< Kutoka 34 >

1 Bwana akamwambia Mose, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitaandika juu yake maneno yale yaliyokuwa kwenye vile vibao vya kwanza, ulivyovivunja.
I reèe Gospod Mojsiju: isteši sebi dvije ploèe od kamena kao što su bile prve, da napišem na tijem ploèama rijeèi koje su bile na prvijem ploèama, koje si razbio.
2 Uwe tayari asubuhi, kisha upande juu ya Mlima Sinai. Uje mbele zangu kukutana nami huko juu ya mlima.
I budi gotov za sjutra da rano izaðeš na goru Sinajsku, i staneš preda me na vrh gore.
3 Mtu yeyote asije pamoja nawe, wala asionekane mtu popote juu ya mlima, wala kondoo na mbuzi au ngʼombe wasilishe karibu mbele ya huo mlima.”
Ali neka niko ne ide s tobom, i niko neka se ne pokaže na svoj gori, ni ovce ni goveda da ne pasu blizu gore.
4 Kwa hiyo Mose akachonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, naye akapanda juu ya Mlima Sinai asubuhi na mapema, kama Bwana alivyokuwa amemwagiza, akachukua vile vibao viwili vya mawe mikononi mwake.
I istesa Mojsije dvije ploèe od kamena kao što su bile prve, i ustavši rano izaðe na goru Sinajsku, kao što mu zapovjedi Gospod, i uze u ruku svoju dvije ploèe kamene.
5 Kisha Bwana akashuka katika wingu akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina lake, Bwana.
A Gospod siðe u oblaku, i stade ondje s njim, i povika po imenu: Gospod.
6 Bwana akapita mbele ya Mose, akitangaza, “Bwana, Bwana, Mungu mwenye huruma na neema, asiye mwepesi wa hasira, mwingi wa upendo na uaminifu,
Jer prolazeæi Gospod ispred njega vikaše: Gospod, Gospod, Bog milostiv, žalostiv, spor na gnjev i obilan milosrðem i istinom.
7 akidumisha upendo kwa maelfu, pia akisamehe uovu, uasi na dhambi. Lakini haachi kuadhibu mwenye hatia; huwaadhibu watoto na watoto wao kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata katika kizazi cha tatu na cha nne.”
Koji èuva milost tisuæama, prašta bezakonja i nepravde i grijehe, koji ne pravda krivoga, i pohodi grijehe otaèke na sinovima i na unucima do treæega i èetvrtoga koljena.
8 Mara Mose akasujudu na kuabudu.
A Mojsije brže savi glavu do zemlje i pokloni se,
9 Mose akasema, “Ee Bwana, kama nimepata kibali mbele zako, basi Bwana uende pamoja nasi. Ingawa watu hawa ni wenye shingo ngumu, samehe uovu wetu na dhambi yetu, tuchukue kuwa urithi wako.”
I reèe: ako sam našao milost pred tobom, Gospode, neka ide Gospod posred nas, jer je narod tvrdovrat; i oprosti nam bezakonje naše i grijeh naš, i uzmi nas za našljedstvo.
10 Kisha Bwana akasema: “Tazama ninafanya Agano mbele ya watu wako wote. Mbele ya watu wako wote nitafanya maajabu ambayo hayajafanyika katika taifa lolote katika ulimwengu wote. Watu wale mnaoishi miongoni mwao wataona jinsi ilivyo ya kushangaza ile kazi nitakayowafanyia mimi Bwana wenu.
A on reèe: evo postavljam zavjet; pred cijelim narodom tvojim uèiniæu èudesa, koja nijesu uèinjena nigdje na zemlji ni u kom narodu, i vidjeæete djelo Gospodnje sav narod, meðu kojim si, jer æe biti strašno što æu ja uèiniti s tobom.
11 Tii yale ninayokuamuru leo. Tazama nawafukuza mbele yako Waamori, Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Drži što ti danas zapovjedam; evo, ja æu izagnati ispred tebe Amoreje i Hananeje i Heteje i Ferezeje i Jeveje i Jevuseje.
