< Kutoka 39 >

1 Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Iz modre, vijolične in škrlatne so naredili službene obleke, da opravljajo službo na svetem kraju in naredijo sveta oblačila za Arona; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
2 Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
Naredil je efód iz zlate, modre, vijolične, škrlatne in sukane tančice.
3 Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
Zlato so prekovali v tanke plošče in ga narezali v žice, da bi ga vdelali v modro, v vijolično, v škrlatno in v tanko laneno platno, s spretno izdelavo.
4 Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
Za to so naredili obramna dela, da to spojijo skupaj; z dvema robovoma je bilo to spojeno skupaj.
5 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Skrbno narejen pas njegovega efóda, ki je bil na njem, je bil iz istega, glede na njegovo delo; iz zlate, modre, vijolične, škrlatne in sukane tančice; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
6 Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
Izdelali so oniksova kamna, obdana z ležiščema iz zlata, vgravirana kakor so vgravirani pečati, z imeni Izraelovih otrok.
7 Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Položil jih je na ramena efóda, da bodo kamni za spomin Izraelovim otrokom; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
8 Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
Naredil je naprsnik spretne izdelave, podoben efódovemu delu; iz zlate, modre, vijolične, škrlatne in sukane tančice.
9 Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
Bil je štirioglat; naprsnik so naredili prepognjen. Pedenj je bila njegova dolžina in pedenj njegova širina; bil je prepognjen.
10 Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
Na njem so postavili štiri vrste kamnov. Prva vrsta je bil sardij, topaz in granat. To je bila prva vrsta.
11 safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
Druga vrsta smaragd, safir in diamant.
12 safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
Tretja vrsta hijacint, ahat in ametist.
13 katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
Četrta vrsta beril, oniks in jaspis; bili so obdani v ležišča iz zlata v njihovih obdanostih.
14 Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
Kamni so bili glede na imena Izraelovih otrok, dvanajst, glede na njihova imena, podobni gravuram pečata, vsak s svojim imenom, glede na dvanajst rodov.
15 Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
Na naprsniku so naredili verižici na krajih, iz spletenega dela, iz čistega zlata.
16 Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
Naredili so dve ležišči iz zlata in dva zlata obročka in dva zlata obročka vstavili v dva konca naprsnika.
17 Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
Vstavili so dve spleteni verižici iz zlata v dva obročka, na krajeh naprsnika.
18 nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
Dva konca dveh spletenih verižic so privezali na dve ležišči in ju pritrdili na obramna dela efóda, pred njim.
19 Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
Naredili so dva obročka iz zlata in ju položili na dva konca naprsnika, na njegov rob, ki je bil na notranji strani efóda.
20 Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
Naredili so dva druga zlata obročka in ju položili na dve strani pod efód, proti njegovi prednji strani, nasproti drugemu njegovemu spoju, nad skrbno narejenim pasom efóda.
21 Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Naprsnik z njegovimi obročki so z modrim trakom privezali k obročkom efóda, da bi bil ta lahko nad skrbno narejenim pasom efóda in da se naprsnik ne bi odvezal od efóda; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
22 Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
Naredil je svečano oblačilo efóda iz spletenega dela, celega iz modre.
23 na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
Bila je luknja v sredi svečanega oblačila, kakor luknja brezrokavne verižne srajce s trakom naokoli luknje, da se ne raztrga.
24 Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
Na obšivih svečanega oblačila so naredili granatna jabolka iz modre, vijolične, škrlatne in sukane tančice.
25 Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
Naredili so zvončke iz čistega zlata in zvončke postavili med granatna jabolka, na obšivu svečanega oblačila, naokoli med granatnimi jabolki;
26 Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
zvonček in granatno jabolko, zvonček in granatno jabolko naokoli obšiva svečanega oblačila za služenje v tem; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
27 Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
Naredili so plašče iz tankega lanenega platna iz spletenega dela, za Arona in za njegove sinove
28 na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
in turban iz tankega lanenega platna in čedne klobučke iz tankega lanenega platna in kratke platnene hlače iz sukane tančice
29 Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
in pas iz sukane tančice in modre in vijolične in škrlatne, iz vezenine; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
30 Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
Naredili so ploščico svete krone iz čistega zlata in nanjo napisali pisanje, podobno gravuram pečata: » SVETO Gospodu.«
31 Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
K temu so privezali moder trak, da ga pričvrstijo visoko na turbanu; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
32 Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
Tako je bilo vse delo šotorskega svetišča skupnosti končano. Izraelovi otroci so storili glede na vse, kar je Gospod zapovedal Mojzesu, tako so storili.
33 Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
Šotorsko svetišče so prinesli k Mojzesu, šotor, vso njegovo opremo, njegove zaponke, njegove deske, njegove zapahe, njegove stebre, njegove podstavke,
34 kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
pokrivalo rdeče barvanih ovnovih kož, pokrivalo iz jazbečevih kož, zagrinjalo pokrivala,
35 Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
skrinjo pričevanja, njena drogova, sedež milosti,
36 meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
mizo in vse njene posode in hlebe navzočnosti,
37 kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
čisti svečnik z njegovimi svetilkami, celo s svetilkami, da so razvrščene in vse njegove posode in olje za svetlobo,
38 madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
zlat oltar, mazilno olje in dišeče kadilo, tanko preprogo za vrata šotorskega svetišča,
39 madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
bronast oltar, njegovo rešetko iz brona, njegova drogova in vse njegove posode, [okrogel] umivalnik in njegovo vznožje,
40 mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
tanko preprogo dvora, njegove stebre in njegove podstavke, tanko preprogo za velika dvorna vrata, njene vrvice in njene količke in vse posode službe šotorskega svetišča za shodni šotor,
41 na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
službene obleke, da opravljajo službo na svetem kraju in sveta oblačila za duhovnika Arona in oblačila njegovih sinov, za služenje v duhovniški službi.
42 Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
Glede na vse, kar je Gospod zapovedal Mojzesu, tako so Izraelovi otroci opravili vse delo.
43 Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.
Mojzes je pogledal na vse delo in glej, naredili so ga kakor je Gospod zapovedal, celo tako so ga naredili, in Mojzes jih je blagoslovil.

< Kutoka 39 >