< Kutoka 31 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
L'Éternel parla aussi à Moïse, en disant:
2 “Tazama, nimemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
Vois, j'ai appelé par son nom Betsaléel, fils d'Uri, fils de Hur, de la tribu de Juda;
3 nami nimemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
Et je l'ai rempli de l'esprit de Dieu, en intelligence, en industrie et en science, et pour toutes sortes d'ouvrages;
4 ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
Pour faire des inventions, pour travailler l'or, l'argent et l'airain,
5 kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi.
Pour tailler et enchâsser des pierreries, pour tailler le bois et exécuter toutes sortes d'ouvrages.
6 Tena nimemteua Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, ili kumsaidia. Pia mafundi wote nimewapa ustadi wa kutengeneza kila kitu nilichokuamuru wewe:
Et voici, je lui ai donné pour compagnon Oholiab, fils d'Ahisamac, de la tribu de Dan; et j'ai mis de l'industrie dans le cœur de tout homme intelligent, afin qu'ils fassent tout ce que je t'ai commandé de faire:
7 Hema la Kukutania, Sanduku la Ushuhuda pamoja na kiti cha rehema juu yake, pia na vifaa vyote vya kwenye hema,
Le tabernacle d'assignation, l'arche pour le Témoignage et le propitiatoire qui sera dessus, et tous les ustensiles du tabernacle;
8 meza na vifaa vyake, kinara cha taa cha dhahabu safi na vifaa vyake vyote, madhabahu ya kufukizia uvumba,
La table et ses ustensiles, le chandelier d'or pur et tous ses ustensiles, l'autel du parfum,
9 madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, sinia na kinara chake,
L'autel de l'holocauste et tous ses ustensiles, la cuve et sa base;
10 pamoja na mavazi matakatifu yaliyofumwa ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe wakati wanahudumu katika kazi ya ukuhani,
Les vêtements du service, les vêtements sacrés pour Aaron le sacrificateur, et les vêtements de ses fils pour exercer la sacrificature;
11 pia mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri kwa ajili ya Mahali Patakatifu. Watavitengeneza sawasawa kama vile nilivyokuagiza wewe.”
L'huile de l'onction, et le parfum d'aromates pour le sanctuaire. Ils feront selon tout ce que je t'ai commandé.
12 Kisha Bwana akamwambia Mose,
L'Éternel parla encore à Moïse, en disant:
13 “Waambie Waisraeli, ‘Ninyi ni lazima mzishike Sabato zangu. Hii itakuwa ni ishara kati yangu na ninyi kwa ajili ya vizazi vijavyo, ili mpate kujua kwamba Mimi Ndimi Bwana, niwafanyaye ninyi watakatifu.
Et toi, parle aux enfants d'Israël, et dis: Seulement, vous observerez mes sabbats. Car c'est un signe entre moi et vous, dans toutes vos générations, afin qu'on sache que c'est moi, l'Éternel, qui vous sanctifie.
14 “‘Mtaishika Sabato, kwa sababu ni takatifu kwenu. Yeyote atakayeinajisi lazima auawe, yeyote atakayefanya kazi siku hiyo lazima akafie mbali na watu wake.
Observez donc le sabbat; car c'est pour vous un jour saint. Ceux qui le profaneront seront punis de mort; si quelqu'un fait une œuvre en ce jour, cette personne-là sera retranchée du milieu de ses peuples.
15 Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba ni Sabato ya kupumzika, takatifu kwa Bwana. Yeyote afanyaye kazi yoyote siku ya Sabato ni lazima auawe.
On travaillera pendant six jours; mais, au septième jour, ce sera le sabbat du repos, consacré à l'Éternel; quiconque fera une œuvre le jour du sabbat, sera puni de mort.
16 Waisraeli wataishika Sabato, kuiadhimisha kwa vizazi vijavyo kuwa Agano la milele.
Ainsi les enfants d'Israël observeront le sabbat, pour célébrer le sabbat dans toutes leurs générations, comme une alliance perpétuelle.
17 Itakuwa ishara kati yangu na Waisraeli milele, kwa kuwa kwa muda wa siku sita Bwana aliumba mbingu na dunia, na siku ya saba akaacha kufanya kazi, akapumzika.’”
C'est un signe entre moi et les enfants d'Israël à perpétuité; car l'Éternel a fait en six jours les cieux et la terre, mais au septième jour il a cessé et s'est reposé.
18 Bwana alipomaliza kusema na Mose juu ya Mlima Sinai, Mungu akampa vile vibao viwili vya Ushuhuda, vibao vya mawe vilivyoandikwa kwa kidole cha Mungu.
Et quand Dieu eut achevé de parler avec Moïse, sur la montagne du Sinaï, il lui donna les deux tables du Témoignage, tables de pierre, écrites du doigt de Dieu.

< Kutoka 31 >