< Ezekieli 21 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole de l’Éternel vint à moi, disant:
2 “Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
Fils d’homme, tourne ta face contre Jérusalem, et distille [tes paroles] contre les sanctuaires, et prophétise contre la terre d’Israël,
3 uiambie: ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
et dis à la terre d’Israël: Ainsi dit l’Éternel: Voici, c’est à toi que j’en veux, et je tirerai mon épée de son fourreau, et je retrancherai de toi le juste et le méchant.
4 Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utakuwa wazi dhidi ya kila mmoja kuanzia kusini mpaka kaskazini.
Parce que je retrancherai de toi le juste et le méchant, à cause de cela mon épée sortira de son fourreau contre toute chair, du midi jusqu’au nord;
5 Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Bwana nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
et toute chair saura que moi, l’Éternel, j’ai tiré mon épée de son fourreau: elle n’y retournera plus.
6 “Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
Et toi, fils d’homme, gémis à te briser les reins, gémis avec amertume devant leurs yeux.
7 Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatokea, asema Bwana Mwenyezi.”
Et il arrivera que, quand ils te diront: Pourquoi gémis-tu? tu diras: C’est à cause de la rumeur, car elle vient; et tout cœur sera défaillant, et toutes les mains deviendront lâches, et tout esprit faiblira, et tous les genoux se fondront en eau. Voici, elle vient, elle est là, dit le Seigneur, l’Éternel.
8 Neno la Bwana likanijia, kusema:
Et la parole de l’Éternel vint à moi, disant:
9 “Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
Fils d’homme, prophétise, et dis: Ainsi dit l’Éternel: Dis: L’épée, l’épée est aiguisée et aussi fourbie.
10 umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ungʼae kama umeme wa radi! “‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unaidharau kila fimbo ya namna hiyo.
C’est afin qu’elle égorge bien, qu’elle est aiguisée; c’est pour briller comme l’éclair, qu’elle est fourbie. Ou bien nous réjouirions-nous, [disant]: Le sceptre de mon fils méprise tout bois?
11 “‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
Et il l’a donnée à fourbir, pour qu’on la prenne dans la main; c’est une épée aiguisée, et elle est fourbie, pour la mettre dans la main de celui qui tue.
12 Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
Crie et hurle, fils d’homme! Car elle sera contre mon peuple, elle sera contre tous les princes d’Israël: ils sont livrés à l’épée avec mon peuple; c’est pourquoi frappe sur ta cuisse.
13 “‘Kwa maana upanga huu umejaribiwa na kuhakikishwa, itakuwaje basi fimbo ya ufalme ya Yuda inayoudharau kama haitakuwepo tena, bali itakuwa imeondolewa kabisa? asema Bwana Mwenyezi.’
Car l’épreuve [est faite]; et quoi?… si même le sceptre méprisant n’existe plus? dit le Seigneur, l’Éternel.
14 “Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa kuchinja, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
Et toi, fils d’homme, prophétise, et frappe tes mains l’une contre l’autre, et que [les coups de] l’épée redoublent jusqu’à la troisième fois; c’est l’épée des tués, l’épée qui a tué le grand, [et] qui les environne.
15 Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa kuchinja kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama umeme wa radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
C’est afin que le cœur se fonde et que les occasions de chute soient multipliées, que j’envoie l’épée menaçante contre toutes leurs portes. Ah! elle est faite pour briller comme l’éclair, et affilée pour tuer.
16 Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
Ramasse [tes forces], va à droite, tourne-toi, va à gauche, où que ta face soit dirigée.
17 Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Bwana nimesema.”
Et moi aussi je frapperai mes mains l’une contre l’autre, et je satisferai ma fureur. Moi, l’Éternel, j’ai parlé.
18 Neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole de l’Éternel vint à moi, disant:
19 “Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
Et toi, fils d’homme, place devant toi deux chemins par où vienne l’épée du roi de Babylone: qu’ils partent tous deux du même pays; et fais-toi un indicateur, fais-le à l’entrée du chemin d’une ville.
20 Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
Tu disposeras un chemin pour que l’épée vienne à Rabba des fils d’Ammon, et [un chemin] en Juda, [pour que l’épée vienne] à Jérusalem, la [ville] forte.
21 Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
Car le roi de Babylone se tient au point d’embranchement de la route, à la tête des deux chemins, pour pratiquer la divination: il secoue les flèches, il interroge les théraphim, il examine le foie.
22 Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka vyombo vya kuvunjia boma, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka vyombo vya kuvunjia boma kwenye malango, kuweka jeshi kuzunguka na kufanya uzingiraji.
Dans sa droite est la divination touchant Jérusalem, pour placer des béliers, pour qu’on ouvre la bouche en cris de carnage, pour qu’on élève la voix en cris de guerre, pour placer des béliers contre les portes, pour élever des terrasses, pour bâtir des tours.
23 Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha juu ya uovu wao na kuwachukua mateka.
Et ce sera pour eux, à leurs yeux, une divination fausse, pour eux qui se sont engagés par serment; mais lui, il rappellera le souvenir de l’iniquité, pour qu’ils soient pris.
24 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu enyi watu mmekumbusha uovu wenu kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mfanyayo, kwa kuwa mmefanya jambo hili, mtachukuliwa mateka.
C’est pourquoi, ainsi dit le Seigneur, l’Éternel: Parce que vous rappelez en mémoire votre iniquité, en ce que vos transgressions sont découvertes, de sorte que vos péchés paraissent dans toutes vos actions; parce que vous êtes rappelés en mémoire, vous serez pris par [sa] main.
25 “‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yako imewadia, ambaye wakati wako wa adhabu umefikia kilele chake,
Et toi, profane, méchant prince d’Israël, dont le jour est venu au temps de l’iniquité de la fin,
26 hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa na aliyekwezwa atashushwa.
ainsi dit le Seigneur, l’Éternel: Ôte la tiare, et enlève la couronne; ce qui est ne sera plus. Élève ce qui est bas, et abaisse ce qui est élevé.
27 Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya mpaka aje yule ambaye ndiye mwenye haki nao; yeye ndiye nitakayempa.’
J’en ferai une ruine, une ruine, une ruine! Ceci aussi ne sera plus, jusqu’à ce que vienne celui auquel appartient le juste jugement, et je le lui donnerai.
28 “Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao. “‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama umeme wa radi!
Et toi, fils d’homme, prophétise, et dis: Ainsi dit le Seigneur, l’Éternel, touchant les fils d’Ammon et touchant leur opprobre; et tu diras: L’épée, l’épée est tirée, elle est fourbie pour la tuerie, pour dévorer, pour briller,
29 Wakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako, wanapobashiri uongo kwa ajili yako, wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu, wale walio waovu, wale ambao siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
pendant qu’ils ont pour toi des visions de vanité et qu’ils devinent pour toi le mensonge, pour te jeter sur les cous des méchants qui sont tués, dont le jour est venu au temps de l’iniquité de la fin.
30 Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
Remets-la dans son fourreau! Je te jugerai au lieu où tu fus créé, au pays de ton origine.
31 Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
Je verserai sur toi mon indignation, je soufflerai contre toi le feu de mon courroux, et je te livrerai en la main d’hommes brutaux, artisans de destruction.
32 Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Bwana nimesema.’”
Tu seras pour le feu, pour être dévoré; ton sang sera au milieu du pays; on ne se souviendra pas de toi; car moi, l’Éternel, j’ai parlé.

< Ezekieli 21 >