< Kutoka 38 >

1 Akatengeneza madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa mbao za mti wa mshita, kimo chake dhiraa tatu; nayo ilikuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wa dhiraa tano
Och han gjorde bränneoffersaltaret af furoträ, fem alnar långt och bredt, rätt fyrakant, och tre alnar högt;
2 Akatengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu zikawa zimeungana, akafunika madhabahu kwa shaba.
Och gjorde fyra horn, som utgingo af fyra hörnen, och öfverdrog dem med koppar;
3 Akatengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama na vyombo vya kuchukulia moto.
Och gjorde allahanda redskap till altaret, tråg, skoflar, bäcken, eldgafflar, kolpannor; allt af koppar;
4 Akatengeneza wavu wa shaba chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
Och gjorde på altaret ett galler, såsom ett nät omkring, af koppar, ifrå nedan uppåt, intill halfväges på altaret;
5 Akasubu pete za shaba za kushikilia ile mipiko kwa ajili ya zile pembe nne za huo wavu wa shaba.
Och göt fyra ringar på de fyra hörnen af koppargallret till stängerna.
6 Akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuifunika kwa shaba.
Dem gjorde han af furoträ, och öfverdrog dem med koppar;
7 Akaiingiza ile mipiko kwenye zile pete, ili iwe pande mbili za madhabahu kwa ajili ya kuibeba. Akaitengeneza madhabahu yenye uvungu ndani yake akitumia mbao.
Och satte dem in uti ringarna på sidone af altaret, att man bar det dermed; och gjorde det ihålt;
8 Akatengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kutoka kwa vioo vya shaba vilivyotolewa na wanawake waliohudumu pale ingilio la Hema la Kukutania.
Och gjorde tvättekaret af koppar, och dess fot ock af koppar, tvärtemot härarna, som för dörrene af vittnesbördsens tabernakel lågo.
9 Kisha akatengeneza ua. Upande wa kusini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na ulikuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
Och gjorde han en gård, på södra sidone en bonad, hundrade alnar lång, af tvinnadt hvitt silke;
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Med hans tjugu stolpar och tjugu fötter af koppar; men deras knappar och gjordar af silfver;
11 Upande wa kaskazini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Sammalunda ock på norra sidone hundrade alnar, med tjugu stolpar och tjugu fötter af koppar; men deras knappar och gjordar af silfver;
12 Upande wa mwisho wa magharibi ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini na ulikuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
På vestra sidone femtio alnar, med tio stolpar och tio fötter; men deras knappar och gjordar af silfver;
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, pia ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini.
På östra sidone femtio alnar;
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
Femton alnar på hvarjo sidone vid porten af gårdenom; ju med tre stolpar, och tre fötter;
15 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mwingine wa ingilio la ua, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
Så att aller bonaden till gården var af tvinnadt hvitt silke;
16 Mapazia yote yaliyozunguka ua yalikuwa ya kitani iliyosokotwa vizuri.
Och fötterna till stolparna af koppar, och deras knappar och gjordar af silfver; så att deras knappar voro öfverdragne med silfver.
17 Vitako vya nguzo vilikuwa vya shaba. Kulabu na tepe juu ya nguzo zilikuwa za fedha, na ncha zake zilifunikwa kwa fedha. Kwa hiyo nguzo zote za ua zilikuwa na tepe za fedha.
Men deras gjordar voro af silfver på alla stolparna i gården.
18 Pazia la ingilio la ua lilikuwa la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini kama zile za kwenye ua, na kimo chake kilikuwa dhiraa tano,
Och klädet till ingången på gårdenom gjorde han stickadt af gult silke, skarlakan, rosenrödt, och tvinnadt hvitt silke; tjugu alnar långt, och fem alnar högt, efter det mått, som bonaden var till gården;
19 likiwa na nguzo nne na vitako vinne vya shaba. Kulabu zake na tepe zake zilikuwa za fedha, na ncha zake zilikuwa zimefunikwa kwa fedha.
Dertill fyra stolpar och fyra fötter af koppar; och deras knappar af silfver, och deras knöpar öfverdragne; och deras gjordar af silfver.
