< Kutoka 27 >

1 “Jenga madhabahu ya mbao za mti wa mshita, kimo chake kiwe dhiraa tatu; itakuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano.
"You shall make the altar of acacia wood, eight feet seven inches long, and eight feet seven inches broad; the altar shall be foursquare: and its height shall be five feet two inches.
2 Tengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu ziwe zimeungana, na ufunike madhabahu kwa shaba.
You shall make its horns on its four corners; its horns shall be of one piece with it; and you shall overlay it with bronze.
3 Tengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama, na vyombo vya kuchukulia moto.
You shall make its pots to take away its ashes, its shovels, its basins, its flesh hooks, and its fire pans: all its vessels you shall make of bronze.
4 Kisha tengenezea hayo madhabahu wavu wa shaba, na utengeneze pete za shaba kwenye kila moja ya hizo pembe nne za huo wavu.
You shall make a grating for it of network of bronze: and on the net you shall make four bronze rings in its four corners.
5 Weka wavu huo chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
You shall put it under the ledge around the altar beneath, that the net may reach halfway up the altar.
6 Tengeneza mipiko ya mti wa mshita kwa ajili ya madhabahu, na uifunike kwa shaba.
You shall make poles for the altar, poles of acacia wood, and overlay them with bronze.
7 Hiyo mipiko itaingizwa kwenye zile pete ili iwe pande mbili za madhabahu inapobebwa.
Its poles shall be put into the rings, and the poles shall be on the two sides of the altar, when carrying it.
8 Tengeneza madhabahu yawe na uvungu ndani yake ukitumia mbao. Utaitengeneza sawasawa na vile ulivyoonyeshwa mlimani.
You shall make it with hollow planks. They shall make it as it has been shown you on the mountain.
9 “Tengeneza ua kwa ajili ya Hema la Kukutania. Upande wa kusini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na utakuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
"You shall make the court of the tabernacle: for the south side southward there shall be hangings for the court of fine twined linen one hundred seventy-two feet three inches long for one side:
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
and its pillars shall be thirty-four feet five inches, and their sockets twenty, of bronze; the hooks of the pillars and their fillets shall be of silver.
11 Upande wa kaskazini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, nao utakuwa na mapazia, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Likewise for the north side in length there shall be hangings one hundred seventy-two feet three inches, and its pillars thirty-four feet five inches, and their sockets thirty-four feet five inches, of bronze; the hooks of the pillars, and their fillets, of silver.
12 “Upande wa magharibi wa ua utakuwa na upana wa dhiraa hamsini, nao utakuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi.
For the breadth of the court on the west side shall be hangings of eighty-six feet one inch; their pillars seventeen feet three inches, and their sockets seventeen feet three inches.
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, ua pia utakuwa na upana wa dhiraa hamsini.
The breadth of the court on the east side eastward shall be eighty-six feet one inch.
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yatakuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
The hangings for the one side of the gate shall be twenty-five feet ten inches; their pillars five feet two inches, and their sockets five feet two inches.
15 Kutakuwepo tena na mapazia ya dhiraa kumi na tano kwa upande mwingine wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
For the other side shall be hangings of twenty-five feet ten inches; their pillars five feet two inches, and their sockets five feet two inches.
16 “Kuhusu ingilio la ua, weka pazia lenye urefu wa dhiraa ishirini la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo litashikiliwa na nguzo nne na vitako vinne.
For the gate of the court shall be a screen of thirty-four feet five inches, of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen, the work of the embroiderer; their pillars six feet eleven inches, and their sockets six feet eleven inches.
17 Nguzo zote zinazozunguka ua zitakuwa na tepe na kulabu za fedha, na vitako vya shaba.
All the pillars of the court around shall be filleted with silver; their hooks of silver, and their sockets of bronze.
18 Ua wa kukutania utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini, ukiwa na mapazia ya kitani yaliyosokotwa vizuri yenye urefu wa dhiraa tano kwenda juu na vitako vya shaba.
The length of the court shall be one hundred seventy-two feet three inches, and the breadth eighty-six feet one inch every where, and the height eight feet seven inches, of fine twined linen, and their sockets of bronze.
19 Vyombo vingine vyote vinavyotumika katika maskani kwa shughuli yoyote, pamoja na vigingi vyote na hata vile vya ua, vitakuwa vya shaba.
All the instruments of the tabernacle in all its service, and all its pins, and all the pins of the court, shall be of bronze.
20 “Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa kwa ajili ya mwanga ili zile taa ziwake mfululizo.
"You shall command the children of Israel, that they bring to you pure olive oil beaten for the light, to cause a lamp to burn continually.
21 Katika Hema la Kukutania, nje ya pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, Aroni na wanawe watahakikisha kuwa taa hizo zinawaka kuanzia jioni mpaka asubuhi mbele za Bwana. Hili litakuwa agizo la milele miongoni mwa Waisraeli kwa vizazi vyote vijavyo.
In the Tent of Meeting, outside the veil which is before the testimony, Aaron and his sons shall keep it in order from evening to morning before Jehovah: it shall be a statute forever throughout their generations on the behalf of the children of Israel.

< Kutoka 27 >