< Kutoka 35 >

1 Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye:
Y Moisés envió a todos los hijos de Israel a que se unieran, y les dijo: Esto es lo que el Señor ha dicho y estas son sus órdenes.
2 Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe.
Seis días se trabajará, pero el séptimo día es un día santo para ustedes, un día de reposo para el Señor; cualquiera que haga algún trabajo en ese día será condenado a muerte.
3 Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”
No se encenderá fuego en ninguna de sus casas en el día de reposo.
4 Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru:
Y dijo Moisés a toda la congregación de los hijos de Israel: Este es el mandato que el Señor ha dado:
5 Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba;
Toma de entre ustedes una ofrenda al Señor; cualquiera que tenga la voluntad en su corazón, que dé su ofrenda al Señor; oro y plata y bronce;
6 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi;
Y tela azul, púrpura y rojo, y el mejor lino fino y cabello de cabras,
7 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
Y pieles de carnero de color rojo, y cuero, y madera de acacia,
8 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
Y aceite para las luces, y especias para el aceite sagrado de la unción y para él incienso aromático para quemar.
9 vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
Y piedras de ónice y las joyas para cortar para el efod y para él pectoral del sacerdote.
10 “Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru:
Y cada hombre de corazón sabio entre ustedes venga y haga lo que el Señor le haya ordenado;
11 Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako;
La casa y su tienda y su cubierta, sus ganchos y sus tablas, sus varillas y sus columnas y sus basas;
12 Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia;
El arca con sus varillas y él propiciatorio el velo colgando delante de ella;
13 meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho;
La mesa y sus varas, todos sus vasos, y el pan de la propiciación;
14 kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga;
Y el candelabro para las luces, con sus vasijas y sus lámparas y el aceite para la luz;
15 madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani;
Y el altar para la quema de especias, con sus varas, y el aceite sagrado de la unción y él incienso aromático, y la cortina para la puerta, a la puerta de la tienda;
16 madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake;
El altar de las ofrendas quemadas, con su enrejado de bronce, sus varas y todos sus utensilios, la palangana para lavar y su base;
17 pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua;
Las cortinas para él atrio, sus columnas y sus bases, y el telón para la entrada;
18 vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake;
Los estacas para la tienda, y las estacas para el atrio y sus cuerdas;
19 mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”
Las túnicas para ministrar en el lugar santo, las túnicas sagradas para el sacerdote Aarón, y las túnicas para sus hijos cuando actúan como sacerdotes.
20 Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose,
Y todos los hijos de Israel se apartaron de Moisés.
21 na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
Y a todos los que sintieron movidos de corazón, a todos los que se guiaron por el impulso de su espíritu, vinieron con su ofrenda para el Señor, para lo que fuera necesario para la Tienda de reunión y su obra y para las vestiduras sagradas.
22 Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Vinieron, hombres y mujeres, todos los que estaban dispuestos a dar, y dieron alfileres, narigueras, anillos de dedo y adornos para el cuello, todo de oro; todos dieron una ofrenda de oro al Señor.
23 Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta.
Y todos los que tenían tela azul, púrpura y rojo, y el mejor lino y pelo de cabra, y pieles de oveja de color rojo y cuero, se los dieron.
24 Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta.
Todos los que tenían plata y bronce les ofrecieron al Señor; y todos los que tenían madera de acacia, como la que se necesitaba para el trabajo, se la dieron.
25 Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi.
Y todas las mujeres que eran expertas con sus manos, hicieron telas, y dieron la obra de sus manos, tela azul, púrpura y rojo, y el mejor lino.
26 Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi.
Y aquellas mujeres que tenían el conocimiento, hicieron el cabello de las cabras en tela.
27 Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani.
Y los príncipes dieron piedras de ónice, y las joyas cortadas para el efod y el pectoral del sacerdote;
28 Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri.
Y la sal y el aceite para la luz, y el aceite santo para la unción y él incienso aromático.
29 Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.
Los hijos de Israel, cada hombre y cada mujer, por el impulso de sus corazones, dieron sus ofrendas libremente al Señor por la obra que el Señor le había ordenado a Moisés que hiciera.
30 Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
Y Moisés dijo a los hijos de Israel: He aquí que el SEÑOR designó a Bezaleel, hijo de Uri, hijo de Hur, de la tribu de Judá;
31 naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
Y lo ha llenado del espíritu de Dios, en toda sabiduría, conocimiento y arte de todo tipo;
32 ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
Como diseñador experto de cosas bellas, trabajando en oro, plata y bronce;
33 kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza.
Entrenado en el corte de piedras y el adorno de la madera y en todo tipo de trabajos manuales.
34 Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine.
Y le dio a él, y a Aholiab, hijo de Ahisamac, de la tribu de Dan, el poder de entrenar a otros.
35 Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.
A ellos les ha dado conocimiento de todas las artes del artesano, del diseñador y del obrero experto; del fabricante de bordado en tela azul, púrpura y rojo y el mejor lino y del fabricante de telas; son capacitados en todas las artes del diseñador y el obrero entrenado.

< Kutoka 35 >