< Ezekieli 29 >

1 Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili, neno la Bwana likanijia kusema:
In the tenth year, in the tenth month on the twelfth day of the month, the word of Yahweh came to me, saying,
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Farao mfalme wa Misri na utabiri dhidi yake na dhidi ya Misri yote.
“Son of man, set your face against Pharaoh, the king of Egypt; prophesy against him and against all of Egypt.
3 Nena, nawe useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Mimi ni kinyume nawe, Farao, mfalme wa Misri, joka kubwa ulalaye katikati ya vijito vyako. Unasema, “Mto Naili ni wangu mwenyewe; niliufanya kwa ajili yangu mwenyewe.”
Declare and say, 'The Lord Yahweh says this: Behold! I am against you, Pharaoh, king of Egypt. You, the great sea monster that lurks in the midst of the river, that says, “My river is my own. I have made it for myself.”
4 Lakini nitatia ndoana katika mataya yako nami nitawafanya samaki wa vijito vyako washikamane na magamba yako. Nitakutoa katikati ya vijito vyako, pamoja na samaki wote walioshikamana na magamba yako.
For I will place hooks in your jaw, and the fish of your Nile will cling to your scales; I will lift you up from the middle of your river along with all the fish of the river that cling to your scales.
5 Nitakutupa jangwani, wewe pamoja na samaki wote wa vijito vyako. Utaanguka uwanjani, nawe hutakusanywa au kuchukuliwa. Nitakutoa uwe chakula kwa wanyama wa nchi na ndege wa angani.
I will throw you down into the wilderness, you and all the fish from your river. You will fall on the open field; you will not be gathered nor lifted up. I will give you as food to the living things of the earth and to the birds of the heavens.
6 Ndipo wale wote waishio Misri watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Umekuwa fimbo ya tete kwa nyumba ya Israeli.
Then all the inhabitants of Egypt will know that I am Yahweh, because they have been a reed stalk to the house of Israel.
7 Walipokushika kwa mikono yao, ulivunjika na kuchana mabega yao; walipokuegemea, ulivunjika na migongo yao ikateguka.
When they took hold of you in their hand, you broke and tore open their shoulder; and when they leaned on you, you were broken, and you caused their legs to be unsteady.
8 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaleta upanga juu yako na kuua watu wako na wanyama wao.
Therefore the Lord Yahweh says this: Behold! I will bring a sword against you. I will cut off both man and beast from you.
9 Misri itakuwa ukiwa na isiyolimwa wala kukaliwa na watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Kwa sababu ulisema, “Mto Naili ni wangu; mimi niliufanya,”
So the land of Egypt will become desolate and a ruin. Then they will know that I am Yahweh, because the sea monster had said, “The river is mine, for I have made it.”
10 kwa hiyo mimi ni kinyume nawe na kinyume na vijito vyako, nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa magofu na ukiwa isiyolimwa wala kukaliwa na watu kuanzia Migdoli hadi Aswani, hata kufikia mpakani wa Ethiopia.
Therefore, behold! I am against you and against your river, so I will give the land of Egypt over to desolation and waste, and you will become a wasteland from the Migdol to Syene and the borders of Cush.
11 Hakuna unyayo wa mtu au mnyama utakaopita ndani yake, wala hakuna yeyote atakayeishi humo kwa muda wa miaka arobaini.
No man's foot will pass through it, and no wild animal's foot will pass through it. It will not be inhabited for forty years.
12 Nitaifanya nchi ya Misri ukiwa, miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yake itabaki ukiwa miaka arobaini miongoni mwa miji iliyo magofu. Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi nyingine.
For I will make the land of Egypt a desolation in the midst of uninhabited lands, and its cities in the midst of wasted cities will become a desolation for forty years; then I will scatter Egypt among the nations, and I will disperse them though the lands.
13 “‘Lakini hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mwishoni mwa hiyo miaka arobaini, nitawakusanya Wamisri kutoka mataifa walikotawanywa.
For the Lord Yahweh says this: At the end of forty years I will gather Egypt from the peoples among whom they were scattered.
14 Nitawarudisha hao Wamisri kutoka kwenye kutekwa kwao na kuwaweka katika Pathrosi, nchi ya baba zao. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu.
I will restore the fortunes of Egypt and bring them back to the region of Pathros, to the land of their origin. Then they will be a lowly kingdom there.
15 Utakuwa ufalme dhaifu kuliko zote na kamwe Misri haitajikweza tena juu ya mataifa mengine. Nitaufanya ufalme wake dhaifu sana kiasi kwamba kamwe hautatawala tena juu ya mataifa mengine.
It will be the lowliest of the kingdoms, and it will not be lifted up any more among the nations. I will diminish them so they will no longer rule over nations.
16 Misri haitakuwa tena tumaini la watu wa Israeli bali itakuwa kumbukumbu ya dhambi yao kwa kuigeukia kuomba msaada. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’”
The Egyptians will no longer be a reason for confidence for the house of Israel. Instead, they will be a reminder of the iniquity that Israel committed when they turned to Egypt for help. Then they will know that I am the Lord Yahweh.'”
17 Katika mwaka wa ishirini na saba, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
Then it came about in the twenty-seventh year on the first of the first month, that the word of Yahweh came to me, saying,
18 “Mwanadamu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliongoza jeshi lake kufanya kazi ngumu dhidi ya Tiro; kila kichwa kilipata upaa na kila bega likachunika. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kutokana na muda wote aliongoza hiyo vita dhidi ya Tiro.
“Son of man, Nebuchadnezzar the king of Babylon stationed his army to do hard work against Tyre. Every head was rubbed until it was made bald, and every shoulder was made raw. Yet he and his army received no payment from Tyre for the hard work that he carried out against it.
19 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaitia Misri mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atachukua utajiri wa Misri. Atateka mateka na kuchukua nyara mali za Misri kama ujira kwa ajili ya jeshi lake.
Therefore the Lord Yahweh says this, 'Behold! I am giving the land of Egypt to Nebuchadnezzar the king of Babylon, and he will take away its wealth, plunder its possessions, and carry off all he finds there; that will be his army's wages.
20 Nimempa mfalme wa Babeli nchi ya Misri kuwa ujira kwa juhudi zake kwa sababu yeye na jeshi lake walifanya kwa ajili yangu, asema Bwana Mwenyezi.
I have given him the land of Egypt as the wages for the work they did for me—this is the Lord Yahweh's declaration.
21 “Katika siku hiyo nitaifanya nyumba ya Israeli iwe na nguvu nami nitakifungua kinywa chako miongoni mwao. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”
On that day I will make a horn sprout up for the house of Israel, and I make you speak in their midst, so that they will know that I am Yahweh.'”

< Ezekieli 29 >