall know that I am Jehovah."'"

< Ezekieli 35 >