< Kutoka 38 >

1 Akatengeneza madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa mbao za mti wa mshita, kimo chake dhiraa tatu; nayo ilikuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wa dhiraa tano
Bezalel made the altar for burnt offerings of acacia wood. It was five cubits long and five cubits wide—a square—and three cubits high.
2 Akatengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu zikawa zimeungana, akafunika madhabahu kwa shaba.
He made extensions of its four corners shaped like ox horns. The horns were made of one piece with the altar, and he covered it with bronze.
3 Akatengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama na vyombo vya kuchukulia moto.
He made all the equipment for the altar—pots for ashes, shovels, basins, meat forks, and firepans. He made all this equipment with bronze.
4 Akatengeneza wavu wa shaba chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
He made a grate for the altar, a network of bronze to be placed under the ledge, halfway down to the bottom.
5 Akasubu pete za shaba za kushikilia ile mipiko kwa ajili ya zile pembe nne za huo wavu wa shaba.
He cast four rings for the four corners of the bronze grate, as holders for the poles.
6 Akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuifunika kwa shaba.
Bezalel made poles of acacia wood and covered them with bronze.
7 Akaiingiza ile mipiko kwenye zile pete, ili iwe pande mbili za madhabahu kwa ajili ya kuibeba. Akaitengeneza madhabahu yenye uvungu ndani yake akitumia mbao.
He put the poles through the rings on the sides of the altar, to carry it. He made the altar hollow, out of planks.
8 Akatengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kutoka kwa vioo vya shaba vilivyotolewa na wanawake waliohudumu pale ingilio la Hema la Kukutania.
Bezalel made the large bronze basin with a bronze stand. He made the basin out of mirrors belonging to the women who served at the entrance to the tent of meeting.
9 Kisha akatengeneza ua. Upande wa kusini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na ulikuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
He also made the courtyard. The hangings on the south side of the courtyard were of fine linen, one hundred cubits long.
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
The hangings had twenty posts, with twenty bronze bases. There were hooks attached to the posts, as well as silver rods.
11 Upande wa kaskazini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Likewise along the north side, there were hangings one hundred cubits long with twenty posts, twenty bronze bases, hooks attached to the posts, and silver rods.
12 Upande wa mwisho wa magharibi ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini na ulikuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
The hangings of the west side were fifty cubits long, with ten posts and bases. The hooks and rods of the posts were silver.
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, pia ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini.
The courtyard was also fifty cubits long on the east side.
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
The hangings for one side of the entrance were fifteen cubits long. They had three posts with three bases.
15 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mwingine wa ingilio la ua, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
On the other side of the entrance of the courtyard were also hangings fifteen cubits long, with three posts and three bases.
16 Mapazia yote yaliyozunguka ua yalikuwa ya kitani iliyosokotwa vizuri.
All the hangings around the courtyard were made of fine linen.
17 Vitako vya nguzo vilikuwa vya shaba. Kulabu na tepe juu ya nguzo zilikuwa za fedha, na ncha zake zilifunikwa kwa fedha. Kwa hiyo nguzo zote za ua zilikuwa na tepe za fedha.
The bases for the posts were made of bronze. The hooks and rods for the posts were made of silver, and the covering for the tops of the posts was also made of silver. All the courtyard posts were covered with silver.
18 Pazia la ingilio la ua lilikuwa la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini kama zile za kwenye ua, na kimo chake kilikuwa dhiraa tano,
The curtain at the courtyard gate was twenty cubits long. The curtain was made of blue, purple, and scarlet linen, fine twined linen, and was twenty cubits long. It was twenty cubits in length and five cubits in height, like the courtyard curtains.
19 likiwa na nguzo nne na vitako vinne vya shaba. Kulabu zake na tepe zake zilikuwa za fedha, na ncha zake zilikuwa zimefunikwa kwa fedha.
It had four bronze bases and silver hooks. The covering for their tops and its rods were made of silver.
20 Vigingi vyote vya maskani na vya ua ulioizunguka vilikuwa vya shaba.
All the tent pegs for the tabernacle and courtyard were made of bronze.
21 Ifuatayo ni orodha ya vifaa vilivyotumika kwa ajili ya ujenzi wa maskani, maskani ya Ushuhuda, ambavyo vilitayarishwa na Walawi kama alivyoagiza Mose, chini ya usimamizi wa Ithamari, mwana wa kuhani Aroni.
This is the inventory of the tabernacle, the tabernacle of the covenant decrees, as it was taken following Moses' instructions. It was the work of the Levites under the direction of Ithamar son of Aaron the priest.
22 (Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, alifanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose,
Bezalel son of Uri son of Hur, from the tribe of Judah, made everything that Yahweh had commanded Moses.
23 akiwa pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, fundi stadi wa kutia nakshi, kubuni michoro, mtarizi kwa rangi ya buluu, ya zambarau, nyekundu na kitani safi.)
Oholiab son of Ahisamak, from the tribe of Dan, worked with Bezalel as an engraver, as a skillful workman, and as an embroiderer in blue, purple, and scarlet wool, and in fine linen.
24 Jumla ya dhahabu iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa kwa ajili ya kazi ya mahali patakatifu ilikuwa na uzito wa talanta 29 na shekeli 730, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
All the gold that was used for the project, in all the work connected with the holy place—the gold from the wave offering—was twenty-nine talents and 730 shekels, measured by the standard of the sanctuary shekel.
25 Fedha iliyopatikana kutokana na jumuiya ya watu waliohesabiwa ilikuwa yenye uzito wa talanta mia moja na shekeli 1,775, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
The silver given by the community weighed one hundred talents and 1,775 shekels, according to the sanctuary shekel,
26 Kila mtu alitoa beka moja, ambayo ni sawa na nusu shekeli ya fedha, kwa kazi ya mahali patakatifu, kutoka kwa kila mtu aliyekuwa amehesabiwa mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi, ambao jumla yao walikuwa wanaume 603,550.
or one beka per man, which is half a shekel, measured by the sanctuary shekel. This figure was reached on the basis of every person who was counted in the census, those twenty years old and older—603,550 men in all.
27 Talanta hizo 100 za fedha zilitumika kusubu vile vitako mia moja kwa ajili ya mahali patakatifu na pazia: vitako mia moja kwa talanta mia, yaani, talanta moja kwa kila kitako.
One hundred talents of silver were cast for the bases of the holy place and the curtain's bases—one hundred bases, one talent for each base.
28 Akatumia zile shekeli hizo 1,775 kutengeneza kulabu za nguzo, kufunika ncha za nguzo na kutengeneza vitanzi vyake.
With the remaining 1,775 shekels of silver, Bezalel made the hooks for the posts, covered the tops of the posts, and made the rods for them.
29 Shaba iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa ilikuwa na uzito wa talanta 70 na shekeli 2,400.
The bronze from wave offering weighed seventy talents and 2,400 shekels.
30 Akaitumia hiyo shaba kutengeneza vitako vya ingilio la Hema la Kukutania, madhabahu ya shaba pamoja na ule wavu wake na vyombo vyake vyote,
With this he made the bases for the entrance to the tent of meeting, the bronze altar, its bronze grate, all the equipment for the altar,
31 vile vitako vya ule ua uliozunguka na vile vya ingilio, na vigingi vyote vya Maskani pamoja na ule ua uliozunguka.
the bases for the courtyard, the bases for the courtyard entrance, all the tent pegs for the tabernacle, and all the tent pegs for the courtyard.

< Kutoka 38 >