< Kutoka 39 >

1 Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Także z błękitnej [tkaniny], purpury i karmazynu zrobili szaty do służby, do posługiwania w świątyni. Zrobili też święte szaty dla Aarona, jak PAN rozkazał Mojżeszowi.
2 Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
I zrobili efod ze złota, błękitnej [tkaniny], purpury, karmazynu i skręconego bisioru.
3 Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
Naklepali też złote blaszki i nacięli z nich nici do przetykania haftem błękitnej [tkaniny], purpury, karmazynu i bisioru.
4 Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
Zrobili do niego naramienniki, aby się jeden z drugim mógł złączyć. Łączyły się na dwóch końcach.
5 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Także pas do efodu, który był na nim, z tego samego był i tak samo zrobiony: ze złota, błękitnej [tkaniny], purpury, karmazynu i skręconego bisioru, jak PAN rozkazał Mojżeszowi.
6 Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
Do tego obrobili kamienie onyksu osadzone w złotych oprawkach, wyryte tak jak pieczęci bywają ryte, z imionami synów Izraela.
7 Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
I umieścili je na naramiennikach efodu, [aby były] kamieniami pamiątkowymi dla synów Izraela, jak PAN rozkazał Mojżeszowi.
8 Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
Zrobili też haftowany pektorał podobnie jak efod: ze złota, błękitnej [tkaniny], purpury, karmazynu i skręconego bisioru.
9 Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
Był kwadratowy; zrobili podwójny pektorał, na piędź długości i na piędź szerokości, złożony we dwoje.
10 Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
I osadzili w nim cztery rzędy kamieni w [tym] porządku: karneol, topaz i szmaragd w pierwszym rzędzie.
11 safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
A w drugim rzędzie: karbunkuł, szafir i diament.
12 safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
A w trzecim rzędzie: hiacynt, agat i ametyst.
13 katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
A w czwartym rzędzie: beryl, onyks i jaspis, wszystkie osadzone w złotych oprawach.
14 Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
A tych kamieni z imionami synów Izraela było dwanaście, według ich imion, [które] ryte [były] jak na pieczęci; każdy według swego imienia, według dwunastu pokoleń.
15 Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
Zrobili też do pektorału łańcuszki plecione ze szczerego złota.
16 Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
Zrobili także dwie złote oprawki i dwa złote pierścienie i przyczepili te dwa pierścienie do obu rogów pektorału.
17 Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
I włożyli te dwa złote łańcuszki w oba pierścienie u rogów pektorału.
18 nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
Drugie zaś końce obu łańcuszków przymocowali do tych dwóch oprawek i przyprawili z przodu do naramienników efodu.
19 Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
Zrobili również dwa złote pierścienie, które przymocowali do dwóch rogów pektorału na jego wewnętrznym brzegu, który był od strony efodu.
20 Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
Zrobili jeszcze dwa złote pierścienie, które przyprawili na dwie strony efodu, u dołu, naprzeciwko jego spojenia, ponad pasem efodu.
21 Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
I przywiązali pektorał jego pierścieniami do pierścieni efodu sznurem błękitnym, aby był nad pasem efodu, żeby pektorał nie odstawał od efodu, jak PAN rozkazał Mojżeszowi.
22 Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
Zrobili także tkany płaszcz pod efod, cały z błękitnej [tkaniny];
23 na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
A pośrodku płaszcza otwór, jak otwór w pancerzu, i obwódkę dokoła brzegu, aby się nie rozdzierał.
24 Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
Także u dołu tego płaszcza zrobili jabłka granatu z błękitnej [tkaniny], purpury, karmazynu i skręconego [bisioru].
25 Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
Zrobili też dzwonki ze szczerego złota i pozawieszali te dzwonki między te jabłka granatu u dołu dokoła płaszcza, pośród jabłek granatu;
26 Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Dzwonek, a potem jabłko granatu i znów dzwonek, i jabłko granatu, u dołu dokoła płaszcza do usługiwania, jak PAN rozkazał Mojżeszowi.
27 Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
Zrobili też dla Aarona i jego synów szaty tkane z bisioru.
28 na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
Mitrę także z bisioru i ozdobne mitry z bisioru, i spodnie ze skręconego bisioru.
29 Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Pas także ze skręconego bisioru, błękitnej [tkaniny], purpury i karmazynu, haftowany, jak PAN rozkazał Mojżeszowi.
30 Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
Zrobili też blaszkę do świętej korony ze szczerego złota i wyryli na niej napis jak na pieczęci: Świętość PANU.
31 Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
A przymocowali do niej sznur z błękitnej [tkaniny], aby była przywiązana na przodzie mitry, jak PAN rozkazał Mojżeszowi.
32 Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
I tak skończyły się wszystkie prace około przybytku, [czyli] Namiotu Zgromadzenia. I synowie Izraela zrobili wszystko, jak PAN rozkazał Mojżeszowi; tak zrobili.
33 Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
I przynieśli ten przybytek do Mojżesza, namiot i wszystkie naczynia do niego, jego haki, deski, drążki, słupy i podstawki;
34 kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
Przykrycie ze skór baranich farbowanych na czerwono, przykrycie ze skór borsuczych i zasłonę do osłonięcia;
35 Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
Arkę świadectwa i drążki do niej, i przebłagalnię;
36 meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
Stół, wszystkie naczynia do niego i chleb pokładny;
37 kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
Szczerozłoty świecznik, lampy do niego – lampy ustawione w porządku – i wszystkie naczynia do niego, i oliwę do świecenia;
38 madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
Także złoty ołtarz, olejek do namaszczania, wonne kadzidło i zasłonę do wejścia do namiotu;
39 madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
Miedziany ołtarz i do niego miedzianą kratę, drążki i wszystkie naczynia do niego, kadź i podstawę do niej.
40 mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
Zasłony do dziedzińca, słupy i podstawki do niego, zasłonę do bramy dziedzińca, sznury i kołki do niej i wszelkie naczynia do służby w przybytku, [czyli] do Namiotu Zgromadzenia;
41 na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
Szaty do służby w posługiwaniu w świątyni, święte szaty dla kapłana Aarona i szaty jego synów do sprawowania urzędu kapłańskiego.
42 Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
Według wszystkiego, co PAN rozkazał Mojżeszowi, tak synowie Izraela wykonali całą tę pracę.
43 Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.
I Mojżesz obejrzał tę całą robotę, a zrobili ją, jak PAN rozkazał; tak właśnie zrobili. I Mojżesz im błogosławił.

< Kutoka 39 >