12 Uwe mwangalifu, usifanye agano na wale wanaokaa katika nchi ile unayoiendea, la sivyo watakuwa mtego katikati yako.
Èuvaj se da ne hvataš vjere s onima koji žive u zemlji u koju æeš doæi, da ti ne budu zamka usred tebe.
13 Bomoa madhabahu yao, vunja mawe yao ya kuabudia na ukatekate nguzo zao za Ashera.
Nego oltare njihove oborite, i likove njihove izlomite, i gajeve njihove isijecite.
14 Usiabudu mungu mwingine, kwa kuwa Bwana, ambaye jina lake ni Wivu, ni Mungu mwenye wivu.
Jer ne valja da se klanjaš drugomu bogu: jer se Gospod zove revnitelj, Bog je revnitelj.
15 “Uwe mwangalifu usifanye agano na wale watu wanaoishi katika nchi, kwa maana wakati wanapojifanyia ukahaba kwa miungu yao na kuwatolea kafara, watakualika wewe nawe utakula sadaka za matambiko yao.
Nemoj hvatati vjere s onima koji žive u onoj zemlji, da ne bi èineæi preljubu za bogovima svojim i prinoseæi žrtvu bogovima svojim pozvali te, i ti jeo žrtve njihove.
16 Unapowachagua baadhi ya binti zao kuwa wake wa wana wenu na binti hao wakajifanyia ukahaba kwa miungu yao, watawaongoza wana wenu kufanya vivyo hivyo.
I da ne bi kæerima njihovijem ženio sinove svoje, i da ne bi kæeri njihove èineæi preljubu za bogovima svojim uèinile da sinovi tvoji èine preljubu za bogovima njihovijem.
17 “Usijifanyie sanamu za kusubu.
Livenih bogova ne gradi sebi.
18 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, kama nilivyokuamuru. Fanya hivi kwa wakati ulioamriwa, katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa kuwa katika mwezi huo ndipo wewe ulipotoka Misri.
Praznik prijesnijeh hljebova drži; sedam dana jedi prijesne hljebove, kao što sam ti zapovjedio, na vrijeme, mjeseca Aviva, jer si toga mjeseca izašao iz Misira.
19 “Mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo ni mali yangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza wote wa kiume wa mifugo yako, ikiwa ni wa ngʼombe au wa kondoo au mbuzi.
Sve što otvora matericu moje je, i svako muško u stoci tvojoj što otvora matericu, goveèe ili sitna stoka.
20 Utakomboa mzaliwa wa kwanza wa punda kwa mwana-kondoo, lakini kama humkomboi, utavunja shingo yake. Utakomboa wazaliwa wako wa kwanza wote wa kiume. “Mtu yeyote asije mbele zangu mikono mitupu.
Ali magare koje otvori matericu otkupi jagnjetom ili jaretom; ako li ga ne bi otkupio, slomi mu vrat; i svakoga prvenca izmeðu sinova svojih otkupi; i da se niko ne pokaže prazan preda mnom.
21 “Kwa siku sita utafanya kazi, lakini siku ya saba utapumzika, hata ikiwa ni majira ya kulima au ya kuvuna lazima upumzike.
Šest dana radi, a u sedmi dan poèini, i od oranja i od žetve poèini.
22 “Utaadhimisha Sikukuu ya Majuma kwa malimbuko ya mavuno ya ngano, na Sikukuu ya Mavuno mwishoni mwa mwaka.
Praznuj praznik sedmica, prvina žetve pšeniène, i praznik berbe na svršetku godine.
23 Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote watakuja mbele za Bwana Mwenyezi, Mungu wa Israeli.
Tri puta u godini da se svako muško izmeðu vas pokaže pred Gospodom Bogom Izrailjevim.
24 Nitawafukuza mataifa mbele yako na kupanua mipaka ya nchi yako, wala hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yako wakati unapokwenda mara tatu kila mwaka kuonana na Bwana Mungu wako.
