< Kutoka 35 >

1 Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye:
Moses assembled all the community of the Israelites and said to them, “These are the things that Yahweh has commanded you to do.
2 Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe.
On six days work may be done, but for you, the seventh day must be a holy day, a Sabbath day of complete rest, holy to Yahweh. Whoever does any work on that day must be put to death.
3 Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”
You must not light a fire in any of your homes on the Sabbath day.”
4 Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru:
Moses spoke to all the community of the Israelites, saying, “This is the thing that Yahweh commanded.
5 Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba;
Take an offering for Yahweh, all of you who have a willing heart. Bring an offering to Yahweh—gold, silver, bronze,
6 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi;
blue, purple, and scarlet wool and fine linen; goats' hair;
7 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
ram skins dyed red and sea cow hides; acacia wood;
8 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
oil for the sanctuary lamps, spices for the anointing oil and the fragrant incense,
9 vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
onyx stones and other precious stones to be set for the ephod and breastpiece.
10 “Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru:
Every skilled man among you is to come and make everything that Yahweh has commanded—
11 Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako;
the tabernacle with its tent, its covering, its clasps, frames, bars, posts, and bases;
12 Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia;
also the ark with its poles, the atonement lid, and the curtain to conceal it.
13 meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho;
They brought the table with its poles, all its utensils, and the bread of the presence;
14 kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga;
the lampstand for the lights, with its accessories, its lamps, and the oil for the lamps;
15 madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani;
the incense altar with its poles, the anointing oil and the fragrant incense; the hanging for the tabernacle entrance;
16 madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake;
the altar for burnt offerings with its bronze grate and its poles and utensils; and the large basin with its base.
17 pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua;
They brought the hangings for the courtyard with its posts and bases, and the curtain for the courtyard entrance;
18 vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake;
and the tent pegs for the tabernacle and courtyard, together with their ropes.
19 mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”
They brought the finely-woven garments for serving in the holy place, the holy garments for Aaron the priest and his sons, for them to serve as priests.”
20 Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose,
Then all the tribes of Israel left and went away from Moses's presence.
21 na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
Everyone whose heart stirred him up and whom his spirit made willing came and brought an offering to Yahweh for the construction of the tabernacle, for all the items of service in it, and for the holy garments.
22 Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
They came, both men and women, all who had a willing heart. They brought brooches, earrings, rings, and ornaments, all kinds of gold jewelry. They all presented offerings of gold as a wave offering to Yahweh.
23 Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta.
Everyone who had blue, purple, or scarlet wool, fine linen, goat hair, ram skins dyed red, or sea cow skins brought them.
24 Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta.
Everyone making an offering of silver or bronze brought it as an offering to Yahweh, and everyone who had acacia wood for any use in the work brought it.
25 Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi.
Every skilled woman spun wool with her hands and brought what she had spun—blue, purple, or scarlet wool, or fine linen.
26 Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi.
All the women whose hearts stirred them up and who had skill spun goats' hair.
27 Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani.
The leaders brought onyx stones and other gems to be set into the ephod and the breastpiece;
28 Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri.
they brought spices and oil for the lamps, for the anointing oil, and for the fragrant incense.
29 Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.
The Israelites brought a freewill offering to Yahweh; every man and woman whose heart was willing brought materials for all the work that Yahweh had commanded through Moses to be made.
30 Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
Moses said to the Israelites, “See, Yahweh has called by name on Bezalel son of Uri son of Hur, from the tribe of Judah.
31 naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
He has filled Bezalel with his Spirit, to give him wisdom, understanding, and knowledge, for all kinds of craftsmanship,
32 ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
to make artistic designs and to work in gold, silver, and bronze;
33 kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza.
also to cut and set stones and to carve wood—to do all kinds of design and craftsmanship.
34 Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine.
He has put it in his heart to teach, both he and Oholiab son of Ahisamak, from the tribe of Dan.
35 Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.
He has filled them with skill to do all kinds of work, to work as craftsmen, as engravers, as embroiderers in blue, purple, and scarlet wool and fine linen, and as weavers. They are craftsmen in all sorts of work, and they are artistic designers.

< Kutoka 35 >