< Kutoka 35 >

1 Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye:
Moses assembled all the congregation of the children of Israel, and said to them, "These are the words which Jehovah has commanded, that you should do them.
2 Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe.
'Six days shall work be done, but on the seventh day there shall be a holy day for you, a Sabbath of solemn rest to Jehovah: whoever does any work in it shall be put to death.
3 Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”
You shall kindle no fire throughout your habitations on the Sabbath day.'"
4 Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru:
Moses spoke to all the congregation of the children of Israel, saying, "This is the thing which Jehovah commanded, saying,
5 Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba;
'Take from among you an offering to Jehovah. Whoever is of a willing heart, let him bring it, Jehovah's offering: gold, silver, bronze,
6 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi;
blue, purple, scarlet, fine linen, goats' hair,
7 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
rams' skins dyed red, sea cow hides, acacia wood,
8 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
oil for the light, spices for the anointing oil and for the sweet incense,
9 vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
onyx stones, and stones to be set for the ephod and for the breastplate.
10 “Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru:
"'Let every wise-hearted man among you come, and make all that Jehovah has commanded:
11 Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako;
the tabernacle, its outer covering, its roof, its clasps, its boards, its bars, its pillars, and its sockets;
12 Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia;
the ark, and its poles, the mercy seat, the curtain to screen it;
13 meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho;
the table with its poles and all its vessels, and the show bread;
14 kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga;
the lampstand also for the light, with its vessels, its lamps, and the oil for the light;
15 madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani;
and the altar of incense with its poles, the anointing oil, the sweet incense, the screen for the door, at the door of the tabernacle;
16 madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake;
the altar of burnt offering, with its grating of bronze, its poles, and all its vessels, the basin and its base;
17 pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua;
the hangings of the court, its pillars, their sockets, and the screen for the gate of the court;
18 vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake;
the pins of the tabernacle, the pins of the court, and their cords;
19 mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”
the finely worked garments, for ministering in the holy place, the holy garments for Aaron the priest, and the garments of his sons, to minister in the priest's office.'"
20 Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose,
All the congregation of the children of Israel departed from the presence of Moses.
21 na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
They came, everyone whose heart stirred him up, and everyone whom his spirit made willing, and brought Jehovah's offering, for the work of the Tent of Meeting, and for all of its service, and for the holy garments.
22 Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
They came, both men and women, as many as were willing-hearted, and brought brooches, earrings, signet rings, and armlets, all jewels of gold; even every man who offered an offering of gold to Jehovah.
23 Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta.
Everyone, with whom was found blue, purple, scarlet, fine linen, goats' hair, rams' skins dyed red, and sea cow hides, brought them.
24 Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta.
Everyone who did offer an offering of silver and bronze brought Jehovah's offering; and everyone, with whom was found acacia wood for any work of the service, brought it.
25 Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi.
All the women who were wise-hearted spun with their hands, and brought that which they had spun, the blue, the purple, the scarlet, and the fine linen.
26 Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi.
All the women whose heart stirred them up in wisdom spun the goats' hair.
27 Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani.
And the leaders brought the onyx stones, and the stones to be set, for the ephod and for the breastplate;
28 Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri.
and the spice, and the oil for the light, for the anointing oil, and for the sweet incense.
29 Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.
The children of Israel brought a freewill offering to Jehovah; every man and woman, whose heart made them willing to bring for all the work, which Jehovah had commanded to be made by Moses.
30 Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
Moses said to the children of Israel, "Look, God has called by name Bezalel the son of Uri, the son of Hur, of the tribe of Judah.
31 naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
He has filled him with the Spirit of God, in wisdom, in understanding, in knowledge, and in all manner of workmanship;
32 ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
and to make skillful works, to work in gold, in silver, in bronze,
33 kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza.
in cutting of stones for setting, and in carving of wood, to work in all kinds of skillful workmanship.
34 Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine.
He has put in his heart that he may teach, both he, and Oholiab, the son of Ahisamach, of the tribe of Dan.
35 Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.
He has filled them with wisdom of heart, to work all manner of workmanship, of the engraver, of the skillful workman, and of the embroiderer, in blue, in purple, in scarlet, and in fine linen, and of the weaver, even of those who do any workmanship, and of those who make skillful works.

< Kutoka 35 >