Jer æu izagnati narode ispred tebe, i meðe tvoje raširiæu, i niko neæe poželjeti zemlje tvoje, kad staneš dolaziti da se pokažeš pred Gospodom Bogom svojim tri puta u godini.
25 “Usinitolee damu ya dhabihu pamoja na kitu chochote chenye chachu, wala usibakize dhabihu yoyote ya Sikukuu ya Pasaka mpaka asubuhi.
Nemoj prinositi krvi od žrtve moje uz hljebove kisele, i da ne prenoæi do jutra žrtva praznika pashe.
26 “Leta matunda ya kwanza yaliyo bora zaidi ya ardhi yako katika nyumba ya Bwana Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”
Prvine od prvoga roda zemlje svoje donesi u kuæu Gospoda Boga svojega; nemoj kuhati jareta u mlijeku majke njegove.
27 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Andika maneno haya, kwa maana kulingana na maneno haya, nimefanya Agano na wewe pamoja na Israeli.”
I reèe Gospod Mojsiju: napiši sebi te rijeèi; jer po tijem rijeèima uèinih zavjet s tobom i s Izrailjem.
28 Mose alikuwa huko pamoja na Bwana kwa siku arobaini usiku na mchana bila kula chakula wala kunywa maji. Naye akaandika juu ya vibao maneno ya Agano, yaani zile Amri Kumi.
I Mojsije osta ondje kod Gospoda èetrdeset dana i èetrdeset noæi, hljeba ne jeduæi ni vode pijuæi; i napisa Gospod na ploèe rijeèi zavjeta, deset rijeèi.
29 Mose alipoteremka kutoka Mlima Sinai akiwa na vile vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake, hakujua kuwa uso wake ulikuwa ukingʼaa, kwa sababu alikuwa amezungumza na Bwana.
I kad Mojsije slažaše s gore Sinajske, i držaše u ruci dvije ploèe svjedoèanstva slazeæi s gore, ne znaðaše da mu koža na licu posta svijetla dokle govoraše s njim.
30 Aroni na Waisraeli wote walipomwona Mose, kuwa uso wake unangʼaa, waliogopa kumkaribia.
I vidje Aron i svi sinovi Izrailjevi Mojsija, a to mu se svijetli koža na licu, i ne smješe pristupiti k njemu.
31 Lakini Mose akawaita, kwa hiyo Aroni na viongozi wote wa jumuiya wakarudi, naye akazungumza nao.
Ali ih zovnu Mojsije, i vratiše se k njemu Aron i svi glavari u zboru, i govori s njima Mojsije.
32 Baadaye Waisraeli wote wakamkaribia, naye akawapa amri zote Bwana alizompa katika Mlima wa Sinai.
Potom pristupiše svi sinovi Izrailjevi, i zapovjedi im sve što mu kaza Gospod na gori Sinajskoj.
33 Mose alipomaliza kuzungumza nao, akaweka utaji kwenye uso wake.
A kad im Mojsije izgovori, zastrije lice svoje pokrivalom.
34 Lakini kila wakati Mose alipoingia mbele za Bwana kuzungumza naye, aliondoa ule utaji mpaka alipotoka nje. Naye alipotoka nje na kuwaambia Waisraeli lile ambalo ameagizwa,
Ali kad Mojsije dolažaše pred Gospoda da s njim govori, skidaše pokrivalo dokle ne bi izašao; a izašavši kazivaše sinovima Izrailjevijem što mu se zapovjedaše.
35 waliona kuwa uso wake unangʼaa. Kisha Mose angeliweka tena utaji juu ya uso wake mpaka alipokwenda kuzungumza na Bwana.
Tada viðahu sinovi Izrailjevi lice Mojsijevo, gdje se svijetli koža na licu njegovu, te Mojsije opet zastiraše pokrivalom lice svoje dokle ne bi opet ušao da govori s njim.

< Kutoka 34 >