< Kutoka 28 >

1 “Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Fais aussi approcher de toi, d'entre les enfants d'Israël, Aaron ton frère, avec ses fils, pour exercer devant moi la sacrificature: Aaron, Nadab et Abihu, Éléazar et Ithamar, fils d'Aaron.
2 Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
Et tu feras à Aaron, ton frère, des vêtements sacrés, pour sa gloire et pour son ornement.
3 Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
Et tu parleras à tous ceux qui sont intelligents, que j'ai remplis d'un esprit de sagesse, et ils feront les vêtements d'Aaron pour le consacrer, pour qu'il exerce la sacrificature devant moi.
4 Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Et voici les vêtements qu'ils feront: Le pectoral, l'éphod, la robe, la tunique brodée, la tiare et la ceinture. Ils feront donc des vêtements sacrés à Aaron, ton frère, et à ses fils, pour qu'ils exercent devant moi la sacrificature.
5 Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
Et ils prendront de l'or, de la pourpre, de l'écarlate, du cramoisi et du fin lin.
6 “Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
Et ils feront l'éphod d'or, de pourpre, d'écarlate, de cramoisi et de fin lin retors, en ouvrage d'art.
7 Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
Il y aura à ses deux extrémités deux épaulettes qui se joindront; et c'est ainsi qu'il sera joint.
8 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
La ceinture pour l'attacher, qui se mettra par-dessus, sera du même ouvrage et de la même pièce; elle sera d'or, de pourpre, d'écarlate et de fin lin retors.
9 “Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
Et tu prendras deux pierres d'onyx, et tu graveras sur elles les noms des enfants d'Israël:
10 kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
Six de leurs noms sur une pierre, et les six autres noms sur la seconde pierre, d'après l'ordre de leurs naissances.
11 Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
Tu graveras sur les deux pierres, en travail de lapidaire, en gravure de cachet, les noms des enfants d'Israël; tu les enchâsseras dans des chatons d'or.
12 na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
Et tu mettras les deux pierres sur les épaulettes de l'éphod, comme des pierres de mémorial pour les enfants d'Israël; et Aaron portera leurs noms devant l'Éternel, sur ses deux épaules, en mémorial.
13 Tengeneza vijalizo vya dhahabu
Tu feras aussi des agrafes d'or,
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
Et deux chaînettes d'or pur, que tu tresseras en forme de cordons, et tu mettras dans les agrafes les chaînettes ainsi tressées.
15 “Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
Tu feras aussi le pectoral du jugement en ouvrage d'art; tu le feras comme l'ouvrage de l'éphod; tu le feras d'or, de pourpre, d'écarlate, de cramoisi et de fin lin retors.
16 Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
Il sera carré et double; sa longueur sera d'un empan, et sa largeur d'un empan.
17 Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
Et tu le garniras d'une garniture de pierreries à quatre rangs de pierres: au premier rang, une sardoine, une topaze et une émeraude;
18 katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
Au second rang une escarboucle, un saphir et une calcédoine;
19 safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
Au troisième rang, une opale, une agate et une améthyste;
20 na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
Et au quatrième rang, un chrysolithe, un onyx et un jaspe. Ces pierres seront enchâssées dans de l'or, dans leurs garnitures.
21 Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
Et les pierres, selon les noms des enfants d'Israël, seront au nombre de douze, d'après leurs noms; elles seront pour les douze tribus, chacune d'après son nom, en gravure de cachet.
22 “Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
Tu feras aussi, sur le pectoral, des chaînettes, tressées en forme de cordons, en or pur.
23 Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
Puis tu feras sur le pectoral deux anneaux d'or; et tu mettras les deux anneaux aux deux extrémités du pectoral.
24 Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
Et tu mettras les deux cordons d'or aux deux anneaux, aux extrémités du pectoral.
25 nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
Et tu mettras les deux bouts des deux cordons aux deux agrafes; et tu les mettras sur les épaulettes de l'éphod sur le devant.
26 Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
Tu feras aussi deux autres anneaux d'or, et tu les mettras sur les deux autres extrémités du pectoral, sur le bord qui sera du côté de l'éphod, en dedans.
27 Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
Et tu feras deux autres anneaux d'or, et tu les mettras aux deux épaulettes de l'éphod par le bas, sur le devant, à côté de l'endroit où il se joint, au-dessus de la ceinture de l'éphod.
28 Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
Et on attachera le pectoral par ses anneaux aux anneaux de l'éphod, avec un cordon de pourpre, afin qu'il tienne sur la ceinture de l'éphod, et que le pectoral ne se détache pas de l'éphod.
29 “Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
Ainsi Aaron portera les noms des enfants d'Israël, au pectoral du jugement, sur son cœur, quand il entrera dans le lieu saint, pour servir continuellement de mémorial devant l'Éternel.
30 Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
Et tu mettras sur le pectoral du jugement l'Urim et le Thummim, et ils seront sur le cœur d'Aaron quand il entrera devant l'Éternel; et Aaron portera le jugement des enfants d'Israël sur son cœur, devant l'Éternel, continuellement.
31 “Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
Tu feras aussi la robe de l'éphod, entièrement de pourpre.
32 na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
Et l'ouverture pour passer la tête sera au milieu; il y aura une bordure à son ouverture tout autour, d'ouvrage tissé, comme l'ouverture d'une cotte d'armes, afin qu'elle ne se déchire pas.
33 Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
Et tu mettras à ses bords des grenades de pourpre, d'écarlate, et de cramoisi, à ses bords, tout autour; et des clochettes d'or entremêlées, tout autour:
34 Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
Une clochette d'or et une grenade, une clochette d'or et une grenade, aux bords de la robe, tout autour.
35 Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
Or, Aaron en sera revêtu pour faire le service; et on en entendra le son, quand il entrera dans le lieu saint devant l'Éternel, et quand il en sortira; et il ne mourra point.
36 “Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
Tu feras aussi une lame d'or pur, sur laquelle tu graveras, en gravure de cachet: SAINTETÉ A L'ÉTERNEL.
37 Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
Tu la mettras sur un cordon de pourpre; elle sera sur la tiare, sur le devant de la tiare;
38 Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
Et elle sera sur le front d'Aaron; et Aaron portera les iniquités que les enfants d'Israël auront commises dans les saintes oblations qu'ils offriront, dans toutes leurs saintes offrandes; et elle sera sur son front continuellement, pour les rendre agréables devant l'Éternel.
39 “Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
Tu feras aussi la tunique en tissu de fin lin, et tu feras une tiare de fin lin; mais tu feras la ceinture en ouvrage de broderie.
40 Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
Tu feras aussi pour les fils d'Aaron des tuniques, des ceintures et des mitres pour leur gloire et pour leur ornement.
41 Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Et tu en revêtiras Aaron, ton frère, et ses fils avec lui; tu les oindras, tu les installeras, et tu les consacreras, afin qu'ils exercent la sacrificature devant moi.
42 “Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
Fais-leur aussi des caleçons de lin, pour couvrir leur nudité; qu'ils tiennent depuis les reins jusqu'aux cuisses.
43 Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.
Et Aaron et ses fils en seront revêtus quand ils entreront dans le tabernacle d'assignation, ou quand ils approcheront de l'autel, pour faire le service dans le lieu saint, et ils ne seront point coupables, et ne mourront point. C'est une ordonnance perpétuelle pour lui et pour sa postérité après lui.

< Kutoka 28 >