20 Vigingi vyote vya maskani na vya ua ulioizunguka vilikuwa vya shaba.
Och alla pålarna till tabernaklet, och till gården allt omkring, voro af koppar.
21 Ifuatayo ni orodha ya vifaa vilivyotumika kwa ajili ya ujenzi wa maskani, maskani ya Ushuhuda, ambavyo vilitayarishwa na Walawi kama alivyoagiza Mose, chini ya usimamizi wa Ithamari, mwana wa kuhani Aroni.
Detta är nu summan af det, som vittnesbördsens tabernakel tillhörde, det förtäljdt är, såsom Mose sagt hade, till Leviternas Gudstjenst under Ithamars hand, som var Prestens Aarons son;
22 (Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, alifanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose,
Hvilket Bezaleel, Uri son, Hurs sons, af Juda slägte, gjorde, allt såsom Herren hade budit Mose;
23 akiwa pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, fundi stadi wa kutia nakshi, kubuni michoro, mtarizi kwa rangi ya buluu, ya zambarau, nyekundu na kitani safi.)
Och med honom Aholiab, Ahisamachs son, af Dans slägte, en mästare till snida, till virka och till sticka med gult silke, skarlakan, rosenrödt, och hvitt silke.
24 Jumla ya dhahabu iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa kwa ajili ya kazi ya mahali patakatifu ilikuwa na uzito wa talanta 29 na shekeli 730, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
Allt det guld, som förarbetadt vardt i detta hela helgedomens verk, det till veftoffer gifvet vardt, var nio och tjugu centener, sjuhundrade och tretio siklar, efter helgedomens sikel.
25 Fedha iliyopatikana kutokana na jumuiya ya watu waliohesabiwa ilikuwa yenye uzito wa talanta mia moja na shekeli 1,775, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
Men silfret, som kom ifrå menighetene, var hundrade centener; tusende, sjuhundrade fem och sjutio siklar, efter helgedomens sikel.
26 Kila mtu alitoa beka moja, ambayo ni sawa na nusu shekeli ya fedha, kwa kazi ya mahali patakatifu, kutoka kwa kila mtu aliyekuwa amehesabiwa mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi, ambao jumla yao walikuwa wanaume 603,550.
Så mång hufvud, så många halfva siklar, efter helgedomens sikel, af alla dem som räknade vordo, ifrå tjugu år och deröfver, sexhundradetusend, tretusend, femhundrade och femtio.
27 Talanta hizo 100 za fedha zilitumika kusubu vile vitako mia moja kwa ajili ya mahali patakatifu na pazia: vitako mia moja kwa talanta mia, yaani, talanta moja kwa kila kitako.
Utaf de hundrade centener silfver göt man fötterna till helgedomen, och fötterna till förlåten; hundrade fötter utaf hundrade centener, ju en centener till foten.
28 Akatumia zile shekeli hizo 1,775 kutengeneza kulabu za nguzo, kufunika ncha za nguzo na kutengeneza vitanzi vyake.
Men utaf de tusend, sjuhundrade och fem och sjutio siklar, vordo gjorde knapparna till stolparna; och deras knöpar öfverdragne, och deras gjordar.
29 Shaba iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa ilikuwa na uzito wa talanta 70 na shekeli 2,400.
Veftoffret af koppar var sjutio centener; tutusend och fyrahundrade siklar.
30 Akaitumia hiyo shaba kutengeneza vitako vya ingilio la Hema la Kukutania, madhabahu ya shaba pamoja na ule wavu wake na vyombo vyake vyote,
Deraf vordo gjorde fötterna uti dörrene till vittnesbördsens tabernakel, och kopparaltaret, och koppargallret dertill; och all redskapen till altaret;
31 vile vitako vya ule ua uliozunguka na vile vya ingilio, na vigingi vyote vya Maskani pamoja na ule ua uliozunguka.
Dertill fötterna till gården allt omkring, och fötterna i ingången på gårdenom; alle pålarna till tabernaklet, och alle pålarna till gården allt omkring.

< Kutoka 38 >