< Kutoka 26 >

1 “Tengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo.
Et tu feras le tabernacle de dix tapis de fin coton retors, et de bleu, et de pourpre, et d’écarlate; tu les feras avec des chérubins, d’ouvrage d’art.
2 Mapazia yote yatatoshana kwa ukubwa: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
La longueur d’un tapis sera de 28 coudées, et la largeur d’un tapis de quatre coudées: une même mesure pour tous les tapis.
3 Unganisha mapazia matano pamoja; fanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
Cinq tapis seront joints l’un à l’autre, et cinq tapis seront joints l’un à l’autre.
4 Tengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, na ufanye vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
Et tu feras des ganses de bleu sur le bord d’un tapis, à l’extrémité de l’assemblage; et tu feras de même au bord du tapis qui sera à l’extrémité dans le second assemblage.
5 Fanya vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vielekeane.
Tu feras 50 ganses à un tapis, et tu feras 50 ganses à l’extrémité du tapis qui est dans le second assemblage, les ganses seront vis-à-vis l’une de l’autre.
6 Kisha tengeneza vifungo hamsini vya dhahabu ili vitumike kufunga na kuunganisha mapazia pamoja kufanya Hema liwe kitu kimoja.
Et tu feras 50 agrafes d’or, et tu joindras les tapis l’un à l’autre par les agrafes, et ce sera un seul tabernacle.
7 “Tengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
Et tu feras des tapis de poil de chèvre pour une tente [qui sera] par-dessus le tabernacle; tu feras onze de ces tapis;
8 Mapazia hayo kumi na moja yatakuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
la longueur d’un tapis sera de 30 coudées, et la largeur d’un tapis de quatre coudées: une même mesure pour les onze tapis.
9 Unganisha hayo mapazia matano yawe fungu moja, na hayo mengine sita yawe fungu lingine. Kunja hilo pazia la sita mara mbili mbele ya maskani.
Et tu joindras cinq tapis à part, et six tapis à part; et tu replieras le sixième tapis sur le devant de la tente.
10 Tengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
Et tu feras 50 ganses sur le bord du tapis qui sera à l’extrémité de l’assemblage, et 50 ganses sur le bord du tapis du second assemblage.
11 Kisha tengeneza vifungo hamsini vya shaba, uviingize katika vile vitanzi ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
Et tu feras 50 agrafes d’airain, et tu feras entrer les agrafes dans les ganses; et tu assembleras la tente, et elle sera une.
12 Kuhusu kile kipande cha ziada cha pazia la Hema, nusu ya hilo pazia lililobaki litaningʼinizwa upande wa nyuma wa Hema.
Et ce qui pend, le surplus des tapis de la tente, la moitié du tapis, savoir le surplus, pendra sur le derrière du tabernacle;
13 Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika.
et la coudée deçà, et la coudée delà, qui est de surplus dans la longueur des tapis de la tente, pendront sur les côtés du tabernacle, deçà et delà, pour le couvrir.
14 Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
Et tu feras pour la tente une couverture de peaux de béliers teintes en rouge, et une couverture de peaux de taissons par-dessus.
15 “Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
Et tu feras les ais pour le tabernacle; ils seront de bois de sittim, [placés] debout;
16 Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi na upana wa dhiraa moja na nusu,
la longueur d’un ais sera de dix coudées, et la largeur d’un ais d’une coudée et demie.
17 zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
Il y aura deux tenons à un ais, en façon d’échelons, l’un répondant à l’autre; tu feras de même pour tous les ais du tabernacle.
18 Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
Et tu feras les ais pour le tabernacle, 20 ais pour le côté du midi vers le sud;
19 kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
et tu feras 40 bases d’argent sous les 20 ais, deux bases sous un ais pour ses deux tenons, et deux bases sous un ais pour ses deux tenons;
20 Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini
et pour l’autre côté du tabernacle, du côté du nord, 20 ais,
21 na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
et leurs 40 bases d’argent, deux bases sous un ais, et deux bases sous un ais.
22 Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
Et pour le fond du tabernacle, vers l’occident, tu feras six ais.
23 na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali.
Et tu feras deux ais pour les angles du tabernacle, au fond;
24 Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana.
ils seront joints par le bas, et parfaitement unis ensemble par le haut dans un anneau; il en sera de même pour les deux; ils seront aux deux angles.
25 Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
Et il y aura huit ais, et leurs bases d’argent: 16 bases, deux bases sous un ais, et deux bases sous un ais.
26 “Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
– Et tu feras des traverses de bois de sittim, cinq pour les ais d’un côté du tabernacle,
27 matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
et cinq traverses pour les ais de l’autre côté du tabernacle, et cinq traverses pour les ais du côté du tabernacle, pour le fond, vers l’occident;
28 Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
et la traverse du milieu sera au milieu des ais, courant d’un bout à l’autre.
29 Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.
Et tu plaqueras d’or les ais, et tu feras d’or leurs anneaux qui recevront les traverses, et tu plaqueras d’or les traverses.
30 “Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
Et tu dresseras le tabernacle selon son ordonnance qui t’a été montrée sur la montagne.
31 “Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia.
Et tu feras un voile de bleu, et de pourpre, et d’écarlate, et de fin coton retors; on le fera d’ouvrage d’art, avec des chérubins;
32 Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha.
et tu le mettras sur quatre piliers de [bois de] sittim, plaqués d’or, et leurs crochets seront d’or; ils seront sur quatre bases d’argent.
33 Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu.
Et tu mettras le voile au-dessous des agrafes, et tu mettras là, au-dedans du voile, l’arche du témoignage; et le voile fera séparation pour vous entre le lieu saint et le lieu très saint.
34 Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu.
Et tu mettras le propitiatoire sur l’arche du témoignage, dans le lieu très saint.
35 Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.
Et tu placeras la table en dehors du voile, et le chandelier vis-à-vis de la table, sur le côté du tabernacle qui est vers le sud, et tu mettras la table sur le côté nord.
36 “Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
Et tu feras pour l’entrée de la tente un rideau de bleu, et de pourpre, et d’écarlate, et de fin coton retors, en ouvrage de brodeur;
37 Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.
et tu feras pour le rideau cinq piliers de bois de sittim, et tu les plaqueras d’or, et leurs crochets seront d’or; et tu fondras pour eux cinq bases d’airain.

< Kutoka 26 >