< Ezekieli 26 >

1 Mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
And it was doon in the enleuenthe yeer, in the firste dai of the monethe, the word of the Lord was maad to me, and he seide,
2 “Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu, ‘Aha! Lango la kwenda kwa mataifa limevunjika, nayo milango yake iko wazi mbele yangu, sasa kwa kuwa amekuwa magofu nitastawi.’
Thou, sone of man, for that that Tire seide of Jerusalem, Wel! the yatis of puplis ben brokun, it is turned to me; Y schal be fillid, it is forsakun;
3 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na wewe, ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi dhidi yako, kama bahari inayovurumisha mawimbi yake.
therfor the Lord God seith these thingis, Lo! Tire, Y on thee; and Y schal make many folkis to stie to thee, as the see flowynge stieth.
4 Watavunja kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nitakwangua udongo wake na kuufanya mwamba mtupu.
And thei schulen distrie the wallis of Tire, and thei schulen distrie the touris therof; and Y schal rase the dust therof fro it, and Y schal yyue it in to a `moost clere stoon.
5 Itakuwa huko katikati ya bahari patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki, kwa maana nimenena, asema Bwana Mwenyezi. Atakuwa nyara kwa mataifa,
Driyng of nettis schal be in the myddis of the see, for Y spak, seith the Lord God. And Tire schal be in to rauysching to hethene men.
6 nayo makao yake huko bara yataangamizwa kwa upanga. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.
And the douytris therof that ben in the feeld, schulen be slayn bi swerd; and thei schulen wite, that Y am the Lord.
7 “Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kutoka kaskazini nitamleta dhidi ya Tiro Mfalme Nebukadneza wa Babeli, mfalme wa wafalme, akiwa na farasi na magari ya vita, wapanda farasi na jeshi kubwa.
For whi the Lord God seith these thingis, Lo! Y schal brynge to Tire Nabugodonosor, the king of Babiloyne, fro the north, the kyng of kyngis, with horsis, and charis, and knyytis, and with a cumpeny, and greet puple.
8 Atayaharibu makao yako huko bara kwa upanga, ataweka jeshi kukuzingira, atakuzingira mpaka kwenye kuta za ngome zako na kuinua ngao zake dhidi yako.
He schal sle bi swerd thi douytris that ben in the feeld, and he schal cumpasse thee with strengthingis, and he schal bere togidere erthe in cumpas. And he schal reise a scheeld ayens thee,
9 Ataelekeza mapigo ya vyombo vyake vya kubomolea dhidi ya kuta zako na kubomoa minara yako kwa silaha zake.
and he schal tempre engynes lijc vineres, and engines `that ben clepid wetheris ayens thi wallis; and he schal distrie thi touris bi his armure.
10 Farasi zake zitakuwa nyingi sana kiasi kwamba utafunikwa na mavumbi watakayotimua. Kuta zako zitatikisika kwa mshindo wa farasi wa vita, magari makubwa na magari ya vita wakati aingiapo malango yako kama watu waingiao mji ambao kuta zake zimebomolewa kote.
Bi flowynge of his horsis, the dust of tho schal hile thee; thi wallis schulen be mouyd of the soun of knyytis, and of wheelis, and of charis; whanne he schal entre bi the yatis, as bi entryngis of a citee distried,
11 “Kwato za farasi zake zitakanyaga barabara zako zote, atawaua watu wako kwa upanga na nguzo zako zilizo imara zitaanguka chini.
with the clees of hise horsis he schal defoule alle thi stretis. He shal sle bi swerd thi puple, and thi noble ymagis schulen falle doun in to erthe.
12 Watateka utajiri wako na kuchukua nyara bidhaa zako, watazivunja kuta zako na kuzibomoa nyumba zako nzuri, watatupa baharini mawe yako, mbao zako na kifusi chako.
Thei schulen waste thi richessis, thei schulen rauysche thi marchaundies; and thei schulen distrie thi wallis, and thei schulen distrie thin housis ful clere, and thi stoonys, and thi trees, and thei schulen putte thi dust in the myddis of watris.
13 Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na uimbaji wako wa kinubi kamwe hautasikika tena.
And Y schal make to reste the multitude of thi syngeris, and the sown of thin harpis schal no more be herd;
14 Nitakufanya mwamba mtupu, nawe utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za kuvulia samaki. Kamwe hutajengwa tena, kwa maana Mimi Bwana nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
and Y schal yyue thee in to a moost cleer stoon. Thou schalt be driyng of nettis, and thou schalt no more be bildid, for Y the Lord spak, seith the Lord God.
15 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa Tiro: ‘Je, nchi za pwani hazitatetemeka kwa kishindo cha anguko lako, wakati majeruhi wanapolia kwa maumivu makali na wakati mauaji yanaendelea ndani yako?
The Lord God seith these thingis of Tire, Whether ilis schulen not be moued of the sown of thi fal, and of weiling of thi slayn men, whanne thei ben slayn in the myddis of thee?
16 Ndipo wakuu wote wa mataifa ya pwani watashuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuweka kando majoho yao na kuvua nguo zao zilizotariziwa. Wakiwa wamevikwa hofu kuu, wataketi chini ardhini, wakiwa wanatetemeka kila dakika na wakikustajabia.
And alle the princis of the see schulen go doun of her seetis, and thei schulen do awei her mentils, ether spuylis of slayn enemyes, and thei schulen caste awei her dyuerse clothis, and shulen be clothid with wondring. Thei shulen sitte in the erthe, and thei shulen be astonyed, and thei shulen wondre of thi sodeyn fal.
17 Ndipo wao watakuombolezea na kukuambia: “‘Tazama jinsi ulivyoharibiwa, ee mji uliokuwa na sifa, wewe uliyekaliwa na mabaharia! Ulikuwa na nguvu kwenye bahari, wewe na watu wako; wote walioishi huko, uliwatia hofu kuu.
And thei shulen take weilyng on thee, and schule seie to thee, Hou perischidist thou, noble citee, that dwellist in the see, that were strong in the see with thi dwelleris, whiche dwelleris alle men dredden?
18 Sasa nchi za pwani zinatetemeka katika siku ya anguko lako; visiwa vilivyomo baharini vinaogopa kwa kuporomoka kwako.’
Now schippis schulen wondre in the dai of thi drede, and ilis in the see schulen be disturblid, for noon goith out of thee.
19 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapokufanya uwe mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa tena na watu, nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako na maji yake makuu yatakapokufunika,
For the Lord God seith these thingis, Whanne Y schal yyue thee a citee desolat, as the citees that ben not enhabitid, and Y schal bringe on thee the depthe of watris, and many watris schulen hile thee.
20 ndipo nitakapokushusha chini pamoja na wale washukao shimoni, kwa watu wa kale, nami nitakufanya uishi katika pande za chini za nchi kama katika magofu ya kale, pamoja na wale washukao shimoni, nawe hutarudi au kurejea kwenye makao yako katika nchi ya walio hai.
And Y schal drawe thee doun with hem that goon doun in to a lake, to the puple euerlastynge; and Y schal sette thee in the laste lond, as elde wildirnessis, with hem that ben led doun in to a lake, that thou be not enhabited. Certis whanne Y schal yyue glorye in the lond of lyueris,
21 Nitakufikisha mwisho wa kutisha wala hutakuwepo tena. Watu watakutafuta, lakini kamwe hutaonekana tena, asema Bwana Mwenyezi.”
Y schal dryue thee in to nouyt, and thou schalt not be; and thou schalt be souyt, and thou schalt no more be foundun with outen ende, seith the Lord God.

< Ezekieli 26 >